Microsoft
JF-Expert Member
- Mar 18, 2011
- 623
- 366
Wadau naomba kwa wenye uelewa juu ya hili suala.
Mzazi alikuwa mfanyakazi wa shirika moja linaitwa PLAN INTERNATIONAL hapa Dar, alifariki mwaka 2014.
Baada ya msiba ndugu wakakaa kikao wakamteua mdogo mmoja wa marehemu (hakimu hapa Dar) msimamizi wa mirathi, na wakaamua hela itakayopatikana kutoka katika mafao ya marehemu inunue nyumba Dar es Salaam, alafu hiyo nyumba itakuwa ni mali ya mtoto pekee wa marehemu. Mafao yake yakatoka 2015.
Hela baada ya kutoka (ambayo cheque pia ilikua katika jina la mtoto wa marehemu) ikaingia katika account ya mtoto wa marehemu.
Baada ya hapo mdogo wa marehemu (msimamizi wa mirathi) anakabidhiwa ATM card ili atimize maamuzi ya kikao.
Kilichotokea huyu mjomba amekula baadhi ya hela, maadhimio ya kikao kwamba anunue nyumba hakutekeleza, baada ya kuanza kuulizwa akawa mbogo, mpaka sasa kanunua nyumba ambayo bado hakumalizia kulipia na hataki kuilipia mpaka sasa hana dalili.
Ushahidi upo baada ya ku print bank statement inaonyesha huyu msimamizi wa mirathi amekula Milioni 10.
Huyu mtu anafanya hivi kwasababu ni hakimu wa mahakama moja hapa Dar kwahiyo anaona yeye anaijua sheria kuliko wengine.
Kwa sasa sitataja jina lake ila tarehe 28/Feb nitaleta picha yake hapa, jina kamili Hapa
Najua anasoma kwahiyo uamuzi ni wake.
Msaada ni naomba kujua jinsi ya kumshtaki ili:
1. Alipe hela aliyokula takribani milioni 10
2. Akabidhi nyumba kwa muhusika
3. Naomba kujua kama ninaweza kudai fidia maana tangu hela itoke 2015 mpaka leo ananizungusha na matusi ananitukana nikiuliza.
Kama kuna mwanasheria yupo tayari kunisaidia kupata haki yangu basi reward ipo.
Updates:
Baada ya kufungua huu uzi napata simu za watu nisiowajua wanajifanya wao wananijua na wanataka eti tuonane.
Na kwa habari nilizopata huyu mtu yupo mahakama ya UPANGA kwa sasa.
Mzazi alikuwa mfanyakazi wa shirika moja linaitwa PLAN INTERNATIONAL hapa Dar, alifariki mwaka 2014.
Baada ya msiba ndugu wakakaa kikao wakamteua mdogo mmoja wa marehemu (hakimu hapa Dar) msimamizi wa mirathi, na wakaamua hela itakayopatikana kutoka katika mafao ya marehemu inunue nyumba Dar es Salaam, alafu hiyo nyumba itakuwa ni mali ya mtoto pekee wa marehemu. Mafao yake yakatoka 2015.
Hela baada ya kutoka (ambayo cheque pia ilikua katika jina la mtoto wa marehemu) ikaingia katika account ya mtoto wa marehemu.
Baada ya hapo mdogo wa marehemu (msimamizi wa mirathi) anakabidhiwa ATM card ili atimize maamuzi ya kikao.
Kilichotokea huyu mjomba amekula baadhi ya hela, maadhimio ya kikao kwamba anunue nyumba hakutekeleza, baada ya kuanza kuulizwa akawa mbogo, mpaka sasa kanunua nyumba ambayo bado hakumalizia kulipia na hataki kuilipia mpaka sasa hana dalili.
Ushahidi upo baada ya ku print bank statement inaonyesha huyu msimamizi wa mirathi amekula Milioni 10.
Huyu mtu anafanya hivi kwasababu ni hakimu wa mahakama moja hapa Dar kwahiyo anaona yeye anaijua sheria kuliko wengine.
Kwa sasa sitataja jina lake ila tarehe 28/Feb nitaleta picha yake hapa, jina kamili Hapa
Najua anasoma kwahiyo uamuzi ni wake.
Msaada ni naomba kujua jinsi ya kumshtaki ili:
1. Alipe hela aliyokula takribani milioni 10
2. Akabidhi nyumba kwa muhusika
3. Naomba kujua kama ninaweza kudai fidia maana tangu hela itoke 2015 mpaka leo ananizungusha na matusi ananitukana nikiuliza.
Kama kuna mwanasheria yupo tayari kunisaidia kupata haki yangu basi reward ipo.
Updates:
Baada ya kufungua huu uzi napata simu za watu nisiowajua wanajifanya wao wananijua na wanataka eti tuonane.
Na kwa habari nilizopata huyu mtu yupo mahakama ya UPANGA kwa sasa.