Msaada namna faida inavotengenezwa kupitia uwakala

Msaada namna faida inavotengenezwa kupitia uwakala

Kama una mtaji mdogo na unategemea uwakala pekee hutoboi na unaweza kufilisika. Maana siku hizi wamepunguza kamishen. Ni afadhali ufungue duka na ndani ya duka ndo uweke na uwakala angalau utapata faida na utasurvival. Ila kama una mtaji mkubwa na ukipata eneo lenye mzunguko mzuri inakulipa. Kuna biashara nyingi zenye faida kuliko hiyo ila vijna hawataki kuzifanya wanataka biashara simple awe anapepewa na feni ila faida ndo ivo ni ndogo.
 
Kwema wakuu!? Naomba msaada wa namna faida inavotengenezwa kupitia uwakala wa mitandao ya simu.
Faida inapatikana kwa kufanya miamala mingi zaidi kwa siku at least ukiweza kufanya transactions 100 hadi 200 kila mtandao kwa siku utatengeneza kamisheni yako iwe nzuri zaidi. Huwa wanalipa kwa mirejea

1,000-3,000 mrejea sh36

4,000 mrejea sh40

5,000-6,000 mrejea sh 96

7,000-9,000 mrejea sh 100

10,000-40,000 mrejea sh 290

50,000-90,000 mrejea sh 320

100,000-199,999 mrejea sh 550

200,000- 299,999 mrejea sh 1,100

Hiyo ni kwa wateja wanaotoa na kuweka inatofautiana kidogo sana kwahiyo ukifanya transactions kama 200 kwa kila mtandao utaona faida kidogo

Kila la kheri
 
Kama una mtaji mdogo na unategemea uwakala pekee hutoboi na unaweza kufilisika. Maana siku hizi wamepunguza kamishen. Ni afadhali ufungue duka na ndani ya duka ndo uweke na uwakala angalau utapata faida na utasurvival. Ila kama una mtaji mkubwa na ukipata eneo lenye mzunguko mzuri inakulipa. Kuna biashara nyingi zenye faida kuliko hiyo ila vijna hawataki kuzifanya wanataka biashara simple awe anapepewa na feni ila faida ndo ivo ni ndogo.
Kama biashara ipi mkuu?
 
Kama biashara ipi mkuu?
ni vigumu kumshauli mtu kama hujui mtaji wake unaanzia sh ngapi na anaishi wapi

Labda nijaribu kidogo kama uko mikoani umeshawahi kuwaza kufungua duka la viungo? Mfano hiliki tangawizi vitunguu swaumu pilipili manga mdalasini karafuu kahawa n.k? Unauza kwa jumla na rejareja. Ni biashara nzuri ina faida sana na sio risk kama uwakala maana kwenye uwakala ukipata shot ndo umeyumba maana pesa unakuwa nayo mkononi tofauti na hiyo biashara niliyokuambia hata ukipata hasara kwenye kitu kimoja kingine kitakupa faida. Pia unaweza kuongeza na vitu vingine kadri upendavyo. Jaribu ukifanikiwa mshukuru Mwenyezi Mungu. Hiyo ni biashara moja nimekutajia ila ziko nyingi. Pia katika hizo nilizotaja unaweza kuamua kubase kwenye biashara mojawapo peke yake na ukafanikiwa inategemea biashara yako unaifanyaje. Mfano kuna matajiri kazi yao ni kuuza tangawizi tu na wametajirika kupitia kazi hiyo.
 
Biashara zipo nyingi sana tena za mtaji mdogo na zenye faida na mtaji unakua na kufikia mafanikio. Tatizo vijana wengi wanataka kujifungia dar. Nawashauri vijana wenzangu wajaribu kwenda mikoani wajionee fursa tele za kuwapatia mafanikio. Na wale ambao wako mikoani angalieni mikoa yenye fursa ambayo watu wake bado wamelala wekeza hapo mpaka waje waamke we umeshatajirika. Mfano mikoa yenye wasukuma wengi, hawa jamaa hawajui mambo ya biashara wao wanachojua ni kulima na kufuga na wakivuna pesa wanaenda kutumia na wanawake. Kwa hiyo biashara yoyote utakayofungua usukumani itakulipa hasa msimu wa mavuno yaani mwezi wa nne mpaka wa 9. Mwezi wa 9 mpaka masika uza pembejeo na vifaa vya kilimo. Mambo ni mengi siwezi kueleza yote.
 
ni vigumu kumshauli mtu kama hujui mtaji wake unaanzia sh ngapi na anaishi wapi

Labda nijaribu kidogo kama uko mikoani umeshawahi kuwaza kufungua duka la viungo? Mfano hiliki tangawizi vitunguu swaumu pilipili manga mdalasini karafuu kahawa n.k? Unauza kwa jumla na rejareja. Ni biashara nzuri ina faida sana na sio risk kama uwakala maana kwenye uwakala ukipata shot ndo umeyumba maana pesa unakuwa nayo mkononi tofauti na hiyo biashara niliyokuambia hata ukipata hasara kwenye kitu kimoja kingine kitakupa faida. Pia unaweza kuongeza na vitu vingine kadri upendavyo. Jaribu ukifanikiwa mshukuru Mwenyezi Mungu. Hiyo ni biashara moja nimekutajia ila ziko nyingi. Pia katika hizo nilizotaja unaweza kuamua kubase kwenye biashara mojawapo peke yake na ukafanikiwa inategemea biashara yako unaifanyaje. Mfano kuna matajiri kazi yao ni kuuza tangawizi tu na wametajirika kupitia kazi hiyo.
Maelezo mazuri, huwa natamani sana biashara za mazao, biashara yenye faida ni aidha uzalishaji (production) au muingizaji (importer) , ila changamoto kubwa ya biashara za mazao ni udalali na huwezi uza bila ya udalali nikifikiria hapo huwa nachoka
 
