Msaada wa connection CRDB Bank kwa anayeweza nisaidia

Msaada wa connection CRDB Bank kwa anayeweza nisaidia

Wakiangalia mzunguko, si lazima uwe kwenye benki unayoombea mkopo... Jipange vizuri... bank statement unazo, taarifa ya biashara unayo, leseni za biashara unayo, usajiri wa biashara ( Brela ) fanya mchanganuo wa biashara yako, ukiwa na document zote hizo , with confidence nenda uongee na meneja wa tawi la karibu na dhamana yako ilipo.... Usisikie wanakupa majibu gani... ....Mabenki wanatafuta sana watu wa kukopa.. Sijajua unachukua mkopo kwa ajili ya nini na unafanya biashara gani..

Kumbuka benki hawatoi mkopo kuanzisha biashara , wanatoa mikopo ya biashara kukuza mtaji, au uzalishaji unaoendelea...

Kama hayo yote , uko tayari nenda benki mbalimbali, lakini anza na NMB... halafu angalia benki walio karibu na dhamana yako ilipo.... Inamaanisha wilaya au kata ya karibu ... Ziangalie benki zenye muelekeo huo.
maana CRDB hawa hawa wana Branch huko dhamana ilipo sasa najiuliza hawa wakisema n mbali je hao wenzao walioko huko je? nmewaza kama wewe mkuu nitafute bank ambapo dhamana ipo ila nawaza Biashara itakua mbali na wao Je hayatokua yale yale?? tupotezeane muda?

Unajua CRDB niliwategemea kwa kiasi kikubwa sana maana mimi ni WAKALA wao PIA, yani hii bank wamenikera mpaka sijui nisemeje, na laiti wangeniambia haya yote nisinge hangaika mimi.
 
Valuation report lazima iwepo maana sio wao wanaidhinisha mikopo direct, wao watapitisha lakini lazima makao makuu wapelekewe wajadiliane ili kuidhinisha mkopo, sasa bila ya valuation report watajuaje dhamani halisi ya dhamana yako??

Kuna bank kama Azania wameanza ukuda, wanatoa si zaidi ya 50% ya thamani inayoonekana kwenye valuation report
valuation ikija 17m maana yake mkopo wako hupewi zaidi ya 50% asee huu ni ukuda mno.

Sasa mtu anamiliki nyumba ina range 15m to 17m ana biashara ya capital yakutosha unakuja umwambie umpe mil 7 si matusi haya?

wakati mil 7 ni hela unayoweza kupewa na ACCESS BANK hata bila dhamana yani biashara yako tu inakudhamini huna nyumba wala kiwanja 7m access wanakupa.. ila BANK hizi mpka nyumba aseee
 
Ni majuzi hapa nimeomba MKOPO wa CRDB kwenye biashara wakahitaji vielelezo vyote nikawapa.

Dhamana ipo (nyumba) iliyopo 25km tokea High Way, wakaenda itembelea dhamana wakajitidhisha ila wakaniambia POLICY yao haiwaruhusu kukopesha dhamana iliyo mbali kiasi hicho.

Wakaniambia kwamba nitafute dhamana nyingine, ndugu zanguni kichwa kimegandana.

Mkopo wanasema umeahapitishwa ilibaki dhamana tu hela iwekwe,

Biashara iko vizuri
Mzunguko uko vizuri
Account iko vizuri
Kila kitu kipo vizuri

Dhamana eti wanasema ipo mbali naombeni msaada wenu tafadhali.

Kama kuna mtu anaweza nisaidia swala langu kwa Kuongea na TOP of the top kwenye mikopo,anisaidiea nitatoa PERCENT kidogo ikihitajika.

Naombeni tu yeyote anaeona anaweza nisaidia hili basi nitashukuru.

Asante.

Hadi leo unahangaikaje na benki moja kama unapewa hela bure?

Mambo mengine unajitakia mwenyewe, kuna benki ukienda leo siku 2 wameshakupa hela kutegemea na kiwango.

Wewe ni mfanyabiashara gani, napata mashaka hata kama unavyonunua mzigo usikute umeng’ang’ana na msambazaji mmoja bila kutazama masoko mengine.

Wake up comrade!!
 
Hadi leo unahangaikaje na benki moja kama unapewa hela bure?

Mambo mengine unajitakia mwenyewe, kuna benki ukienda leo siku 2 wameshakupa hela kutegemea na kiwango.

Wewe ni mfanyabiashara gani, napata mashaka hata kama unavyonunua mzigo usikute umeng’ang’ana na msambazaji mmoja bila kutazama masoko mengine.

Wake up comrade!!
Mfano wa hizo bank za chap chap n zipi mkuu,nipe mwanga boss wangu
 
Hadi leo unahangaikaje na benki moja kama unapewa hela bure?

Mambo mengine unajitakia mwenyewe, kuna benki ukienda leo siku 2 wameshakupa hela kutegemea na kiwango.

Wewe ni mfanyabiashara gani, napata mashaka hata kama unavyonunua mzigo usikute umeng’ang’ana na msambazaji mmoja bila kutazama masoko mengine.

Wake up comrade!!
kuna mtu alini tonya CRDB wako faster mkuu na alienipa hyo taarifa ni staff wa crdb ndiomana ila sio kwamba nawaganda sana CRDB.
 
Mfano wa hizo bank za chap chap n zipi mkuu,nipe mwanga boss wangu

Hiyo ni home work ndogo sana, sidhani kama kuna ulazima wa kuzitaja hapa nazo zaweza kuwa na changamoto zake.

Nilitaka ufanye kazi yako kwa usahihi ilifanye maamuzi. Kukopa kuna mambo mengi sana sio tu hilo la uharaka.

Fanya tathminikwa kutembelea sehemu ulipo na benki zilizopo, pata taarifa kwa wenzako hao staff baadae sana.
 
valuation ikija 17m maana yake mkopo wako hupewi zaidi ya 50% asee huu ni ukuda mno.

Sasa mtu anamiliki nyumba ina range 15m to 17m ana biashara ya capital yakutosha unakuja umwambie umpe mil 7 si matusi haya?

wakati mil 7 ni hela unayoweza kupewa na ACCESS BANK hata bila dhamana yani biashara yako tu inakudhamini huna nyumba wala kiwanja 7m access wanakupa.. ila BANK hizi mpka nyumba aseee
Ndo hivo mkuu, valuation yenyewe ni bei ghali nyumba ya kawaida labda wakufanyie kwa laki 5, na bado mkopo unaweza usipate

Bank hawataki hasara kabisa, ukishindwa Wanataka wakipiga mnada iwe rahisi wao kuuza ndo maana nyumba ya 15M watakupa kama 8M tu....

Na bado hapo utakatwa pesa ya bima ya mkopo
 
Back
Top Bottom