Msaada,mtaji wa mil.3 kwa mwanza nifanye biashara ipi

Msaada,mtaji wa mil.3 kwa mwanza nifanye biashara ipi

frnk

Senior Member
Joined
Jun 19, 2012
Posts
160
Reaction score
12
Habari Wadau, naombeni msaada kwa hapa mwanza ninaweza tumia vipi huu mtaj mdogo niliokua nao,angalau nikabiliane na ugumu wa maisha, kwa kuzingatia bado ninasoma sheria hapa SAUT, naombeni mawazo yenu wadau angalau niweze kua mjasiliamali mdogo....

Natanguliza shukrani za dhati katika kupokea mawazo yenu wana JF wenzangu.
 
baba ungekua na m2 ninge kwambia anza bihashara ya asali ingekulipa fasta!
 
Kwa vile uko shule huhitaji biashara za kusafiri au kukaa dukani! Kwa mtaji wako huo hebu nusa nusa kando kando ya ziwa, upate ka kiwanja ukodi 15m x 8m! Hela yako inatosha kabisa kusimamisha green house! Kwa pesa hiyo hiyo green house itakuwa na mfumo wa umwagiliaji wa matone! Utatumia nguvu kidogo tu kutayarisha matuta. Ukipanda nyanya aina ya Anna F1 unavuna miezi 6 hadi 8! Ukivutiwa na idea hii uliza chochote nitakupa full dose ya mbinu muhimu! Green house itakufanya uzalishe kipindi cha mvua ambako bei iko juu! Hicho kiplot kina zaa mara 10 ya eneo hilo kwa nje! Miradi iko mingi jamani tufanye ile ambayo haina ushindani!
 
Kwa vile uko shule huhitaji biashara za kusafiri au kukaa dukani! Kwa mtaji wako huo hebu nusa nusa kando kando ya ziwa, upate ka kiwanja ukodi 15m x 8m! Hela yako inatosha kabisa kusimamisha green house! Kwa pesa hiyo hiyo green house itakuwa na mfumo wa umwagiliaji wa matone! Utatumia nguvu kidogo tu kutayarisha matuta. Ukipanda nyanya aina ya Anna F1 unavuna miezi 6 hadi 8! Ukivutiwa na idea hii uliza chochote nitakupa full dose ya mbinu muhimu! Green house itakufanya uzalishe kipindi cha mvua ambako bei iko juu! Hicho kiplot kina zaa mara 10 ya eneo hilo kwa nje! Miradi iko mingi
jamani tufanye ile ambayo haina ushindani!

Kama kumbukumbu zangu ni sahihi, ndiyo leo nasoma uzi on Green house farming. Ninahamu sana na suala hili, ila sijui gharama na mbinu muafaka. Kwa maelezo na mwito wako, naomba maelezo zaidi on this issue. Mimi nina shamba la ekari mbili pale Kisarawe ningependa kujiingiza kwenye green house farming hasa kwa mahindi au nyanya kama ulivyo mshauri ndugu FRNK. Na mimi naomba ushauri wako. ASANTE
 
Kwa vile uko shule huhitaji biashara za kusafiri au kukaa dukani! Kwa mtaji wako huo hebu nusa nusa kando kando ya ziwa, upate ka kiwanja ukodi 15m x 8m! Hela yako inatosha kabisa kusimamisha green house! Kwa pesa hiyo hiyo green house itakuwa na mfumo wa umwagiliaji wa matone! Utatumia nguvu kidogo tu kutayarisha matuta. Ukipanda nyanya aina ya Anna F1 unavuna miezi 6 hadi 8! Ukivutiwa na idea hii uliza chochote nitakupa full dose ya mbinu muhimu! Green house itakufanya uzalishe kipindi cha mvua ambako bei iko juu! Hicho kiplot kina zaa mara 10 ya eneo hilo kwa nje! Miradi iko mingi jamani tufanye ile ambayo haina ushindani!

Mkuu shukrani... kwa ekari moja , kufunga mfumo wa Green House inaweza kwenda hadi bei gani?!
 
