Msaada: Mbinu Kufukuza Nyoka mashambani

Msaada: Mbinu Kufukuza Nyoka mashambani

Wapendwa,
katika jitihada za kupambana na umaskini, nilichukua kakichaka ambako nakasafisha kwa ajili ya shamba na shughuli za ufugaji. Changamoto niliyokutana nayo ni kuwa:
1. Kuna vichaka vingi vinavyozunguka eneo hili kiasi kwamba hata nikisafisha bado majirani zangu wanabaki na vichaka
2. Eneo hili ni zuri sana lakini lina nyoka wengi.
Naomba kujua mbinu za kisayansi - chemicals, mimea ya kupanda kufukuza nyoka, etc ninazoweza kutumia ili niepukane na adha ya nyoka hawa.
Nitashukuru kupata michango iliyo makini.
Da pole Sana mkuu but kuna mti Wa mnyoka (Mnyonga Pembe ) hufanya kazi zifuatazo Kwanza hutoa harufu ambayo Adui Nyoka na kenge hufukuzwa yaan haishi mazingira hayo,pia husaidia kuponya Kama mtu kangatwa na nyoka au kutemewa mate kwa kusaga majani au magome na kumpaka haichukui muda kapona pia husaidia Kuku waliodumaa au wenye minyoo kuwaboost inshort nyoka hapatani na huu, unapadwa Kama muhogo either Kama Ua kuzunguunga nyumba au mipakani mwa shamba na kuuprune kuleta shape unapatikana Tanga nitafute whatsapp nikutumie picha kwa no 0788293736
 
kapandikize wadudu waoitwa sangara. ni aina ya siafu na wanaishi kwenye vishimo wanavojichimbia wenyewe ardhini. hawa wadudu ni dhahama kubwa sana kwa nyoka. popote walipo nyoka hakanyagi
Sehemu ambazo sangara wanaishi mimea hasa mazao huwa hayastawi, kwa hiyo atatua tatizo la nyoka ila ataleta tatizo kubwa zaidi la rutuba ktk udongo, nadhani maeneo Kisarawe Maneromango watakuwa wanalijua vizuri
 
Mkuu tafuta mti mmoja unaitwa Mnyonga pembe upo Kama mihogo unatoa harufu ambayo husaidia kufukuza nyoka ningepost picha uutafute upo tanga but simu aisapoti
 
Ya kweli haya?

Mzee mbona unanitisha nitaogopa kwenda shambani kwangu sasa
Yupo sahii sana ila uzur wa koboko hukaa mbali sana na watu yani huwa hapendi mechanical kelele. Kwake kelele humpandisha hasra so hukaaa mbali sana na sehem zenye kelele
Black mamba a.k.a koboko huwa anawika kama jogoo ni nyoka hatari zaidi maana yeye ukipita maeneo yake lazima akuue tofauti na wengine ambao mpaka aidha umkanyage au umguse. Anakawaida ya kukaa juu ya mti na kugonga kichwani, akikukosa atakukimbiza mpaka akupate ukiwahi kwenye gari hukaa chini ya gari na utatoka nae mbeya mpaka dar ukishuka tu game linaendelea baada ya half time. Ndo maana jamaa akasema hapo hawapo maana mtoa mada tayari angekua rip.
 
Hio niliona live kwenye documentary moja ya DWTV, Huyo nyoka alijificha chini ya prado aisee!
Mwanzo alionekana anavuka upande mmoja wa barabara kwenda mwingine mzungu akamuona metre kadhaa mbele akasimamisha gari ili amuache avuke, then akaendelea na safari ile anafika home si ndio kufungua mlango wa gari ashuke, hapo hapo akapokea sakramenti. Uzuri alikuwa na mkewe ndio hapo hapo akawasha gari tena kuelekea hospitali ya jirani kupata huduma dokta ndio akaambiwa angechelewa kidogo tu hata nusu saa asingetoboa!
Ndio maana biblia imeandika muwe werevu kama nyoka
 
Fuga paka wa kutosha.. 100% hutakuja kuona nyoka shambani mwako....
 
NDUGU YANGU TAFUTA MAFUTA YA MKIA WA KONDO CHANGANYA NA MCHANGA KISHA MWAGA KUZUNGUKA ENEO LOTE HUTAKAA UMUONE NYOKA WANAOGOPA SANA HIYO KITU
 
hio miti inachukua muda mpk kukua...wakati unasubiria miti ikue choma matairi kuzunguka eneo la shamba ikiwezekana pembe zote nne halafu usiyaondoe mabaki yaache hapo hapo wkt unasubiria miti ikue...fanya hivyo kwa kadri utakavyokua unapata muda ..husaidia sana maana ile harufu hua hawaipendi.
 
kapandikize wadudu waoitwa sangara. ni aina ya siafu na wanaishi kwenye vishimo wanavojichimbia wenyewe ardhini. hawa wadudu ni dhahama kubwa sana kwa nyoka. popote walipo nyoka hakanyagi
ulikuwa sahihi mkuu
 
Otesha miti inayotoa harufu wakat wa jion na asubuh hiyo itamaliza kabsa hlo tatizo..au vngnevyo uwe na destur ya kuchoma mpira au plastics mara kwa mara angalau utawapunguza
 
choma tairi shamba kaka, mi mwenyewe na hao reptiles mbalimbali
 
Hatua ya muda mfupi ni kunyunyizia diesel (au mafuta ya taa) kuzunguka eneo lako.
Unaweza kutumia sprayer kama hii hapa chini kwenye picha kunyunyizia diesel hiyo kuzunguka eneo lako.
Harufu ya diesel inawakera sana nyoka na wataenda mbali.
Ila itabidi urudie ku-spray kama mvua itanyesha, maana maji ya mvua yakapunguza harufu ya diesel.

Hand-Sprayer-NS-15A-.jpg
Vipi kwa kwenge? Inafanya kazi hii?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiboko yao ni OIL CHAFU KUZUNGUSHIA KWENYE MIPAKA YAKO.
 
black mamba akiachama kinywa chake ni cheusi but the body is green
Mkuu mpaka anaachanisha mdomo wake nimchunguze kama ni mweusi mimi nakuwa nasubili nini hapo???

Embu acha masikhara bwana,katika viumbe sitaki masikhara navyo ni hawa mabwana.
 
Kuna mti wa miiba mirefu mweupe, na majani membamba.; tunaita MWERERA unatoa harufu na ungaunga sio rafiki kwa nyoka. Hapa nilipo haipo ningetuma picha.
 
Back
Top Bottom