Msaada wa kimawazo: Nahisi naanza kupata depression

Msaada wa kimawazo: Nahisi naanza kupata depression

Ndugu yangu mleta uzi nakaribia kufanana nawe kimazingira yaliyonitokea.
Nikiwa na miaka 27 kama wewe nilioa mwanamke ambaye tayari nilikuwa na mtoto nae ingawa nami kwa kipindi hicho nilikuwa na ndoto nyingi sana na suala la kuoa lilikuwa mbali kabisa na fikra zangu.
Ila mimi niliamua 'kuscrifice' baadhi ya ndoto zangu kwa ajili ya ustawi wa mwanangu na mapenzi ya mwanamke wangu.
Leo hivi baada ya miaka 15 nami nikiwa baba wa watoto wanne maisha yanaendela na mapenzi yanazidi kustawi ndani ya ndoa yetu.
Wakati mwengine maisha ya ndoa na hatima ya tutakaokuja kuishi nao yanakuwa nje ya umiliki wetu.
Sasa huu ndio ushauri wa mwanaume. Mtoa mada kama ana akili inampasa kuchukua ushauri kwa watu wenye uzoefu kwenye suala kama lake.
 
Sasa wewe hufai kumshauri huyu mtoa mada ushafeli, tena ukute hapo kila mtoto na mama yake. Unadhani utakuwa na familia ya namna gani? Sahau familia bora hapo.
Poa uliyefaulu.

Endelea kufaulu mkuu.

#YNWA
 
Kuna mambo mawili nitakushauri.
1. Wewe ndio utaishi naye. Kwa hio usifanye uamuzi mzito huu kwa kishinikizwa na Yeyote. Fuata moyo wako. Na kama moyo wako unasema hapana, basi Simama imara hapo. Sio wazazi wako, au wazazi wake, au yeye akushinikize. Maamuzi kama hayo ukifuata moyo wako. hautajuta hata siku moja.
2. Mchukue tu kama mke. Japo moyo haujaridhika. Ila mwanzishie mradi auendeleze. Na hapo ujue utachepuka sana sababu roho haijatulia kwa huyo. Itabidi akuvumilie tu kwa hilo.
Namuona new nyange in town
 
Furaha yako haipaswi kuibwa na yeyote yule


Kaa nae mbali mbali mok moyo utakaporidhia
 
Unaonekana ni mbinafsi sana,ukipata mtoto unatakiwa kuacha kujifikiria wewe peke yako!you have a family now,na unavyomuelezea huyo binti na uchunguzi wako uliofanya anaonesha anakupenda!fanya maamuzi sahihi utamkumbuka huyo dada baadae!Karma has no menu


Point nzuri Sana.

Mda anamkumbuka mda nao unakua haupo.
 
Dogo usioe kwanza. Komaa na na uamuzi wako huo huo. Huwezi jua kwanini huyo binti analizimisha sana mazingira ya kuolewa na wewe. Ukikaza na akajua uwezokano ndo wa ndoa ni mdogo ndo utaziona rangi zake vizuri.
Inawezekana alikua na mwamba mmoja kwa muda mrefu af mwamba kamzingua mwishoni, so now hataki kuchezewa tena, kakupata kaona upo fresh, una kipato kizuri, familia yako ipo straight hamna longo longo ndo kaamua alizimishe aolewe hapo.
Swali ni:
je anakupenda kweli?
Je akikuta hali ni tofauti na picha aliyonayo atavumilia?
Tabia zake unazijua kweli? Manake kaanza kutengeneza mazingira toka mnakutana, inawezekana anakuigizia, subiri uoe uone.

Ushauri wangu ni uendelee kukomaa na msimamo wako. Time will reveal everything.
Bro wangu kaoa mke wake baada ya mtoto kufikisha miaka mitano, na walikua mkoa mmoja lakini hakuwa akiishi na huyo mwanamke. Kapigiwa sana kelele lakini kakomaa na uamuzi wake. Siku alipokua tayari katoa taarifa tumefanya harusi mambo fresh tu mpaka leo.
 
Hao wanaokushauri uoe tu ndoa zao zinapumulia mashine. Wamejaza michepuko lukuki.
Namuelewa sana Mr. Liverpool, ingawa nimesoma kisa chake na mchungaji wake. Kweli mlango wa mbinguni mdogo sana.

Slogan yetu ni MITANO TENA
 
Another single mum....[emoji848][emoji848][emoji2827][emoji2827][emoji2827][emoji2827][emoji2827]
Single mum wa kujitakia lkn. A man came clean kwamba haitaji mke na asitegemee kama atamuoa, but akaamua kubeba ujauzito to keep him! Sasa hv bidada atajiona mshindi kweli kweli na hvyo wakwe wamemkubali! Ila atakuja kujuta baadae, ndoa itakuwa ndoano.

Usiombe uolewe na mwanaume hajakupenda, utaletewa michepuko nyumbani, atateseka sana kiakili na kihisia. Pole yake
 
Sikiliza moyo wako, masuala ya kuingia ndoani moyo haujaridhika utakuja kujuta na kuishia kumfanyia visa kwenye ndoa. Pia umri kama bado hivi angalau 30 ndio mzuri kuoa.

