Msaada: Nawezaje kufuta account ya mtu ambaye alishafariki Facebook?

Mkogoti

TAPELI Mkubwa
Joined
May 3, 2020
Posts
2,415
Reaction score
3,924
Habari waugwana wa humu, je salama!?

Ok. Sasa bwana mimi nina shida moja kuna account ya mtu wangu wa karibu alishafariki alikuwa na account Facebook na mpaka sasa nikiwa napita kuona baadhi ya vitu lazima nikutane nayo.

Je, naomba nataka niwaambie Facebook waifute nifanyeje msaada wenu
 
Ndio inawezekana uchotakiwa inabidi uwe na login details za mtu huyo?
Fuata taratibu hizi
Settings>personal account and information>account ownership and control>deactivation and deletion>delete account
Baada ya kudelete account itakaa siku 60 ndipo itafutika Ila hakikisha ndani ya siku 60 hizo hau login kwenye hiyo account


 
Hii mpaka uwe umemchagua atakayecontrol account yako baada ya wewe kuondoa katika uso wa dunia hii.
Kama mimi nilivyochagua .
 

Attachments

  • Screenshot_2021-11-04-11-41-09-72.jpg
    68.4 KB · Views: 24
Mkuu sina details zake ya account yani niseme tu sijui ata namba gani!? Alifu gulia si unajua watu wazima
 
Duu mkuu account yake sina details zake kabisa,
 
Msaada mdogo na rahisi ni kuwa, kama shida ni wewe kuona picha zake na kuumia/kuwaza mbali basi mblock tu, hutoona tena hizo picha labda ukachungulie kwa Facebook ya mwingine.
 
Msaada mdogo na rahisi ni kuwa, kama shida ni wewe kuona picha zake na kuumia/kuwaza mbali basi mblock tu, hutoona tena hizo picha labda ukachungulie kwa Facebook ya mwingine.
Mkuu nimekucheck pm🙏😞
 
Kuna process kwa kifupi ili kufuta account ya facebook ya mtu wako wa karibu aliyefariki nenda help center na unatakiwa kuwa na
  • Jina lako kamili
  • barua pepe (email) ambayo facebook wanaweza kuwasiliana na wewe
  • Facebook watahitaji uthibitisho kuwa wewe ni mtu wa karibu wa mtu aliyefariki
  • Jina la marehemu
  • Link ya profile ya facebook ya marehemu ukianza na Facebook – kirjaudu sisään tai rekisteröidy...
  • Email ambayo ilitumika ku-create hiyo facebook account
KISHA
Utakutana na option mbili tatu ila chagua remove this account because the account owner is deceased.
Baada ya hapo utatakiwa kuambatanisha picha ya cheti cha kifo ambacho hakijafanyiwa editing ya aina yoyote hata ku-crop kisha submit.

Subiri siku kadhaa akaunti itaondolewa.
 
Block Acc kama shida ni kuiona acc

Kama kuna ulazima sana wa kuifunga mdau hapo juu kadadafua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…