Kama kumbukumbu zangu ni sahihi, ndiyo leo nasoma uzi on Green house farming. Ninahamu sana na suala hili, ila sijui gharama na mbinu muafaka. Kwa maelezo na mwito wako, naomba maelezo zaidi on this issue. Mimi nina shamba la ekari mbili pale Kisarawe ningependa kujiingiza kwenye green house farming hasa kwa mahindi au nyanya kama ulivyo mshauri ndugu FRNK. Na mimi naomba ushauri wako. ASANTE

Mkuu Mzee Mukaruka: Kilimo cha green house ni kilimo ambacho ni cha hatua kubwa zaidi. Ni kilimo cha kulimia ndani ya mabanda ya nailoni. Mabanda haya yanapitisha mwanga vizuri tu na yanakinga mimea dhidi ya mvua inayosababisha magonjwa mara nyingi kwenye mimea, inakinga mimea dhidi ya joto kali au baridi kali kutegemea na lilivyotengenezwa. Banda hilo hukinga mimea dhidi ya magonjwa mengi na wadudu wengi washambuliao mimea. Mara nyingi kilimo hiki cha green house huendana na matumizi ya umwagiliaji kwa njia ya matone kwa hiyo mahitaji ya maji ni kidogo. Kilimo cha kwenye green house kinatoa mavuno makubwa sana ukilinganisha na kilimo cha nje, kwa mfano nyanya hufikia kuzaa mara 10 ya uzazi ukilinganisha na nyanya iliyopandwa nje kwa eneo sawa. Kwa kuwa mazao yanalimwa kwenye mazingira yaliyodhibitiwa (controlled environment) mazao huweza kustawi vema mwaka mzima, tofauti na kilimo cha nje ambapo hali ya hewa majira fulani huathiri uzaaji na ustawi wa mazao.

Pamoja na kwamba kilimo cha Green house kinatoa uhakika mkubwa sana wa kupunguza risk katika uzalishaji wa mazao ni Technolojia ghari. Gharama inategemea iwapo green house imetengenezwa kwa vyuma au mbao (na miti). Green house ya vyuma inadumu zaidi ya miaka 10, bei zake hutegemea ukubwa wake, green house ya eneo 15 m x 8 m inaweza kugharimu kuanzia mil 3 na kuendelea. Green house ya mbao inaweza kuwa nusu ya bei ya green house ya chuma. Ikitengenezwa vizuri inadumu zaidi ya miaka miwili hasa kama mbao zitadhibitiwa zisioze na kuliwa na mchwa.

Nimeambatanisha link kama utafanikiwa kuzifungua zitakusaidia upate picha halisi.

kilimokisasa - Construction of A Greenhouse
kilimokisasa - Construction of A Greenhouse



Hapa Tanzania kampuni ya BALTON Tanzania Ltd ndiyo imejikita kuuza vifaa vya kutengenezea green house. Wao hawajihusishi kutengeneza green house za mbao bali wanauza set nzima ya greenhouse za chuma na nadhani wanatoa msaada wa utaalamu wa kuijenga. Nimekuwekea anwani yao hapa uweze kuwasiliana ili ujue bei zao kwa sasa.

BALTON DAR ES SALAAM
Mikocheni Light Industiral Area, 23 Coca Cola Road
PO Box 712
Dar Es Salaam, Tanzania
Tel: 00 255 22 277 2826 / 00 255 22 277 2831
Fax: 00 255 22 277 5989
Mob: 00 255 754 332 214 / 00 255 754 320 925barua pepe: balton@baltontz.com


Mwisho namalizia kwa kukueleza kuwa kutokana na ughari wa green house, mazao yanayoshauriwa kulimwa ni yale yenye bei kubwa na uwezo wa kuzaa kwa kipindi kirefu ili uweze kurudisha pesa na kupata faida. Mazao hayo ni kama Nyanya (aina maalum kwa greenhouse - mfano Anna F1), pilipili hoho na matango. Green house zinatumika zaidi mkoani Arusha kwenye kilimo cha Maua. Ni mazao ya bei mbaya tu ndiyo hulimwa humo siyo mahindi wala alizeti.
 

Attachments

Kubota asante nimeiona na nimeielewa vizuri sana. Nitazidi kuifanyia kazi kwa kutafuta kwenye mitandao wauzaji wa used or refurbished green houses hasa kutoka China au India. Balton ni aghari sana. Tutazidi kupeana feedback Kubota.By the way thread yako ya kuku wa kienyeji ni chemsha bongo sana. Sijui hiyo elimu na hayo maujuzi kama inafaa kwa ufugaji wa kuku chotara? Hebu tujuze kama inawezekana.
 
Kubota asante nimeiona na nimeielewa vizuri sana. Nitazidi kuifanyia kazi kwa kutafuta kwenye mitandao wauzaji wa used or refurbished green houses hasa kutoka China au India. Balton ni aghari sana. Tutazidi kupeana feedback Kubota.By the way thread yako ya kuku wa kienyeji ni chemsha bongo sana. Sijui hiyo elimu na hayo maujuzi kama inafaa kwa ufugaji wa kuku chotara? Hebu tujuze kama inawezekana.
 
