nilimpeleka ndugu yangu muhu2 kitengo cha mifupa[moi] wananizungusha pesa nimelipa mizunguko kibao mgonjwa hajapata huduma na mm naona bora nitafute hosp nyingine.wana jf kuna uwezekano kwa siku mbili tatu kupata ufumbuzi.nisaidien
Ndugu
my web pole sana. Ninashangaa sana kwamba umelipia oparesheni MOI wakati hujapangiwa hata siku ya upasiaji. Ni jambo lisilokubalika, ikiwa kweli imetokea.
Lakini ndugu zangu wana JF, msidanganyane kuhusu kuwapo madaktari wazuri wa mifupa nje ya MOI kwa hapa Tanzania. Cream yote ya madaktari wa mifupa Tanzania inakimbilia MOI maana wanalipwa vizuri.
Nawaonea huruma watu wasemao kuna madaktari Peramiho, Ikonda et al, ambazo ni hospitali za mission. Hospitali hizi hutembelewa mara kwa mara na madaktari kama vile toka Ujerumani, ambao huja kufanya upasuaji kwa watanzania kama wanajifunza vile. Ila watu wakiguswa na mzungu huona washapona.
Dr. Baki si mzuri wa kila eneo la mifupa, na amekuwa incompetent katika mengi. Watu huishia kulalama.
TATIZO LA MOI
Tatizo lililo wazi MOI ni foleni za wagonjwa wanaolipa hizi gharama za serikali ili wapate tiba. Wagonjwa wa ajali za Bajaj na bodaboda nao wamekuwa mzigo.
USHAURI
Mtafute daktari anayehusika na tatizo alilonalo mgonjwa halafu akusaidie kumtibu mgonjwa kwa fast track. Ni gharama, lakini ina reflect gharama halisi ya tiba kwa sasa, maana gharama zile zinazolipwa na kusababisha watu wachelewe kufanyiwa operation zinahusisha cost sharing toka serikalini, kitu ambacho serikali inaelekea kushindwa.
Si shauri mgonjwa kupelekwa Mbeya, Bugando, CCBRT au KCMC kwa kuwa vitengo vyao vichanga sana, labda awe na issue ndogo.