Msaada: Nataka kuishitaki nyumba ya ibada iliyo jirani na nyumba yangu

Msaada: Nataka kuishitaki nyumba ya ibada iliyo jirani na nyumba yangu

Ndio kaka tunavumiliana sana kwenye haya mambo... Ila kwa wale yanayowahusu hawanaoni tatizo sio wote ila wengine hata kama hawaswali wanafikir wakikosoa watakuwa wanapata dhambi, si unajua watu tunavyoogopa vitisho vya kiimani.
Swala ni bora kuliko usingizi... Alafu sasa mara nyingi wanaosema hivyo saa hizo ni mababu, tayar walishauchapa usingizi ujanani sasa wamekuwa wazee usingizi ni wa manati, wanawaambia wengine usingizi si muhimu kuliko sala, aliyesema hivyo ni nani???
Hivi anajua kama usingizi ni afya kwa ubongo???

Sent using Jamii Forums mobile app
We jamaa ni comedian

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani nani kazungumzia adhana?,kinacholalamikiwa hapa ni kuamsha watu saa kumi kasoro na maneno ya kitanda ndo jeneza lako ilhali sala inasaliwa saa 11 asubuhi,anaongea dakika kumi nzima tena kwa loud speaker,sasa kama mimi ni mpumbavu basi na wale mashehe waliompiga jamaa stopu nao utawaitaje.alafu tabia kukurupuka na kutukanana sio sifa ya waislamu,mie pia najua matusi tena pengine kuliko wewe so jiheshimu.

Sent using Jamii Forums mobile app
C__Data_Users_DefApps_AppData_INTERNETEXPLORER_Temp_Saved Images_FB_IMG_1498446553489.jpeg
C__Data_Users_DefApps_AppData_INTERNETEXPLORER_Temp_Saved Images_FB_IMG_1498446553489.jpeg
 
Sina tafsiri sahihi ya hili neno "uhuru wa kuabudu" ila naona kama watu wanaitafsiri tofauti wanapitiliza.

K7na nyumba ya ibada hapa jirani huwa wanaamsha watu kwa ajili ya kuswali lakini maneno anayotumia ni ya kuogopesha mpaka kuleta tahruki katika familia yangu.

Naweza kumnukuu "Amkeni mkaswali hizo nyumba zenu hapa naona kama ni makaburi na hicho kitanda ulicholalia ni kama jeneza hilo shuka ulilojifunika ndo sanda amkaaaaa amkaaa".

Haya maneno yakikuamsha usingizini huwezi kulala tena, hii inapelekea familia nzima kushindwa kulala.

Nafikiria kupata msaada wa kisheria.

Sent using Jamii Forums mobile app
We mshtakie Mumgu tu[emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji124] [emoji125] [emoji125] [emoji377] [emoji377] [emoji377]

[emoji56][emoji94][emoji109]with my weather[emoji23][emoji23]
 
Suluhisho:
1.Amka ukaswali
2.Lala na earphone
3.Weka vioo nyumba yako
4.Hama huo mtaa
5.Ongea na huyo jamaa abadilishe maneno, badala ya kuweka vitisho, atumie maneno yenye mvuto. Kama vile, njoo uswali upate mafanikio, ufaulu mitihani, upate kazi, upone maradhi, swalaaa.
 
Kweli wewe ni ILLEGAL MIGRANT ndo maana huwa hamna ADABU,

Nyumba ya IBADA huwa ni tofauti na nyumba za MAIGIZO YA IBADA.

Halafu unachukia kuamshwa,USINGIZI wa alfajiri hauna FAIDA yoyote ni Uzembe tu,

Na pia unachukia kukumbushwa KIFO, utake usitake WOTE TUTAKUFA TU,

Hela na Nguvu ya kufungulia KESI ziweke kwenye IBADA NA SADAKA na sio kwenye UPUMBAVU.

karibu sana jitahidi pia utii na mamlaka zilizokuwa juu yako ili uwe LEGAL MIGRANT.
Ibada ni kwa ajili yako, usitese wengine.
Haina maana kuamka usiku saa 11 na kuanza kupiga kelele zinazoamsha wengine pengine hata hawahusiki na ibada yenu maana kila mtu ana ibada yake. Kuwasaidia toeni ibada zenu katikati ya makazi ambapo mnajikuta mnasumbua wengine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haahaah zile kelele za walokole za vilio usiku kucha hazikukwazi achen utani na dini za wenzenu
Wote batili na wanapaswa wajihoji namna wanasali. Mi siangalii we mkrisyo, baniani ama muislam. Wote wanatukosea na ni ujinga kuamini kila mtu afuate utakavyo.
Biblia inakataza kusali kwa kupayuka payuka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukhanisi huo. Amkeni mkaswali. Unataka kumshtaki kwa faida yako mwenyeo. Kamshtaki uwone Kitakachotokea. Niko Tayari kufa na ww kwa lolote lile na liwe. Unafikiri Allah atakutizama t

Sent using Jamii Forums mobile app
Baadhi ya waislam mfano wewe jifunzeni ustaarabu maana hata dini sidhani inaruhusu hayo makelele ya kupayuka mtaani mpaka watu washindwe kulala. Hujalala kwangu unajuaje kama Nina mgonjwa, watoto wadogo wanaohitaji kulala n.k???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Suala la kuuliza kwa waislam wezangu .Je Mtume wa Mwenyezi Mungu S.A.W..aliwahi kuamsha watu asubuhi kwa maneno kama hayo ?au masahaba zake waliwahi?na kama hajafanya yeye kwa nini tufanye sie ?haya maneno ya naweza kusema kwenye kuwapa mawaidha waislam .sio kufanya kama nguzo ya kuamsha watu kwenda kusali .tumefundishwa adhana na kwa watu wa nyumbani kwako kuwaamsha ikiwa wamo kulala .

Sent using Jamii Forums mobile app
Una hekima sana, pamoja na kwamba unaonekana ni islamic ujajibu kwa jazba...ubarikiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ibada ni kwa ajili yako, usitese wengine.
Haina maana kuamka usiku saa 11 na kuanza kupiga kelele zinazoamsha wengine pengine hata hawahusiki na ibada yenu maana kila mtu ana ibada yake. Kuwasaidia toeni ibada zenu katikati ya makazi ambapo mnajikuta mnasumbua wengine.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kama hutaki tabu kwenye dunia hii JIUE
 
Habari za saizi wakubwa me ni mgeni humu ndani,ila pamoja na ugeni wangu,nimeingia na jambo moja ambalo lanikera sana,nikuhusu msikiti mmoja ambao upo karibu na hapa kwangu huo ni msikiti wa wazee,lakini me naweza sema ni wazee waliyokosa ustaarabu,kwasababu kila siku usiku mida ya saa nane au saa tisa wanawasha maiki na kuanza kulazimisha watu waamke kuswali,na siyo muda huo tuu kila baada ya swala hasa swala ya alfajiri wanapiga kelele mpka saa moja kamili,sasa naombeni ushauri niende kwenye vyombo vya dola nikashtaki au nifanyeje,please naombeni ushauri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom