Msaada: Tatizo la ng'ombe kupepesuka na kutoa udenda anapolala

Msaada: Tatizo la ng'ombe kupepesuka na kutoa udenda anapolala

kingzard

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2017
Posts
636
Reaction score
809
Habari wakuu,

Mimi ni mfugaji wa naombe nilipata changamoto wa ngombe wangu kufa kwa tatizo la kutokula na kutoa udenda pia anapepesuka akitembea. Baada ya kufa alipasuliwa tumbo na kukutwa na maji tumboni na nyongo yake ni kubwa sana na nyeusi sana pia.

Baada ya siku tatu tatizo likaanza kwa ndama dume naye akafa.

Sasa ivi kwa siku 6 zilizopita tatizo limenza kwa mwingine na kuonyesha dalili za wengine kama mwanzo la kutokula majani pia amedhohofika sana na akitembea anapepesuka sana pia anatoa udenda.

Nimemuita daktari wa mifugo kata kaja kampima na kumdunga shindano (kasema ya kushusha joto) akaondoka na hali ya ngombe imekua mbaya zaidi. Naombeni msaada kwa madaktari dawa ya kutatua tatizo. Au namna na jinsi yoyote.

Asan
 
Habari wakuu,

Mimi ni mfugaji wa naombe nilipata changamoto wa ngombe wangu kufa kwa tatizo la kutokula na kutoa udenda pia anapepesuka akitembea. Baada ya kufa alipasuliwa tumbo na kukutwa na maji tumboni na nyongo yake ni kubwa sana na nyeusi sana pia.

Baada ya siku tatu tatizo likaanza kwa ndama dume naye akafa.

Sasa ivi kwa siku 6 zilizopita tatizo limenza kwa mwingine na kuonyesha dalili za wengine kama mwanzo la kutokula majani pia amedhohofika sana na akitembea anapepesuka sana pia anatoa udenda.

Nimemuita daktari wa mifugo kata ..kaja kampima na kumdunga shindano (kasema ya kushusha joto) akaondoka na hali ya ngombe imekua mbaya zaidi .. Naombeni msaada kwa madaktari dawa ya kutatua tatizo. Au namna na jinsi yoyote.

Asan
Pole sana mkuu na changamoto ulizopitia na unazoendelea kupitia, baada ya hapo hebu twende pamoja ili tuweze kukusaidia

Kwanza kitu cha kujua ni kwamba uchunguzi sahihi hukupa dawa sahihi, na baada ya kupata dawa sahihi ndipo kupona kunakuja

Kwa dalili ambazo umesema Ng'ombe wako walikuwa nazo hasa hao wa Kwanza, hapo kuna uwezekano walikuwa na magonjwa yafatayo

1.Homa ya mapafu, ambapo mnyama anakuwa anapata shida ya kuhema,kuchoka sana,kutembea akiwa hana nguvu na mwisho kuwa anatoa mate mdomoni

Lakini pia hizo shida za kupumua huambatana na dalili za mafua na kifua, kwahiyo mnyama anaweza kuwa anatoa makamasi au anaweza kuwa anakohoa sana

na mnyama akichinjwa huwa anakuwa na maji mengi sana katika sehemu ya mbavu/kifuani na yanakuwa kama ya njano hivi

Matibabu yake ni kumchoma huyo mnyama dawa ambayo inatibu maradhi ya mfumo wa hewa, ambayo inaweza kuwa Tylosin 20%, Amoxicillin 15% au Enrofloxacin 10% hizi zote ziwe injection

Na hizo dawa zitatumika Kwa siku 3-5 inategemea na maelekezo ya dawa husika, lakini pia kama mnyama hana Mimba utachoma Dexamethasone ili kwenda kuondoa Athari za mapafu ambazo mara nyingi huwa ni kujaa Maji



2.Ugonjwa wa miguu na kwato, huu mnyama akiupata anakuwa anasumbuliwa na vidonda kwenye midomo pamoja na kwenye kwato, na mara chache kwenye kiwele

Hivo vidonda hupelekea mnyama kutoa mate mdomoni ambayo huning'inia lakini pia hukosa hamu ya Kula maana vidonda hushambulia ulimi pamoja na kinywa chote

na mwisho kabisa mnyama akipata vidonda vya kwenye miguu hufanya ashindwe kutembea au kusimama na ata akisimama/kutembea huwa anatembea upande upande

