MSAADA: Tatizo la vitu kutembea mwilini


Mimi sijafanya meditation ni third eye ambayo iko yenyewe tangu nikiwa mtoto
 
Pole kwa kuumwa.

Ili kupata amani ya moyo, hii inaitwa TACTILE HALLUCINATIONS (FORMICATION). Ni matatizo yanayotokana na athari kwenye mfumo wa ubongo na afya yake. Ni tatizo mtambuka toka kwenye(ORGANIC VS INORGANIC) Maumbile vs Saikolojia vs Experience.

Unahitaji kutulia na kuhudumiwa na mtaalamu wa afya kwa kufuata mlolongo wa comprehesive managements. Huitaji kufanya vipimo hapa na pale (dedicate physician/daktari wa magonjwa ya ndani anaweza kukusaidia sana).

Mawazo ya kulogwa na.mengine ya kukutia hofu hufanya hali kuwa mbaya zaidi.

Hii huusisha:

1: Uchukuaji mzuri wa historia yako ya afya kwa ujumla.

2: Historia ya mapito yako ya zamani na sasa.

3: Saikolojia yako ya maisha na afya

4: Maisha yako kwa ujumla, kazi, familia, marafiki, dini au mahusiano na Muumba.

5: Maisha na maana yake. Malengo vs Mipango vs Ufanisi katika maisha.

6: Stress/matumizi ya pombe/matumizi ya dawa/ ulaji wa chakula ni sehemu muhimu hapa.

7: Kufanyiwa physical examination

8: Kufanyiwa vipimo kulingana na mwelekeo wa mtoa huduma nawe mtakavyokuwa mmelielewa tatizo.
 
Nenda kwa mganga Kigoma kwa kina Zitto Kabwe
 
Nyunyuzia damu ya YESU kwa imani kwenye mwili wako mpaka pale hivyo vitu vinavyotembea vitaisha
 
Huo mzunguko mbaya wa damu unasababishwa na nini na tiba ya hospital huwa ni nini au haipo?
Vitu ni vingi vinavyoweza kusababisha ,inaweza kuwa matatizo ya moyo, Figo au mishipa ya damu. Utaandikiwa dawa kutokana na diagnosis uliyokutwa nayo. Nenda hospitali kubwa kafanye vipimo vikubwa
 
Vitu ni vingi vinavyoweza kusababisha ,inaweza kuwa matatizo ya moyo, Figo au mishipa ya damu. Utaandikiwa dawa kutokana na diagnosis uliyokutwa nayo. Nenda hospitali kubwa kafanye vipimo vikubwa

Nimetoka muhimbili nimepima siumwi kabisa
 
Nimetoka muhimbili nimepima siumwi kabisa
Mara nyingine hospitali kubwa nao wanabahatisha.

Inawezekana kutokana na fatigue ya kazi nyingi, au umemkuta mtu ambaye hajabobea au umeshindwa kujieleza vizuri akishindwa kupata plan ya vipimo.

Kuna jamaa yangu aliwahi kuwa na changamoto ya kiafya, alihangaika hospitali zote kubwa za rufaa Tanzania na vipimo vikubwa Sana. Aliambiwa ugonjwa hauonekani, alikonda Sana na kukata tamaa ya kuishi hadi alipohamia karibu na nyumbani kumsubiri mapenzi ya Mungu Cha kushangaza ugonjwa ulienda kuonekana kwenye hospitali ya Kijiji alipona hadi leo
 
Weka picha...
 
Moja wapo ya dalili za maambukizi ya VVU ni kuhisi Vitu vinatembea Mwilini. Pima Haraka maana ukichelewa vinajitokeza kama Mkanda wa Jeshi, Herpes Zoster
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…