Biashara zipo nyingi sana tena za mtaji mdogo na zenye faida na mtaji unakua na kufikia mafanikio. Tatizo vijana wengi wanataka kujifungia dar. Nawashauri vijana wenzangu wajaribu kwenda mikoani wajionee fursa tele za kuwapatia mafanikio. Na wale ambao wako mikoani angalieni mikoa yenye fursa ambayo watu wake bado wamelala wekeza hapo mpaka waje waamke we umeshatajirika. Mfano mikoa yenye wasukuma wengi, hawa jamaa hawajui mambo ya biashara wao wanachojua ni kulima na kufuga na wakivuna pesa wanaenda kutumia na wanawake. Kwa hiyo biashara yoyote utakayofungua usukumani itakulipa hasa msimu wa mavuno yaani mwezi wa nne mpaka wa 9. Mwezi wa 9 mpaka masika uza pembejeo na vifaa vya kilimo. Mambo ni mengi siwezi kueleza yote.
Tupe nondo mkuu
 
Mzunguko wa miamala na mtaji utakavyo wekeza
Kuna jamaa yangu kawekeza 20m kwenye miamala (bank na mitandao ya sim)

Anasema faida anapata 1m Kila mwezi hapo katoa Kodi,ulinzi,cashier
Kaweka mtaji mkubwa faida ndogo, mwambie atafute location nzuri kwa mtaji huo 4m hakosi
 
Mzunguko wa miamala na mtaji utakavyo wekeza
Kuna jamaa yangu kawekeza 20m kwenye miamala (bank na mitandao ya sim)

Anasema faida anapata 1m Kila mwezi hapo katoa Kodi,ulinzi,cashier
Inategemea na mzunguko wa pesa wa eneo husika
 
Kama una mtaji mdogo na unategemea uwakala pekee hutoboi na unaweza kufilisika. Maana siku hizi wamepunguza kamishen. Ni afadhali ufungue duka na ndani ya duka ndo uweke na uwakala angalau utapata faida na utasurvival. Ila kama una mtaji mkubwa na ukipata eneo lenye mzunguko mzuri inakulipa. Kuna biashara nyingi zenye faida kuliko hiyo ila vijna hawataki kuzifanya wanataka biashara simple awe anapepewa na feni ila faida ndo ivo ni ndogo.
Kama zipi mkuu funguka apa kile unafahamu huenda kikabadilsha jambo tunashare kiongoz
 
Mzunguko wa miamala na mtaji utakavyo wekeza
Kuna jamaa yangu kawekeza 20m kwenye miamala (bank na mitandao ya sim)

Anasema faida anapata 1m Kila mwezi hapo katoa Kodi,ulinzi,cashier
Badp ngoma ngumu.....20M ni hela nyingi ilitakiwa angalau apatw faida ya 2M minimum
 
Mzunguko wa miamala na mtaji utakavyo wekeza
Kuna jamaa yangu kawekeza 20m kwenye miamala (bank na mitandao ya sim)

Anasema faida anapata 1m Kila mwezi hapo katoa Kodi,ulinzi,cashier
Huu ujumbe umenikatisha tamaa.

Mwenyewe anaona anapata saana
 
Kama una mtaji mdogo na unategemea uwakala pekee hutoboi na unaweza kufilisika. Maana siku hizi wamepunguza kamishen. Ni afadhali ufungue duka na ndani ya duka ndo uweke na uwakala angalau utapata faida na utasurvival. Ila kama una mtaji mkubwa na ukipata eneo lenye mzunguko mzuri inakulipa. Kuna biashara nyingi zenye faida kuliko hiyo ila vijna hawataki kuzifanya wanataka biashara simple awe anapepewa na feni ila faida ndo ivo ni ndogo.
Kweli kwa maelezo ya wadau hapa faida ni ndogo sana.
Ukiona wamechili ndani na kiyoyozi cha feni unatamani
 
Faida inapatikana kwa kufanya miamala mingi zaidi kwa siku at least ukiweza kufanya transactions 100 hadi 200 kila mtandao kwa siku utatengeneza kamisheni yako iwe nzuri zaidi. Huwa wanalipa kwa mirejea

1,000-3,000 mrejea sh36

4,000 mrejea sh40

5,000-6,000 mrejea sh 96

7,000-9,000 mrejea sh 100

10,000-40,000 mrejea sh 290

50,000-90,000 mrejea sh 320

100,000-199,999 mrejea sh 550

200,000- 299,999 mrejea sh 1,100

Hiyo ni kwa wateja wanaotoa na kuweka inatofautiana kidogo sana kwahiyo ukifanya transactions kama 200 kwa kila mtandao utaona faida kidogo

Kila la kheri
Asante kwa taarifa ya kina
 
Maelezo mazuri, huwa natamani sana biashara za mazao, biashara yenye faida ni aidha uzalishaji (production) au muingizaji (importer) , ila changamoto kubwa ya biashara za mazao ni udalali na huwezi uza bila ya udalali nikifikiria hapo huwa nachoka
Niliwahi fikiria hii kuuza mahindi nikafanya utafiti Masoko ya Dar aisee Mtaji wa Milioni 30 unapata faida ya 1M kwa ku hustle sana
 
Back
Top Bottom