Msaada: Napigwa shoti nikigusana na mtu au kukanyaga chini bila kuvaa kitu miguuni

Msaada: Napigwa shoti nikigusana na mtu au kukanyaga chini bila kuvaa kitu miguuni

Nimechanganyikiwa usiku nikimgusa mke wangu napigwa shoti, nikikanyaga chini peku peku napigwa shoti mbaya zaidi. Leo asubuhi nimesalimiana na mtu ameshangaa nimepiga shoti yaani hadi ameshtuka kabisa.

Hii ni nini jamani mwenye kujua zaidi anielekeze, maana nahisi kuchanganyikiwa
Ata ukienda chooni kunya unapigwa shoti pia mkuu?
 
Nakuelewa, ilishanitokeaga hiyo hali na watu walikuwa hawanielewi, ila nashukuru iliisha yenyewe...
.
.
Isije ikawa miwaya [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Mie huwa inanitokea mara kwa mara. Hapa juzi juzi nikiwa kanda ya kati nilienda dukani kununua kitu, muuza duka alikuwa wa kike basi ile nampa hela tukapigwa shoti balaaa. Mtoto wa kike aliogopa sana. Namie nikapata upenyo wa kuzengea hapo hapo nikamwambia damu zetu zimeendana ndio maana tumepata shoti. Akaniamini mnoo. Hadi leo ni marafiki.
 
Nimechanganyikiwa usiku nikimgusa mke wangu napigwa shoti, nikikanyaga chini peku peku napigwa shoti mbaya zaidi. Leo asubuhi nimesalimiana na mtu ameshangaa nimepiga shoti yaani hadi ameshtuka kabisa.

Hii ni nini jamani mwenye kujua zaidi anielekeze, maana nahisi kuchanganyikiwa
Hiyo inasababishwa na matumizi ya vitu vinavyocharge mwili hasa maeneo yenye baridi kavu. Baadhi ya vitu kama viatu vya raba, matandiko kama shuka na blanket na tiles za nyumba, aluminium, na vitu vingine vyenye uwezo mkubwa wa kuhifadhi charge. Jaribu kuangalia kama hutumia hivyo vitu nilivyotaja wala hauko eneo lenye baridi basi nenda hospitali.
 
Nimechanganyikiwa usiku nikimgusa mke wangu napigwa shoti, nikikanyaga chini peku peku napigwa shoti mbaya zaidi. Leo asubuhi nimesalimiana na mtu ameshangaa nimepiga shoti yaani hadi ameshtuka kabisa.

Hii ni nini jamani mwenye kujua zaidi anielekeze, maana nahisi kuchanganyikiwa
Uongo mwingine bwana.... sa uo muda adi ukakutana na mtu kusalimiana izo shot si zingeshakuua... au ulikua hugusi tena chini??

Bas we ni "tommorow people"
 
Usipotubu mpaka kufikia kesho tumboni mwako itasikika milio ya shambulio la smg unamaliza magzine, unapumzika kidogo ngoma inajirudiarudia.

Usiseme hatukukwambia cha kufanya.
 
Jaribu kuangalia kitu unachokuwa umekishika kama kina shoti, kama simu au machine nyingine.
 
Nimechanganyikiwa usiku nikimgusa mke wangu napigwa shoti, nikikanyaga chini peku peku napigwa shoti mbaya zaidi. Leo asubuhi nimesalimiana na mtu ameshangaa nimepiga shoti yaani hadi ameshtuka kabisa.

Hii ni nini jamani mwenye kujua zaidi anielekeze, maana nahisi kuchanganyikiwa
My be mfumo wa microchip umenza kaz yake maana hata hii technology ya smart phone hazitaki kuoparate kwa kijiti Ila finger touch ama mlango kufunguka wenyewe ukiukaribia mmm pengine maandiko yameti100
 
Uongo mwingine bwana.... sa uo muda adi ukakutana na mtu kusalimiana izo shot si zingeshakuua... au ulikua hugusi tena chini??

Bas we ni "tommorow people"
Unajua tabia ya charge? Nikupe zoezi kidogo, chana karatasi vipande vidogo vidogo. Pia chukua kalamu ya biki sugua kwenye nywele kichani. Halafu gusisha hiyo biki kwenye hivyo vikaratasi angalia kitakachotokea.

Hivyo hivyo kama mtu kavaa raba zenye kikanyagio cha sufi kwa muda mrefu anapotembea ule msuguano wa mguu na kiatu huucharge mwili. Charge zinaweza kufikia kiwango ambacho mwili hauwezi himili ndipo hutafuta sehemu ya kutokea. Ikitokea mhusika akagusa vitu vingine charge hufatufa upenyo zitoke. Ikitokea hicho kilichoguswa pia kina charge ndipo shot hutokea. Mara nyingi hali hiyo hutokea maeneo yenye baridi au low humidity. Wala haihusiani na shida ya kiafya.
 
Mie huwa inanitokea mara kwa mara. Hapa juzi juzi nikiwa kanda ya kati nilienda dukani kununua kitu, muuza duka alikuwa wa kike basi ile nampa hela tukapigwa shoti balaaa. Mtoto wa kike aliogopa sana. Namie nikapata upenyo wa kuzengea hapo hapo nikamwambia damu zetu zimeendana ndio maana tumepata shoti. Akaniamini mnoo. Hadi leo ni marafiki.
Umesha pigs na show mkuu?
 
Ukiwa maeneo yote au nyumbani kwako tu????
Kama ni nyumbni basi hakikisha nyumba yako imefanyiwa erthing vizure. Protective earth PE iwe sawa isiwe inavujisha umeme

Kama huelewi nicheki kama unahisi chanzo ni hiki
 
Tatizo hilo lipo ndugu, kuna rafiki yangu ana duka, akigusa meza za aluminium anasikia shot kama hiyo. Sijafahamu sababu ni nini lkn naamini watakuja wataalamu kufafanua
Hata mimi kuna kipindi huwa inanitokea sijui ni nini hasa
 
Back
Top Bottom