Msaada kwanini natetemeka sana?



Unayosema ni kweli.
Upande wa wazazi hasa baba alikua mkali sana!
 

Hili ni tatizo kwa watu wengi sana nakumbuka nikiwa chuo kuna jamaa walikuwa wanatumia viroba ndio wanafanya presentation.
 
na ukiwa unapiga gemu dushelele nayo inavibrate au....
 
Hayo ndo yalimkuta Mh Mulugo. Unahitaji mazoezi ya kuongea na public, jitahidi kufanya mala kwa mala itaisha kadri unavyo panda jukwaani. Anza na idadi ndogo unaendelea isiwe mwoga.
 
Mkuu umesema vema.
Naomba huyu mleta mada ajiamini,ili uanze kujiamini anza kuzungumzia vitu ambavyo una uhakika navyo,punguza story za kusimuliwa ambazo hujui undani wake.Na kama unafanya presentation jijengee kujiamini hata kama ataingia mtu mwenye uelewa zaidi yako akilini mwako jijengee kuwa naye ni mwanafunzi wako,hii itakusaidia kujenga kujiamini.
Lkn ninkukumbushe jitahidi kuanza na vitu ambavyo una uhakika navyo kupunguza kuulizwa maswali ambayo hutakuwa na uwezo wa kkuyajibu na hivyo ikakuongezea hofu.
 
Hili ni tatizo kwa watu wengi sana nakumbuka nikiwa chuo kuna jamaa walikuwa wanatumia viroba ndio wanafanya presentation.

Hahahahahahaha! Mkuu, nimecheka sana--si unajua tena viroba vinaua soo?
 

Sijaelewa kama tatizo lako kuu ni hofu ya kuzungumza mbele za watu, na hivyo kutetemeka na kukosa pumzi au ni kutetemeka hata pale unapokuwa peke yako (e.g unajibu msg kwa simu au laptop). Kama ni hilo la kwanza with time na kwa kulifanyia mazoezi waweza kulimaliza, kwani ni kawaida ya wengi kuwa na hofu pale anapofanya presentation, hata kama ni mbele ya watu wachache (kuna exceptions za watu wanaozaliwa na uwezo wa kujieleza) na ndiyo maana watu wote makini (hata akina Obama) huwa wanafanya rehersal ya atakachokiwa. Zamani kwenye mashule ya sekondari kulikuwa na kitu kinaitwa debate clubs ambazo zilisaidia sana vijana kujifunza namna ya kujieleza na kujenga hoja. Hivyo ili uondokane na tatizo hilo ni lazima ujichanganye kwenye mijadala lakini anza na ile unayoielewa vizuri, kwani hofu hii huchangiwa pia na kutoijua/kutoimudu mada yako vizuri.Ni kama mtu anayeingia kwenye chumba cha mtihani akiwa amejiandaa vya kutosha atakuwa at easy as compared na ambaye hajajiandaa.
 
Tell yourself, "relax, you are good"
Take deep breath
 



Kumbuka Obama yeye hutoa tu hali ya mambo ilivyo lakini hakuna anayemuuliza papo hapo.
 

Hyo ni spirit ya hofu
Bila Mungu happ hutoki!

Kuna wakui happ walinga'ang'ana na Mungu wako ok!
 
hauna confidence ndugu jitahidi kuwa chaming na uwe una interaction za hapa na pale na marafiki walochangamka
 
nakumbuka jamaa alikunywa viroba badala atoe conclution akaanza tena introduction..

hahahahahahaaaaaaaaaaaaaa! mkuu usinivunje mbavu! hii kali sana i see! ni shidaaaaaaaaaaaaaaaaa!
 

Nakumbuka wakati nikiwa shule ya msingi nilikuwa nashindwa kabisa kusoma kitabu darasani hadi walimu wakawa wananishangaa wakati kwenye mitihani nilikuwa naongoza. Hili tatizo la kutoongea hadharani ni balaa!
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…