Msaada: Mke wangu hataki kusuka wala kununuliwa nguo nzuri

Msaada: Mke wangu hataki kusuka wala kununuliwa nguo nzuri

Wakuu habari. Nimeoa na nina mwaka na nusu wa ndoa sasa. Nina tatizo ambalo ninahitaji ushauri kwa wazoefu. Binafsi napenda mwanamke anaye pendeza na kujijali , na napenda awe mke wangu ili nisilazimike kutoka huko nje kuchepuka. Sasa nina mke wangu hapendi kusuka, yaani kichwani yupo rough, mara chache (mara moja kwa miezi
Huyo wa hivyo umempata wapi mbona sisi wanachama wa UWABATA tunawasaka saana na hatuwapati?
 
Mlipoanzisha mahusiano alikuwa hivo?
Je ana majukumu mengi?

Labda hapendi kusuka kwahio usimlazimishe ungemshauri akate hata style ya nywele fupi ila aziweke safi na madhubuti.

Kuhusu nguo mnunulie umletee au nenda nae shopping ajaribu umsifie akijaribu anapendeza n.k labda ana low self confidence so anajiona hapendezi na viwalo vya kisasa.Msifie kwamba anapendeza akivaa nguo dizain flani flani na unapenda ukimuona amevaa hivo.

Kuna uwezekano pia yeye anaona una gharimika angali yeye anataka aweke akiba au anafikiria future yenu...Ongea nae uelewe kwanini hataki kupendeza....
 
Ni watu wa Arusha tena mjini kabisa. Kipindi cha uchumba alikua akipendeza haswa sasa sijui ninini kimempata. inanitia simanzi
Mshauri tu kuhusu kunyoa low cut asifuge nywele Kama haziweki katka utaratibu
Kuhusu nguo angalia ile mikato yake anayopenda kuvaa wewe iboreshe kidogooo halafu muwekee mizani ipo siku atazipenda tuu

Kama UNO kitandani analimwaga na msosi anapika vizurii jua tu huyo ndio mke mkuu ukisema umwache huyo hakika kunakitu utakopata ambacho kitaa tunasema MWANA KULITAKA MWANA KULIFIND..

Wengine tumeoa wanawake ambao usasa umewazid kila wikend bata tupu msuko wa 70k kila wiki hadi unahisi kizunguzungu

KIFUPI MKUU UMEPATA JIKOO
 
Huyo ataka ufanye maendeleo kwanza, mwanamke anaekupenda hujinyima kwa baadh ya mambo na kumpa fursa ya kufanya maendeleo mtu wake, hata kama hajakueleza hili jiongeze, mwanamke mwenye akili akiwa ndoani hujivunia maendeleo na si kupendeza.
 
huyo ataka ufanye maendeleo kwanza, mwanamke anaekupenda hujinyima kwa baadh ya mambo na kumpa fursa ya kufanya maendeleo mtu wake, hata kama hajakueleza hili jiongeze, mwanamke mwenye akili akiwa ndoani hujivunia maendeleo na si kupendeza.
Ahsante sana mkuu
 
Hebu nipe namba yake nikusaidie kumshauri
Wakuu habari. Nimeoa na nina mwaka na nusu wa ndoa sasa. Nina tatizo ambalo ninahitaji ushauri kwa wazoefu. Binafsi napenda mwanamke anayependeza na kujijali , na napenda awe mke wangu ili nisilazimike kutoka huko nje
 
