Msaada mwenye connection ya ajira nchi za Kiarabu

Changamoto uliyonayo ni hao tegemezi! Lakini ingekuwa ni Wewe, mke na mtoto, angalau hiyo 250 k ingesaidia hata kama ni ndogo!
Shida nyingine kwa mtoto wa kwanza mara nyingi huwa anaponzwa na huruma iliyopitiliza sana kwa ndugu na jamaa zake!
Ndiyo maana asilimia kubwa ya watoto wa kwanza kuzaliwa hawafanikiwi kimaisha!
Sasa jifanye kichaa uachane na tegemezi hao, uone kama hutatoka!
 
kazi gani unataka uarabuni?njoo inbox nikupe mchongo wa kazi Dubai International Airport ni semi skilled job(Airport cleaner,na Airport porter
Mkuu kama mpaka leo hii unaweza kunipatia mimi ama upo katika nafasi unaweza kunipa huu mchongo naombaa
 
Umefanikiwa kusepa mkuu
 
Naomba unisaidie process zake mkuu
Unaanza Kwa kujaza fomu kwenye mtandao wao wa uhamiaji. Kwenye hiyo fomu utaapload.​
✓passport size yako hivi karibuni.
✓Barua ya utambulisho wa kazini kama inafanya kazi {hii ni muhimu inapunguza maswali}
✓kama barua hapo juu huna utaweka barua ya utambulisho kutoka Kwa mtendaji wa mtaa unaoishi.
✓utaweka kitambulisho chako Cha nida haswa namba Kuna sehemu ya kuiandika mwanzoni kabisa.​
✓cheti chako Cha kuzaliwa
✓cheti Cha kuzaliwa Cha mmoja wa wazazi wako.
✓kitambulisho Cha nida Cha mmoja wa wazazi wako.

Ukisha malizia kuijaza hiyo fomu itakuletea menu yenye control ya kulipia utailipia shilingi elfu 20.

Kama utakuwa na speed kubwa utaidownload hiyo fomu Kisha utaiambatanisha tena na hizo hardcopy ulizo ziupload. Hutokuwa na uwezo wa kudownload hiyo fomu kama hujailipia.

Utatembelea ofisi ya UHAMIAJI iliyo karibu naweza ukiwa na 130,000/= documents zako zikikaguliwa ukaulizwa vi maswali vya hapa na pale, usipo onyesha uoga wakazikubali watakupa control tena ulipe hiyo 130,000/= Kisha utapangiwa siku ya kwenda kuichukua passport Yako ya kusafiria.

N.b

Kuna mbinu nyingine nimeshindwa kuziandika ila ukipenda unaweza kunitumia namba Yako pm. Nika kuelewesha Kwa urefu Zaidi...!​
 
Ok nashukuru Sana mkuu, nitakutumia namb PM
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…