Haya yote utayajua endapo tu utachukua muda wako na kumchunguza vizuri mnayama wako, Kwa kuanzia katika kinywa hadi miguuni, ukikuta tu vidonda mdomoni unajua kuwa huu ugonjwa ni wa kinywa na kwato hivo unaangalia na kwato pia

Endapo kama shida ndio hiyo, basi unaanza Kwa kusugua na chumvi vidonda vya kwenye kinywa hadi Damu zitoke au viwe visafi kabisa na kisha unafatia kusugua pia vidonda vya kwenye kwato kama vipo

Baada ya hapo utamchoma mnyama wako dawa ya Penstrep 20% high dose au Gentamicin 10% high dose pia au sulfa high dose pia, ila kama utatumia sulfa inabidi uchome asubui na jioni Kwa siku 3 ila hizo zingine unachoma Kwa siku mara 1

Na ikibidi ununue na dawa ya vidonda ya kuspray (wound spray) baada ya kuwa umesafisha vidonda unapulizia hiyo Kwa ajili ya kutibu vidonda lakini pia kuzuia infections ambazo zinaweza kusababishwa na kidonda

Kwahiyo zingatia hizo dalili na uhakikishe kabla ya kutumia dawa uwe umejiridhisha na uchunguzi utakaoufanya. All the best
 
Tumia dawa inaitwa Penistrip hakikisha iwe ya kampuni ya BIMEDA choma kwa siku tatu

Ng'ombe wagonjwa watenge
 
Pole sana mkuu na changamoto ulizopitia na unazoendelea kupitia, baada ya hapo hebu twende pamoja ili tuweze kukusaidia

Kwanza kitu cha kujua ni kwamba uchunguzi sahihi hukupa dawa sahihi, na baada ya kupata dawa sahihi ndipo kupona kunakuja

Kwa dalili ambazo umesema Ng'ombe wako walikuwa nazo hasa hao wa Kwanza, hapo kuna uwezekano walikuwa na magonjwa yafatayo

1.Homa ya mapafu, ambapo mnyama anakuwa anapata shida ya kuhema,kuchoka sana,kutembea akiwa hana nguvu na mwisho kuwa anatoa mate mdomoni

Lakini pia hizo shida za kupumua huambatana na dalili za mafua na kifua, kwahiyo mnyama anaweza kuwa anatoa makamasi au anaweza kuwa anakohoa sana

na mnyama akichinjwa huwa anakuwa na maji mengi sana katika sehemu ya mbavu/kifuani na yanakuwa kama ya njano hivi

Matibabu yake ni kumchoma huyo mnyama dawa ambayo inatibu maradhi ya mfumo wa hewa, ambayo inaweza kuwa Tylosin 20%, Amoxicillin 15% au Enrofloxacin 10% hizi zote ziwe injection

Na hizo dawa zitatumika Kwa siku 3-5 inategemea na maelekezo ya dawa husika, lakini pia kama mnyama hana Mimba utachoma Dexamethasone ili kwenda kuondoa Athari za mapafu ambazo mara nyingi huwa ni kujaa Maji



2.Ugonjwa wa miguu na kwato, huu mnyama akiupata anakuwa anasumbuliwa na vidonda kwenye midomo pamoja na kwenye kwato, na mara chache kwenye kiwele

Hivo vidonda hupelekea mnyama kutoa mate mdomoni ambayo huning'inia lakini pia hukosa hamu ya Kula maana vidonda hushambulia ulimi pamoja na kinywa chote

na mwisho kabisa mnyama akipata vidonda vya kwenye miguu hufanya ashindwe kutembea au kusimama na ata akisimama/kutembea huwa anatembea upande upande

Haya yote utayajua endapo tu utachukua muda wako na kumchunguza vizuri mnayama wako, Kwa kuanzia katika kinywa hadi miguuni, ukikuta tu vidonda mdomoni unajua kuwa huu ugonjwa ni wa kinywa na kwato hivo unaangalia na kwato pia

Endapo kama shida ndio hiyo, basi unaanza Kwa kusugua na chumvi vidonda vya kwenye kinywa hadi Damu zitoke au viwe visafi kabisa na kisha unafatia kusugua pia vidonda vya kwenye kwato kama vipo

Baada ya hapo utamchoma mnyama wako dawa ya Penstrep 20% high dose au Gentamicin 10% high dose pia au sulfa high dose pia, ila kama utatumia sulfa inabidi uchome asubui na jioni Kwa siku 3 ila hizo zingine unachoma Kwa siku mara 1

Na ikibidi ununue na dawa ya vidonda ya kuspray (wound spray) baada ya kuwa umesafisha vidonda unapulizia hiyo Kwa ajili ya kutibu vidonda lakini pia kuzuia infections ambazo zinaweza kusababishwa na kidonda

Kwahiyo zingatia hizo dalili na uhakikishe kabla ya kutumia dawa uwe umejiridhisha na uchunguzi utakaoufanya. All the best
Duh... Daktari unarecommend kutibu CBPP aisee!? sawa unatibu lakini sio option ya kwanza. FMD haisababishi vifo kwa ng'ombe kiivyo.
 