Mkuu Kubota nimezipenda sana makala zako kuhusu ujasiriamali. Mi nataka kuwekeza kwenye kilimo eidha kwa kufuga mbuzi/kuku na au kulima mbogamboga na matunda. Ili kufanikiwa katika hayo, maji ni sehemu muhimu sana. Nilifanya survey ya kuchimba kisima cha maji kwenye kishamba changu ili niyatumie kwa umwagiliaji nikaambiwa yapo chini umbali wa mita 150 na bei ikawa iko juu mno kama 14M hivi. Nimepania sana kufanya shughuli hizo za kilimo ili niachane na mambo ya kuajiriwa lakini tatizo ni hayo maji. Kama naweza kupata mchimbaji ambaye atanifanyia kazi hiyo kwa bei ya chini nitafurahi, uwezo wangu haufiki hata nusu ya hiyo bei niliyoisema hapo juu. Naombeni ushauri na mawazo pia wana JF.
 
Kubota asante nimeiona na nimeielewa vizuri sana. Nitazidi kuifanyia kazi kwa kutafuta kwenye mitandao wauzaji wa used or refurbished green houses hasa kutoka China au India. Balton ni aghari sana. Tutazidi kupeana feedback Kubota.By the way thread yako ya kuku wa kienyeji ni chemsha bongo sana. Sijui hiyo elimu na hayo maujuzi kama inafaa kwa ufugaji wa kuku chotara? Hebu tujuze kama inawezekana.

Kuhusu kuku wa kienyeji jibu lako naomba ufungue thread yangu ya kuku wa kienyeji ndiyo ninaenda kukujibia huko ili niue ndege wengi kwa jiwe moja. Sorry kukusumbua.
 
Hiyo Green House mimi siwezi kutengeneza binafsi tu kimagumashi?

nahitaji materials gani na gani?
 
Naomba pia kufahamu hiyo green house inakuwa na mlango?

Je hewa inatoka wapi kama utafunga hiko kibanda kote kote
 
Mkuu Mzee Mukaruka: Kilimo cha green house ni kilimo ambacho ni cha hatua kubwa zaidi. Ni kilimo cha kulimia ndani ya mabanda ya nailoni. Mabanda haya yanapitisha mwanga vizuri tu na yanakinga mimea dhidi ya mvua inayosababisha magonjwa mara nyingi kwenye mimea, inakinga mimea dhidi ya joto kali au baridi kali kutegemea na lilivyotengenezwa. Banda hilo hukinga mimea dhidi ya magonjwa mengi na wadudu wengi washambuliao mimea. Mara nyingi kilimo hiki cha green house huendana na matumizi ya umwagiliaji kwa njia ya matone kwa hiyo mahitaji ya maji ni kidogo. Kilimo cha kwenye green house kinatoa mavuno makubwa sana ukilinganisha na kilimo cha nje, kwa mfano nyanya hufikia kuzaa mara 10 ya uzazi ukilinganisha na nyanya iliyopandwa nje kwa eneo sawa. Kwa kuwa mazao yanalimwa kwenye mazingira yaliyodhibitiwa (controlled environment) mazao huweza kustawi vema mwaka mzima, tofauti na kilimo cha nje ambapo hali ya hewa majira fulani huathiri uzaaji na ustawi wa mazao.

Pamoja na kwamba kilimo cha Green house kinatoa uhakika mkubwa sana wa kupunguza risk katika uzalishaji wa mazao ni Technolojia ghari. Gharama inategemea iwapo green house imetengenezwa kwa vyuma au mbao (na miti). Green house ya vyuma inadumu zaidi ya miaka 10, bei zake hutegemea ukubwa wake, green house ya eneo 15 m x 8 m inaweza kugharimu kuanzia mil 3 na kuendelea. Green house ya mbao inaweza kuwa nusu ya bei ya green house ya chuma. Ikitengenezwa vizuri inadumu zaidi ya miaka miwili hasa kama mbao zitadhibitiwa zisioze na kuliwa na mchwa.

Nimeambatanisha link kama utafanikiwa kuzifungua zitakusaidia upate picha halisi.

kilimokisasa - Construction of A Greenhouse
kilimokisasa - Construction of A Greenhouse



Hapa Tanzania kampuni ya BALTON Tanzania Ltd ndiyo imejikita kuuza vifaa vya kutengenezea green house. Wao hawajihusishi kutengeneza green house za mbao bali wanauza set nzima ya greenhouse za chuma na nadhani wanatoa msaada wa utaalamu wa kuijenga. Nimekuwekea anwani yao hapa uweze kuwasiliana ili ujue bei zao kwa sasa.

