Msaada: Mmewezaje kupona maumivu ya kufiwa na mtu wa karibu?

Msaada: Mmewezaje kupona maumivu ya kufiwa na mtu wa karibu?

snowhite

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
18,065
Reaction score
24,559
Wanajamvi, ninaomba msaada wa dhati kabisa.

Mdogo wangu wa pekee alifariki mwaka jana. Tulizaliwa wawili tu, wazazi pia walishafariki. Baada ya wazazi kufariki, nilikuwa mama yake, alikuwa baba yangu.

Fact kuwa familia hii nimebaki peke yangu, kila nikiwaza inanistrike vibaya mno! Sijui kama nimekubali kuwa hayupo tena au la.

Naogopa kukubali kuwa nimebaki peke yangu. Ninajikuta kama mahala fulani sikumlinda. Alifariki ghafla, nikaambiwa ni presha. Toka tumezika, nimeshindwa kurudi makaburini.

Ninajihisi upweke mkuu, tulikuwa tukishirikiana kufanya mambo mengi pamoja. Hakika sijui namna sahihi ya kudeal na hii trauma.

Mwenye mbinu na aliyepita same situation anisaidie!

Nina sali, ninamwombea, sijioni kuwa sawa.
 
Wanajamvi,
Ninaomba msaada wa dhati kabisa!
Mdogo wangu wa pekee alifariki mwaka jana. Tulizaliwa wawili tu, wazazi pia walishafariki.
Baada ya wazazi kufariki, NILIKUWA MAMA YAKE, ALIKUWA BABA YANGU!
Fact kuwa familia hii nimebaki peke yangu, kila nikiwaza inanistrike vibaya mno!
Sijui kama nimekubali kuwa hayupo tena au la!
Naogopa kukubali kuwa nimebaki peke yangu!
Ninajikuta kama mahala fulani sikumlinda!
Alifariki ghafla, nikaambiwa ni presha.
Toka tumezika, nimeshindwa kurudi makaburini.

Ninajihisi upweke mkuu, tulikuwa tukishirikiana kufanya mambo mengi pamoja!
Hakika sijui namna sahihi ya kudeal na hii trauma!
Mwenye mbinu na aliyepita same situation anisaidie!
Nina sali, ninamwombea
Sijioni kuwa sawa!
Muda unaponya,najua utasema umelisikia sana hili na ni cliche ila ndio ukweli.Labda unaweza usipone kabisa wala kusahau ila muda unapozidi kwenda utazoea tu kuishi bila yeye japo saa hizi unaona kama haiwezekani.Pole sana mkuu
 
Nasikia maumivu yako my dear, kwanza...
1. Kama wewe ni mkristo muombee misa kwa kumshukuru Mungu kwa kipindi chote alichokupa nafasai ya kuwa nao hapa Duniani.
2. Naomba maneo haya ya Biblia yakutie moyo Ayoubu 14.1
3. Tafuta marafiki wanaoweza kukutia moyo, ambao kwa kipindi hiki cha mpito mtakuwa mnazungumza habari nyingine hasa za mambo mnayofanya pamoja.
4. Nakuombea ndugu yangu
 
Pole sana Mkuu. Jitahidi kutembelea kaburi lake mpaka utakapopazoea maumivu yatapungua. Ni kama unakimbia tatizo ambalo halikwepeki,katembelee kaburi la mdogo wako jitahidi upasafishe pia
 
Pole sana ndugu yangu, Jitahidi uikubali hali yaani (KUBALI MATOKEO) kuwa ukumbushe moyo wako kwamba sote Duniani tunapita na saikolojia yako ijue na uzoee!! Na usijute hata Kidogo na umshukuru Mungu kwa uwepo wako maana kuna Jamii inajifunza na kufarijika kupitia UWEPO wako!!
 
Kwanza pole sana nafahamu hali unayopitia kupitia maelezo yako.

Psychosis, PTSD, Axiety, Fear, Denial, Stigma kwa pamoja zinaweza kukuletea Depression ambayo ina matokeo mabaya sana ikiwemo, kujikataa, kudhuru au kujidhuru ikiwa ni pamoja na kuwaza kujitoa uhai..

Kitaalamu huwezi kusahau tatizo bali ulikumbuke tatizo na lisikuumize, njia zipo. Wapo waliofiwa kama wewe bado wana ishi kwa ujasiri na matumaini makubwa haijalishi waliponaje hiyo hali bali jitafute mwenyewe utapona.

Ulichokosa wewe ni njia sahihi ya kujitibu. Karibu PM nikusaidie mkuu. Najuwa hali unayopitia. Situmii kipaji tu ni professional yangu.
 
Wanajamvi,
Ninaomba msaada wa dhati kabisa!
Mdogo wangu wa pekee alifariki mwaka jana. Tulizaliwa wawili tu, wazazi pia walishafariki.
Baada ya wazazi kufariki, NILIKUWA MAMA YAKE, ALIKUWA BABA YANGU!
Fact kuwa familia hii nimebaki peke yangu, kila nikiwaza inanistrike vibaya mno!
Sijui kama nimekubali kuwa hayupo tena au la!
Naogopa kukubali kuwa nimebaki peke yangu!
Ninajikuta kama mahala fulani sikumlinda!
Alifariki ghafla, nikaambiwa ni presha.
Toka tumezika, nimeshindwa kurudi makaburini.

Ninajihisi upweke mkuu, tulikuwa tukishirikiana kufanya mambo mengi pamoja!
Hakika sijui namna sahihi ya kudeal na hii trauma!
Mwenye mbinu na aliyepita same situation anisaidie!
Nina sali, ninamwombea
Sijioni kuwa sawa!
Grief
 
mkuu maumivu yako ni makubwa
cha muhimu kubali hali na ipokee ilivyo ili kuepusha kukuletea msongo wa mawazo

ukiwa na ndugu mnaelewana na akafariki ama kufanya tukio la ajabu lazima ikuume sana tena kama ww unajihisi hatia ya kutomlinda basi inakutafuna si kdg
 
  • Thanks
Reactions: HLM
Pole sana,,ila ukweli ni kuwa time is the true healer,,lakini pia jitahidi kuepuka kukaa mazingira yanayopelekea wewe kuwa katika hali hiyo,,angalia ni ni kipi hasa kinakufurahisha ukifanyapo daily then base nacho ukitumia mda mwingi kukifanya,,mwisho ni muhimu kuwa na rafiki wa karibu/mpenzi,,atakaye play part ya kujithidi wewe unasahau yaliyopita, then unafocus na yaliyopo na yajayo pia.
 
Mungu akutie nguvu mkuu uweze kuachilia maumivu na kuwa sawa japo sio rahisi ila utakua sawa tu. Kwa upande wangu niliondokewaga na wazazi wote wawili mwaka mmoja walipishana mwezi tu, nikiwa darasa la pili, na hapo nilibaki peke angu mdogo angu alikufa alivozaliwa tu.
Muda mwingine nasemaga tu Mungu asante uliwachukua mapema nishazoea kuwa alone kwamba sina wazazi wala ndugu wa damu (japo natamani dogo angekua hai) , Sawa unakua na ndugu wengine but hamuwezi kuwa na bond kama ya ndugu yako wa damu.
Usijilaumu sana wewe sio sababu ya yeye kufa ni kazi ya Mungu tu.
 
Soma bible sana, jitahidi uwe pamoja na Bwana. Shalom (Mungu wa amani) atakupa amani na faraja yenye kuzidi. Achana na mambo ya Muda
 
Back
Top Bottom