Habari wakuu,

Mimi ni mfugaji wa naombe nilipata changamoto wa ngombe wangu kufa kwa tatizo la kutokula na kutoa udenda pia anapepesuka akitembea. Baada ya kufa alipasuliwa tumbo na kukutwa na maji tumboni na nyongo yake ni kubwa sana na nyeusi sana pia.

Baada ya siku tatu tatizo likaanza kwa ndama dume naye akafa.

Sasa ivi kwa siku 6 zilizopita tatizo limenza kwa mwingine na kuonyesha dalili za wengine kama mwanzo la kutokula majani pia amedhohofika sana na akitembea anapepesuka sana pia anatoa udenda.

Nimemuita daktari wa mifugo kata ..kaja kampima na kumdunga shindano (kasema ya kushusha joto) akaondoka na hali ya ngombe imekua mbaya zaidi .. Naombeni msaada kwa madaktari dawa ya kutatua tatizo. Au namna na jinsi yoyote.

Asan
Unafugia wapi ndugu?
 
Ndio madhara ya kukamua asubuhi saa sita na jioni akiwa na njaa .
Hiyo ni homa ya mapafu tafuta dokta amchome avomeki super.
 
Duh... Daktari unarecommend kutibu CBPP aisee!? sawa unatibu lakini sio option ya kwanza. FMD haisababishi vifo kwa ng'ombe kiivyo.
Mkuu jamaa amehitaji ushauri na hapo nilikuwa nipo katika harakati za kujaribu kumsaidia kulingana na uelewa wangu

Nadhani ingekuwa vizuri sana na wewe pia ungeshauri na sio kuishia kukosoa au kukejri na kubakia kumwacha mfugaji njia panda ilhali amehitaji msaada, ungeshauri inawezekana ungekuja na solution nzuri zaidi na wengine tukajifunza pia

Na nimeongelea FMD Kutokana na dalili ambazo yeye amezitaja, na istoshe me sijamuoma mnyama wake hivo kazi inabaki kwake kufanya uchunguzi na kujiridhisha shida ni nini, na kumbuka ndomana kuna Differential diagnosis

Na kumbuka CBPP mkuu hivi sasa imekuwa ni kama vile malaria tu katika sehemu kubwa ya Nchi yetu hivi sasa, hivo tunaishia kutibu tu Kwa sababu inatokea sana katika endemic areas

NB: Mimi sio daktari Ila nimelelewa na kukulia katika familia ya ufugaji na hadi leo hii nafuga na Mzee wangu ndio alikuwa daktari wa wilaya Fulani, kwahiyo at least nina uzoefu wa kutibu Mifugo yangu mwenyewe matatizo madogo madogo na shida zingine ndio huita Daktari Kwa msaada Zaidi

Pamoja na kwamba me sio Daktari ila waga sina ubinafsi linapokuja swala la kujaribu kumshauri/kumsaidia mtu ambae anapitia changamoto humu JF endapo nitahisi naweza kusaidia, maana madaktari wa JF wao wanasubir kukosoa watu na sio kusaidia
 
Mkuu jamaa amehitaji ushauri na hapo nilikuwa nipo katika harakati za kujaribu kumsaidia kulingana na uelewa wangu

Nadhani ingekuwa vizuri sana na wewe pia ungeshauri na sio kuishia kukosoa au kukejri na kubakia kumwacha mfugaji njia panda ilhali amehitaji msaada, ungeshauri inawezekana ungekuja na solution nzuri zaidi na wengine tukajifunza pia

Na nimeongelea FMD Kutokana na dalili ambazo yeye amezitaja, na istoshe me sijamuoma mnyama wake hivo kazi inabaki kwake kufanya uchunguzi na kujiridhisha shida ni nini, na kumbuka ndomana kuna Differential diagnosis

