Msaada: Siku sita tangu nianze dawa za TB nasikia maumivu makali sana ya uti wa Mgongo

Msaada: Siku sita tangu nianze dawa za TB nasikia maumivu makali sana ya uti wa Mgongo

Tanzania kuna "Doctor" alimwambia mtu kuwa ana TB akakndamizwa madawa akawa anazidiwa tu, ndugu zake wakampeleka India huko baada ya vipimo vya uhakika akakutwa hana TB ana acidity tu imemfanyia ulcers inamsumbua. Katibiwa siku tatu, karudi mzima wa afya.

Tanzania tiba ni majanga kusema kweli.
we kilazaa hapo umemsaidia ushauri gani Mtanzania mwenzetu
 
Jmn eeh nina maumivu makali sana tena sana kwny uti wa mgongo na leo ndio sku y 6 tu tangu nianze dozi za TB

Naomben ushauri jmn hii ndio TB tu au kuna tatzo nyngne maana doctor amenijibu endelea na dawa 2 ila nateseka nmelala kitandan napata maumivu makali kwny uti wa mgongo jmn msaada

Sent using Jamii Forums mobile app

Vipi lakini unapata mlo wa kushiba kwa wakati? Pamoja na maziwa usikose kula kila baada ya masaa manne na mwulize Dr wako kama unaweza kutumia pain killer ya Flamar

Wanaojua zaidi nisahihisheni kama nimekosea
 
Jmn eeh nina maumivu makali sana tena sana kwny uti wa mgongo na leo ndio sku y 6 tu tangu nianze dozi za TB

Naomben ushauri jmn hii ndio TB tu au kuna tatzo nyngne maana doctor amenijibu endelea na dawa 2 ila nateseka nmelala kitandan napata maumivu makali kwny uti wa mgongo jmn msaada

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole mkuu hizo dawa wakati mwingine huwa zinasumbua mpaka mwili uje uzizoee ni ndani ya wiki mbili.
Pia sio vibaya ukisema upo mkoa gani ili tuone ushauri uende hospital ipi.

Kwa Dar huu ugonjwa unakuwa kwa kasi sana hasa kwenye mwendokasi
Na mara nyingi inakuwa ni MDR

Serikali iutazame sana huu mradi kwa jinsi watu wanavyojazana kwenye hayo mabasi
 
Ok me npo Dar
Pole mkuu hizo dawa wakati mwingine huwa zinasumbua mpaka mwili uje uzizoee ni ndani ya wiki mbili.
Pia sio vibaya ukisema upo mkoa gani ili tuone ushauri uende hospital ipi.

Kwa Dar huu ugonjwa unakuwa kwa kasi sana hasa kwenye mwendokasi
Na mara nyingi inakuwa ni MDR

Serikali iutazame sana huu mradi kwa jinsi watu wanavyojazana kwenye hayo mabasi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanzania kuna "Doctor" alimwambia mtu kuwa ana TB akakndamizwa madawa akawa anazidiwa tu, ndugu zake wakampeleka India huko baada ya vipimo vya uhakika akakutwa hana TB ana acidity tu imemfanyia ulcers inamsumbua. Katibiwa siku tatu, karudi mzima wa afya.

Tanzania tiba ni majanga kusema kweli.
Leo bibi umeongea pointi kubwaaa,sijapata kuona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Members naona wengi wamekuwa wakichanganywa na maelezo ya mara kwa mara yaani post nyingi halafu kila moja inaelezea hali tofauti niliyonayo.

Nimeona niweke full mkanda:
Nilipelekwa hospital nilikiwa sijitambui kwa case ya kupata pumzi yaani kuhema sana pumzi fupi fupi na hewa yaani shida nilihudumia na masindano dakika kadhaa nilihisi napata pumzi vyema, nilipoongea na doctor kumuuliza hii ni nini akasema ni PNEUMONIA hiyo basi nilipigwa sindano kila baada ya masaa 6 na dawa nyngne nikajihisi nipo fresh na hata wao waliniruhusu wakijua tatizo limekwisha na mimi nikiamini naenda kusikilizia siku kadhaa nasimama vizuri na nilikuwa nishafanya Xray tayari.

