Msaada: Tatizo la muwasho kwenye njia ya haja Kubwa

Itakuwa ww ni mlaji mzuri wa 🐷🐷🐖
Hapana sili nguruwe, sema ni msomaji mzuri. Huwa sipendi kutowa jibu au majibu yasi na uhakika, mtandao mbona upo waz, kinachosababisha kuwashwa huko ni minyoo na mnyoo mingi ipo kwenye nguruwe kkuliko kwengine kokote, sasa hata ukiitibu minyoo kama unaendelea kula nguruwe, mwasho lazima uendelee.

Hilo ni mojawapo, lingine ni kutojisafisha kwa maji baada ya haja kubwa. Kujifuta kwa au kujipangusa kwa makaratasi baada ya haja kubwa kunababisha muwasho huko.

Kuna sababu nyingi lakini hizo ni za kuzitazama mwanzo na kubadilisha tabia.

Tatizo likiendelea unakwenda hospitali.
 
Mkuu nenda hospitali.Watakufanyia kipimo kinaitwa endoscopy. Majibu yatokanayo na kipimo hiki yatamsaidia daktari kukuandikia dawa ambayo ukiitumia utapona.
 
Dawa za safura
 

PRURITUS ANI

Muwasho kwenye njia ya haja kubwa, husababishwa na:

1: Fangasi
2: Bakteria

NB: Hapa unaweza kupata mchanganyiko wa vyote. Fangusi pamoja na bakteria. Njia rahisi huwa ni kutimia dawa yenye mchanganyiko wa dawa dhidi ya bakteria, fangus na muwasho. Unaweza kufanya hivyo kwa kunawa vyema na kupaka dawa.

3: Minyoo
Hapa suluhisho huwa ni kupata dawa ya minyoo. Kuna aina ya minyoo ambayo hutoka nje wakati wa usiku ili kutaga mayai, huwa ni chanzo kikubwa cha muwasho.

4: Michubuko vs kuchanika/fissures:
Hii inaweza kusababishwa na choo kigumu au kujikuna mwenyewe baada ya kupata muwasho.

Suluhisho:
Kuhakikisha unapata choo laini na kupata dawa ya muwasho. Choo laini hupatikana kwa kunywa naji ya kutosha kulinhana na uzito, kazi na hali ya hewa uliyopo, kula matunda kwa wingi pamoja na mbogamboga.

5: Aina ya vyakula
Ukishapata madhira maeneo husika, vyakula vifuatavyo vyenye kuleta muwashawasha huongezea tatizo: pilipili, kahawa, tangawizi, chocolate nk.
Hivyo, ni vyema kujizuia na vyakula husika.
 
Una moyo mdau shida kama hii unaleta jamvini!? Hata kama ni anonymous lazima kwa kejeli za humu utajisikia vibaya.
 
Hiyo ni dalili ya minyoo, nenda hosp kapime minyoo, utakuja nishukuru hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…