Na kumbuka CBPP mkuu hivi sasa imekuwa ni kama vile malaria tu katika sehemu kubwa ya Nchi yetu hivi sasa, hivo tunaishia kutibu tu Kwa sababu inatokea sana katika endemic areas

NB: Mimi sio daktari Ila nimelelewa na kukulia katika familia ya ufugaji na hadi leo hii nafuga na Mzee wangu ndio alikuwa daktari wa wilaya Fulani, kwahiyo at least nina uzoefu wa kutibu Mifugo yangu mwenyewe matatizo madogo madogo na shida zingine ndio huita Daktari Kwa msaada Zaidi

Pamoja na kwamba me sio Daktari ila waga sina ubinafsi linapokuja swala la kujaribu kumshauri/kumsaidia mtu ambae anapitia changamoto humu JF endapo nitahisi naweza kusaidia, maana madaktari wa JF wao wanasubir kukosoa watu na sio kusaidia
Pole sana. Labda ulikua huijui JF vizuri. Kunae kunguni hizo ni wajuajiii alafu hawana msaada wowote.

Angalau na yeye angetoa ushauri. Ila karukia kukosoa na kukimbia.

Pole ila usichoke kusaidia watu kwa kile ulichonacho kichwani
 
Pole sana. Labda ulikua huijui JF vizuri. Kunae kunguni hizo ni wajuajiii alafu hawana msaada wowote.

Angalau na yeye angetoa ushauri. Ila karukia kukosoa na kukimbia.

Pole ila usichoke kusaidia watu kwa kile ulichonacho kichwani
Shukrani mkuu

Me nawajua vizuri wataalamu wetu wa jf ndomana waga sichoki kutoa msaada wa kimawazo pale ambapo itanihitaji kufanya hivo

Sasa mtu anahisi anafahamu namna ya kutatua shida fulani ila hachangii mawazo yoyote anasubiri watu wachangie ye akosoe

Hiyo ni hali ni mwendelezo wa kutokujiamini Kwa wasomi wetu au ni ule usomi unaoishia kwenye makaratasi ila katika field mtu anakuwa hana mchango wowote
 
Muda mwingine hawa madaktari wa mifugo wanafanya kazi kwa kubahatisha, mwaka 2018 mimi na mjomba wangu ( tunashare ng'ombe wa kienyeji japo yeye ndo anao wengi) tulipoteza ng'ombe 72 mfululizo mpaka alitaka kuwa kichaa.

Unamuita anakuha na dawa anachoma unashangaa ng'ombe anazidi kudhoofika anakufa, kidogo wengine nao wanaambukizana Dr akija tena anakuja na solution nyingine (yani ni kama anabahatisha tu).

Zilibaki ngo'mbe 29 tu, tukaamua kuzihamishia sehemu moja inaitwa Lubaga.
 
Muda mwingine hawa madaktari wa mifugo wanafanya kazi kwa kubahatisha, mwaka 2018 mimi na mjomba wangu ( tunashare ng'ombe wa kienyeji japo yeye ndo anao wengi) tulipoteza ng'ombe 72 mfululizo mpaka alitaka kuwa kichaa.

Unamuita anakuha na dawa anachoma unashangaa ng'ombe anazidi kudhoofika anakufa, kidogo wengine nao wanaambukizana Dr akija tena anakuja na solution nyingine (yani ni kama anabahatisha tu).

Zilibaki ngo'mbe 29 tu, tukaamua kuzihamishia sehemu moja inaitwa Lubaga.
Ni kweli kabisa Mkuu kuna changamoto kubwa sana kwenye issue ya madaktari wa Mifugo

Bahati mbaya hili lilichangiwa na serikali yetu, kuna hawa waliosoma kilimo na Mifugo wanafahamika kama general agriculture

Hawa watu waliajiriwa sana na serikali Kwa ajili ya kuokoa gharama za kulipa mishahara kwani walikuwa wakiajiriwa wanaenda kufanya kazi zote mbili yani ya Afisa kilimo na wakati huo huo Afisa mifugo

ila ukweli ni kwamba hawa jamaa hawako competent kabisa kwenye issue ya Mifugo, ila kwenye kilimo wako vizuri sana yani vizuri Mnooo