BALTON DAR ES SALAAM
Mikocheni Light Industiral Area, 23 Coca Cola Road
PO Box 712
Dar Es Salaam, Tanzania
Tel: 00 255 22 277 2826 / 00 255 22 277 2831
Fax: 00 255 22 277 5989
Mob: 00 255 754 332 214 / 00 255 754 320 925barua pepe: balton@baltontz.com


Mwisho namalizia kwa kukueleza kuwa kutokana na ughari wa green house, mazao yanayoshauriwa kulimwa ni yale yenye bei kubwa na uwezo wa kuzaa kwa kipindi kirefu ili uweze kurudisha pesa na kupata faida. Mazao hayo ni kama Nyanya (aina maalum kwa greenhouse - mfano Anna F1), pilipili hoho na matango. Green house zinatumika zaidi mkoani Arusha kwenye kilimo cha Maua. Ni mazao ya bei mbaya tu ndiyo hulimwa humo siyo mahindi wala alizeti.
Nimeipenda hii
 
Karibu Forever Living, kampuni itakupa kile unachohitaji kukabili maisha kwa mtaji wako unaweza kuwa bilionea in a short run kama uko serious.
 
Hiyo Green House mimi siwezi kutengeneza binafsi tu kimagumashi?

nahitaji materials gani na gani?

Mkuu maundumula, kujenga green house kimagumashi inawezekana sana, kama unaweza kuview you tube sema nikuelekeze utazame inavyotengenezwa kimagumashi! Unaweza kupunguza gharama hadi nusu ya bei ya green house ready made. Green house ready made ni basically za vyuma hizi za kimagumashi ni za miti na mbao, nailoni na mfumo wa umwagiliaji ni ule ule haijalishi ni aina gani. Ukionaje unaweza uchana na mfumo wao wa umwagiliaji ukatumia watering can.
 
Naomba pia kufahamu hiyo green house inakuwa na mlango?

Je hewa inatoka wapi kama utafunga hiko kibanda kote kote

Mkuu Maundumula, ujenzi wa green house unazingatia sana mzunguko wa hewa kuingia na kutoka. Green house huwa zinajengwa kwa kutumia nylon na wavu (insect proof), wavu ndiyo hupitisha hewa. Kama unaweza kufungua attachment kama tano, kwenye post No 8 hapo nyuma utaona picha zitakazo jibu maswali mengi. Tuko pamoja!
 
Anaye taka kufanya hii kitu ni Bora akaenda Arusha au Moshi, ila sana sana Arusha make zimejaa ila zinaendeshwa na wazungu, na mara nyingi zinatumika kwa ajili ya Kilimo cha maua ya kusafirisha kwenda Ulaya,

Ila Green House inahitaji mtaji mkubwa sana, kwa sababu ni lazima uwe na maji ya kutosha kumwagilia na kuhusu hewa same time huwa zinafunuliwa kabisa inabakia Paa tu,

Mara nyingi Green house inategemeana na unacho taka kulima, Mfano wanao lima Maua wakati wa Kiangza huwa wanafunia kwa chini inabakia kwa juu, kwa sababu yale maua kitu yasicho patana nacho ni Maji ya Mvua, make huwa yana Acid ambayo huahaliba maua,

Ni bora aliye siriasi akafunga safari kwenda Arusha kuona kwa macho na hata kuwauliza wahusika maswali,

Na katika hiki kilimo ni Bora ukawa na soko lako la Uhakika na si kulima halafu upelekee Madalali Kariakoo, hapo itakula kwako na hutaweza, mara nyingi wanao fanya hiki kilimo huwa some time ni for export purpose ila kwa ghalama za kuendesha hii kitu ni lazima uwe na soko la uhakika usiingie tu kichwa kichwa kisa umeona mwenzako analima, make ndo tatizo letu hilo,

Ni lazima ujiridhishe na soko na si ujiridhishe kwa kusimuliwa vijiweni, bari kwa ku prove wewe mwenyewe kwamba real kuna soko na hata wahusika umeongea nao na mmekubaliana,

Itakuwa ni uwenda wazimu kufanya Green House and then unapelkea mazao pale kariakoo kusubili madalali waanze kudalalia mzigo wako
 
Back
Top Bottom