Msaada nifanye nini niwe na amani?

Msaada nifanye nini niwe na amani?

Kwanza pole sana kwa yaliyokupata, naandika kwa herufi kubwa "USIACHE KAZI" pasipo kupata kazi sehemu nyingine. Pia tambua kila penye riziki mambo ya majungu hayokosekani.
Habari yako imenigusa sana, kwani nami napitia changamoto hizo hizo mpaka muda huu nipo kitandani. Nilipata ajali ya gari nikavunjika nyonga ikabidi nifanyiwe upasuaji wa kubadilishwa nyonga. Tatizo linakuja ninayoyasikia yanayoendelea huko kazini yanaumiza sana.
pole sana kaka,, mola akupe afya njema tena, maumivu yake nayajua
 
Acha kujiliza mkuu, pambana wewe ni mwanaume. Hiyo kampuni kwani ni ya baba yako? Anza kuchakarika kutafuta kazi nyingine upesi sana na kwa kasi. Shida ya kukaa kampuni moja miaka kibao hadi unazoeleka na kuonekana huna jipya tena.

TAFUTA KAZI SEHEMU NYINGINE, KISHA UKIPATA U RESIGN HAPO UPESI. Ujifunze sasa, usikae tena organization moja muda mrefu unless ni kampuni yako au ya baba yako, kukaa kampuni moja muda mrefu ni recipe nzuri sana ya uvivu, uzembe, majungu,kufanya kazi kwa mazoea (business as usual) na maslahi (mshahara) hafifu.

Mimi sehemu niliyokaa sana nilikaa miaka mitatu. Kampuni zingine zote ni kati ya mwaka mmoja hadi miaka miwili, nimeishia zangu...!!Unaondoka kila mtu anasikitika anataka ubaki. Kanuni yangu nikianza tu kazi, baada ya mwaka mmoja naanza kutafuta kazi nyingine.
Mwingine anaweza kupambana kutafuta kazi usiku na mchana na asipate mkuu.
 
Pole sana...

Screen Shot 2023-04-07 at 09.50.27.png
 
Usiondoke hapo. Ukijiengua kila pasipo na amani hata nchini kwako utaondoka maana kote kuna mapichapicha. Shukuru hata una kazi, wengne tunazitafuta hatari.

Wewe ni mwanaume. Jisemeshe kwamba hili nalo litapita. Ni nyakati tu ambazo huwa hazilast muda mrefu. Afu nikupe tip..acha kusikiliza maneno ya watu. Ingia ofisini, fanya kazi, ondoka. Kaa katika nafasi yako vizuri. Afu saiv shukuru umepata ample time ya kufanya mitikasi mingine. Buni mambo kichwani, umiza akili yako ili upate mradi ama biashara ingine (kama huna) ambayo itakuingizia kipato.

Makazini hakunaga true friends kunakuwaga na unafiki sana, hvyo establish boundaries..afu usipende kushiriki katika kuongelea ama kujadili co-worker wenzako. Ukishiriki katika hayo mambedha, na wewe utakua unajadiliwa tu. Maana unakua umepanda mbegu..utavuna matunda yake.

Lakini pia nakuasa..sikulazimishi, sijui wewe ni dini gani ndugu. Katika dini ama imani yako..tafuta kumjua muumba wako. Jizoeze kuishi maisha ya uchaji na ibada. Sisemi uwe addicted kwenye mambo ya Imani..nope, namaanisha seek your Lord because kuna this peace huwa inakuja. Hasa pale unapokumbuka ahadi au neno kutoka katika vitabu vya dini. Kuna namna ufahamu wako utakuwa rejuvinated vizuri mno. Ila kama ulikuwa mchaji, ongeza kiwango chako cha ibada more and more. Panda viwango..kama ulikua hufungi, funga atleast once or twice per week. Kufunga huwa inasaidia sana kushape nafsi zetu..na kutiisha miili yetu.

Maisha sio kwenda staight..hamna iyo. Maisha yana kupanda na kushuka. Accept hapa umeshuka..lakini hiyo ni stepping stone...kuna accelerator unaiendea itakayokulift higher than stage uliyotoka...Stay strong..it shall pass.
[emoji817][emoji2935][emoji122]

Mungu akubariki sana.
 
Back
Top Bottom