Sasa hawa katika vyuo walivyokuwa wanasoma wamewekeza nguvu kubwa sana kwenye kilimo kuliko Mifugo, unakuta chuo kizima kina Ng'ombe 6 tu alafu wanafunzi wapo 3000, sasa hapo mwanafunzi atajifunza nini kuhusu Mifugo

ila chuo hicho hicho kina hekari Hadi 2000 za mashamba ya mazao na wanafunzi wanashinda huko na kila mwanafunzi ana shmaba lake la kulima na kusimamia sasa sangapi atajua kuhusu Mifugo na huyo ndio anaenda kuwa Afisa mifugo wa kata

Kwahiyo ukimuita huyu daktari akutibie Mifugo yako anachofanya ni pata potea, hakuna anachojua ila atatibu tu kutokana na title anayoifanyia kazi hapo kwenye eneo lake

Madaktari wazuri ni wale ambao wametoka katika vyuo maalumu vya Mifugo tu kama vile vyuo vya Kati LITI na chuo kikuu SUA, japokuwa nawao wana changamoto zao kama kukosa uzoefu nk ila at least hawa wanakuwa wana idea na kile anachokifanya

Ukipata daktari wa SUA mwenye Degree ni mzuri zaidi ila hawapendi kuhudumia wafuga Ng'ombe maana wanasema sie hatulipi vizuri alafu kazi inakuwa kubwa, wanaona bora waishie kutibu Mbwa, paka,Farasi huko ndio wanapata malipo makubwa, ila ukipata mwenye Diploma anafanya kazi za matibabu vizuri sana bila kuchagua kazi

Kwahiyo serikali ndio kiini cha tatizo kwa kuajiri vijana wetu ambao wamesoma kilimo na Mifugo alafu wanaenda kuwa Afisa mifugo ilhali hawajui chochote, daktari anakuja kwako ata kipima joto tu hana huyo teyari ni wa kumtilia mashaka
 
Ni kweli kabisa Mkuu kuna changamoto kubwa sana kwenye issue ya madaktari wa Mifugo

Bahati mbaya hili lilichangiwa na serikali yetu, kuna hawa waliosoma kilimo na Mifugo wanafahamika kama general agriculture

Hawa watu waliajiriwa sana na serikali Kwa ajili ya kuokoa gharama za kulipa mishahara kwani walikuwa wakiajiriwa wanaenda kufanya kazi zote mbili yani ya Afisa kilimo na wakati huo huo Afisa mifugo

ila ukweli ni kwamba hawa jamaa hawako competent kabisa kwenye issue ya Mifugo, ila kwenye kilimo wako vizuri sana yani vizuri Mnooo

Sasa hawa katika vyuo walivyokuwa wanasoma wamewekeza nguvu kubwa sana kwenye kilimo kuliko Mifugo, unakuta chuo kizima kina Ng'ombe 6 tu alafu wanafunzi wapo 3000, sasa hapo mwanafunzi atajifunza nini kuhusu Mifugo

ila chuo hicho hicho kina hekari Hadi 2000 za mashamba ya mazao na wanafunzi wanashinda huko na kila mwanafunzi ana shmaba lake la kulima na kusimamia sasa sangapi atajua kuhusu Mifugo na huyo ndio anaenda kuwa Afisa mifugo wa kata

Kwahiyo ukimuita huyu daktari akutibie Mifugo yako anachofanya ni pata potea, hakuna anachojua ila atatibu tu kutokana na title anayoifanyia kazi hapo kwenye eneo lake

Madaktari wazuri ni wale ambao wametoka katika vyuo maalumu vya Mifugo tu kama vile vyuo vya Kati LITI na chuo kikuu SUA, japokuwa nawao wana changamoto zao kama kukosa uzoefu nk ila at least hawa wanakuwa wana idea na kile anachokifanya

Ukipata daktari wa SUA mwenye Degree ni mzuri zaidi ila hawapendi kuhudumia wafuga Ng'ombe maana wanasema sie hatulipi vizuri alafu kazi inakuwa kubwa, wanaona bora waishie kutibu Mbwa, paka,Farasi huko ndio wanapata malipo makubwa, ila ukipata mwenye Diploma anafanya kazi za matibabu vizuri sana bila kuchagua kazi

Kwahiyo serikali ndio kiini cha tatizo kwa kuajiri vijana wetu ambao wamesoma kilimo na Mifugo alafu wanaenda kuwa Afisa mifugo ilhali hawajui chochote, daktari anakuja kwako ata kipima joto tu hana huyo teyari ni wa kumtilia mashaka
Wewe unaelewa nilimaanisha nini, kuna shida sana kwenye hiyo sekta.
 
Back
Top Bottom