Wakuu habari. Nimeoa na nina mwaka na nusu wa ndoa sasa. Nina tatizo ambalo ninahitaji ushauri kwa wazoefu. Binafsi napenda mwanamke anayependeza na kujijali , na napenda awe mke wangu ili nisilazimike kutoka huko nje kuchepuka. Sasa nina mke wangu hapendi kusuka, yaani kichwani yupo rough, mara chache (mara moja kwa miezi minne hivi) ndio huwa anakubali kwenda saluni kusuka tena kwa ugomvi. Hela za saluni kila mwezi natenga elfu hamsini hadi sabini hivi (kwa uwezo wangu wa kipato) ila mtihani ni kumshawishi akubali. Mara kadhaa nimejikuta natembea na vibinti vinavyopendeza au vinavyokubali nivipendezeshe nje ila hili linanikwaza sana maana sipendi kumsaliti. hata kumtoa kwenda kununua nguo nzuri hataki mara nyingi. Nahitaji ushauri namfanyaje huyu mke wangu ili moyo wangu uweze kutulia. asanteni.
Wakuu habari. Nimeoa na nina mwaka na nusu wa ndoa sasa. Nina tatizo ambalo ninahitaji ushauri kwa wazoefu. Binafsi napenda mwanamke anayependeza na kujijali , na napenda awe mke wangu ili nisilazimike kutoka huko nje kuchepuka. Sasa nina mke wangu hapendi kusuka, yaani kichwani yupo rough, mara chache (mara moja kwa miezi minne hivi) ndio huwa anakubali kwenda saluni kusuka tena kwa ugomvi. Hela za saluni kila mwezi natenga elfu hamsini hadi sabini hivi (kwa uwe
Wakuu habari. Nimeoa na nina mwaka na nusu wa ndoa sasa. Nina tatizo ambalo ninahitaji ushauri kwa wazoefu. Binafsi napenda mwanamke anayependeza na kujijali , na napenda awe mke wangu ili nisilazimike kutoka huko nje kuchepuka. Sasa nina mke wangu hapendi kusuka, yaani kichwani yupo rough, mara chache (mara moja kwa miezi minne hivi) ndio huwa anakubali kwenda saluni kusuka tena kwa ugomvi. Hela za saluni kila mwezi natenga elfu hamsini hadi sabini hivi (kwa uwezo wangu wa kipato) ila mtihani ni kumshawishi akubali. Mara kadhaa nimejikuta natembea na vibinti vinavyopendeza au vinavyokubali nivipendezeshe nje ila hili linanikwaza sana maana sipendi kumsaliti. hata kumtoa kwenda kununua nguo nzuri hataki mara nyingi.

Nahitaji ushauri namfanyaje huyu mke wangu ili moyo wangu uweze kutulia.

asanteni.

zo wangu wa kipato) ila mtihani ni kumshawishi akubali. Mara kadhaa nimejikuta natembea na vibinti vinavyopendeza au vinavyokubali nivipendezeshe nje ila hili linanikwaza sana maana sipendi kumsaliti. hata kumtoa kwenda kununua nguo nzuri hataki mara nyingi. Nahitaji ushauri namfanyaje huyu mke wangu ili moyo wangu uweze kutulia. asanteni. [/QUOTE

Huyo mkeo yupo kati ya makundu haya:
1. Ameshagundua ww ni mchepukaji na unapitia mpaka wasusi na hivyo hawaamini wasije mloga kwa kupitia nywele zake
2. Inawezekana amepata uamsho wa imani yake ambayo inamuelekeza kusuka ni dhambi
3. Amesharidhika, maana alijipamba ili akupate...sasa ameshakupata ajipambe kwa sababu gani tena😂!...mpe sababu ya yeye kujipamba...ila usije kutulilia tena akiitiwa na wachepukaji kama ww akipendeza🤔!
4.....ongeza yako
 
Ni watu wa Arusha tena mjini kabisa. Kipindi cha uchumba alikua akipendeza haswa sasa sijui ninini kimempata. inanitia simanzi
Hahahah ushauziwa mbuzi kwenye gunia mzee 😂😂😂! Hapa na goma langu la kichuga naliseti ila inaonekana alikuwaga gangsta sana miaka ya nyuma ndio anaanza kupata tabia za kisichana! Ye poda kwake mwiko
 
Wakuu habari. Nimeoa na nina mwaka na nusu wa ndoa sasa. Nina tatizo ambalo ninahitaji ushauri kwa wazoefu. Binafsi napenda mwanamke anayependeza na kujijali , na napenda awe mke wangu ili nisilazimike kutoka huko nje
Wakati unachagua kumuoa hukujua kama hapendi mambo ya kusuka na kupendeza? au mwenzetu umeoa kizamani uliletewea na wazazi kutoka kijijini binti usiemjua ukaanza tu kuishi nae? Kama ulimjua toka mwanzo yuko hivyo na still ukaona anafaa acha unafki
 
Wakuu habari. Nimeoa na nina mwaka na nusu wa ndoa sasa. Nina tatizo ambalo ninahitaji ushauri kwa wazoefu. Binafsi napenda mwanamke anayependeza na kujijali , na napenda awe mke wangu ili nisilazimike kutoka huko nje kuchepuka. Sasa nina mke wangu hapendi kusuka, yaani kichwani yupo rough, mara chache (mara moja kwa miezi
Labda hapendi kusuka? Basi mpeleke saloon akate nywele style nzurii atapendeza tuu! Kama hataki basi mpeleke kwa Mwamposa amuombee ☺️
 
Back
Top Bottom