Habari wakuu,
Nimwaka wa tano sasa nasumbuliwa na :
Maumivu makali shingoni yakiambatana na misuli ya shingoni kukaza.
Uti wa mgongo unakaza pamoja na maumivu kila siku. Siwezi kukaa kwa muda mrefu bila kuegemea sehem.
Taya za mdomo zinakaza, nikipiga mwayo huwa Nasikia Kama mifupa iliyokaza inaachia.
Kifua Kina kaza kiasi nikivuta pumzi kwa nguvu husika mifupa inaachia Kama vile ilikuwa imekaza.
Uchovu wa mwili kila siku ni sehemu ya maisha yangu.
Nimeenda Sana hospital lakini nimeishia kuandikiwa Mi antibiotics mpaka nimechoka.
Msaada nifanyenini ili niondokane na maumivu haya?
Nawasilisha.
Geogismimi etc..