Sasa ajabu ni kwamba baada ya kurud home naweza sema homa ilizidi zaidi maana wakati naruhusiwa nilikuwa naweza hata kutembea ila hapa nyumbani nilikuwa nashindwa hata kukaa na kusimama muda wote nilikuwa nalala tu kuhema so niliwasiliana na doctor kumuelewesha hiyo hali aliniambia baadhi ya antibiotics zikagonga mwamba hapo ndo akanishauri nikapime TB aliniongoza nikapime wap nilipelekwa lakini wakati huo mimi nilikuwa sina kikohozi chochote mpaka kule hospital walishindwa kunipima waliamua kunianzisha dozi kutokana na maelezo na ile hali ya kushindwa kukaa na kukutembea na kuhema sana kohozi sikuwapatia wakanambia hyo ni TB wewe nenda katumie baada ya wiki mbili utaanza kuwa fresh basi nilizichukua nikaanza jumanne ile ile.

Sasa nikiwa kwenye hii tiba ndio matatizo yanazidi maana ile hali ya kushndwa kuinuka bado ipo na nahema kwa shida sana na dawa nazingatia

siku ya jana nilihema hema usku kucha nikahc nikitumia dawa za tb ndan y muda wake itatulia lkn nilitumia na nilihema sana na kikohoz ambcho kilitokana na kukosa hewa y kutoshaa ikaonekana itanpa shida maana ukiwa unatumia dawa za tb lazma ule na chakula ni shida maana pumzi imebanwa

nilikimbizwa hospital kupewa huduma y kwnza kupumua nilipotulia nkapelekwa hospital moja y wilaya hpa dar

sasa hawa jamaa wanachodeal nacho ni pumzi na wameniweka kitengo cha pumzi na mashine y kupumulia na kujisaidia na wkt huo dawa za TB nazitumia ila wanadeal sana na pumzi na mimi ninavyojiona changamoto yngu ni pumzi ndo imebak i tu

Nikifkria mchakato wa mimi kuanzishwa dawa za TB na nikiangalia kinachonisumbua naona tofauti inawezekana sina kutokana kwamba sina dalili zake au imo kwahyo natumia dawa za TB nikiwa sina uhakika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duuuh!! Only in Tanzania!
Unamuamzishia mgonjwa madawa makali na ya muda mrefu kama ya TB while hujamfanyia diagnosis kujua kweli ana TB, aisee nimetetemeka!! Pole sana ndugu, Mungu atakuponya!
 
Hao majamaa sio wajinga! We piga dozi mwanzo hata Mimi nilishindwa kuhema wakanipa dawa za TB wakaniambia ndani ya wiki 2 nitapona cha kushangaza nilipiga dozi miezi 2 ile Hali ikakata saivi Nina mwezi toka nimalizie dozi ya miezi 6 Niko fiti kuliko awali
 
Mkuu dawa za TB zinasumbua sana wiki mbili za kwanza ila baada ya hapo unapata relief .

Last two years nilikuwa na TB hata mimi sikuwa nakohoa wala nini ila nilikuwa naihisi maumivu tu chini ya mbavu upande wa kulia na nikiinama nilikuwa nahisi kama napaliwa na maji hivi. Uzito ulipungua mpaka nikafika 39Kgs kiasi kana kwamba hata mimi mwenyewe nilikuwa najiogopa. Kila nikienda hospitali walikuwa wananibadilishia dawa tu hivyo mwisho wa siku wakanipeleka kitengo cha TB.

Zile wiki mbili za kwanza nilipata athari za aina tofauti kama vile irritation ya whole body hivyo nilipewa dawa ya kuzuia hizo athari eventually after six months ya kutumia dawa za TB nili gain uzito wangu halisi na sasa hivi nipo poa sina tatizo lolote la kiafya.

Ushauri wangu kwako mkuu tumia dawa kwa usahihi ili uweze kupona vizuri TB huwa inachukua muda sana kugundulika kwa hivi vipimo vyetu vya hapa Tanzania. Unakuta mtu ameshateseka sana ndio anakuja kugundulika dakika za mwisho.
 
Back
Top Bottom