Sikiliza moyo wako, period. Maisha mafupi haya.
 
Unaonekana ni mbinafsi sana,ukipata mtoto unatakiwa kuacha kujifikiria wewe peke yako!you have a family now,na unavyomuelezea huyo binti na uchunguzi wako uliofanya anaonesha anakupenda!fanya maamuzi sahihi utamkumbuka huyo dada baadae!Karma has no menu
Nadhani thread ingefungwa hapa.
 
Ndugu, sio kila mara utaiendesha SITUATION, kuna muda SITUATION lazima ukubali ikuendeshe
 
Mwana kulitafuta, ukimwacha hyo mwanamke, kuna siku utajuta sana..ni suala la muda tu, Im telling.
Nina ndugu yangu kipindi ana mgogoro na mwanamke anayeishi naye baada ya kumfumania pia mke alikuwa mbinafsi hapendi ndugu wa mwanamme and blabla..
Jamaa akaja pata mwanamke mwingine mwalimu yupo simple wa kawaida tu sio mzuri kivile kama yule wa kwanza ila alikuwa anapendwa na kila mtu hasa upande wa jamaa. Akamzalisha kisha akaanza kumpotezea dada wa watu, akajaribu kubembeleza wee alivyokuja kugundua jamaa karudi kwa ex wake dada akaamua kumove on kimoja nakuendelea na mambo yake ya shule.
Yule dada leo hii ni proffessor pia alikuwa mtu mkubwa sana kwe serikali ya Kikwete, jamaa ni full kujuta full depression mambo yamemwendea vibaya mwanamke yuleyule wa mwanzo ni full kumsumbua, malaya ni malaya tu hadi huruma..
ANGALIZO
Hii ni kwa mwanamke na mwanaume..Huwa tunawachukulia poa sana wale tunaowaona wanatupenda sana na kuwafanyia visa huku tukiamini hawatatuacha bila kujua wao ndo wamebeba mustakabali mzima na maono na mafanikio ya maisha yetu..
 
Wahenga walisema...


Mkataa pema pabaya panamuita!!!



Ni hayo tu.

Alamsiki!
 
Mim nkafkir hata umepatwa na tatizo kubwa sana, au bidadada kakusngizia mimba. Kumbe unajaribu kuonesha vile hautaki kuchkua majukumu yako mpaka unapata depression,
Unataka uoe malaika au wa kwako ni special order
 
Kuna wakati wanaume sijui nini kinatupelekesha kwenye mioyo yetu, ukute huyo ndiye mke uliyepangiwa na Mungu lakini kwa kuwa huna utulivu wa moyo na nafsi unataka kufanya maamuzi ambayo baadae yatakugharimu...

Kumbuka mtoto wako wa kuzaa anauma sana, sasa unataka umuache yeye na mama yake bila kufikiria mara mbilimbili kwamba huko unakotaka kwenda ni kwa namna gani patakuwa salama kwako?
 
Mimi ni kijana, miaka 27. Ninaishi na kufanya kazi mkoani nyanda za juu kusini huku. Nina kazi nzuri na vibiashara vya hapa na pale vya kuniweka mjini. Nilikua na malengo mengi sana na swala la kuoa sikua nimelipanga kwa sasa. Sikua na uhusiano wowote serious.

Mwaka jana mwanzoni kuna binti nilikutana nae maeneo ya mjini, ni mzuri sana na ana kazi yake nzuri tu, very social na ana roho nzuri sana tulibadilishana contacts baadae tukaanza kuwasiliana na baada ya kama wiki tukafanya mapenzi.

Alionesha kunipenda toka tunakutana. Akataka tuendelee na uhusiano, nikamwambia sawa lakini nikamfahamisha kuwa mimi sina mpango wa kuoa hivi karibuni so kama ana mtafuta mwanaume wa maisha yake sio mimi kwa sasa.
Alilia sana siku ile nikajua tumeshaachana. Lakini baadae akanitafuta na kuniambia hana shida tuendelee.

Tukapima na kuendelea na uhusiano. Mara ya kwanza tulitumia kinga. Nkaona ili twende sawa, nijue mzunguko wake wa mwezi na lini yupo safe na lini yupo danger.

Baada ya miezi miwili akaniambia ana mimba ya wiki 3. Nikivuta picha katika hyo wiki ya kutunga mimba nilionana nae mara moja tu, nlikua busy sana na mdogo wangu alikua amekuja kwangu kipindi hicho, hyo siku alilazimisha sana tuonane na kunihakikishia kuwa yupo safe mpaka ikabidi twende lodge. Kwake alikua anaishi na binamu yake

Nkapata picha either mimba sio yangu au kanitegeshea. Nkamuita nkakaa nae chini na kuongea nae kwa kirefu sana. Nkamuambia kama mtoto sio wangu ntajua tu na hakuna kitakachoendelea kati yetu. Na hata kama ni wangu, siwezi kubadilisha plan zangu za maisha so asiwaze kabisa kama ataolewa coz amebeba mimba. Alichoniambia ni kuwa mimba ni yangu na anaomba walau shangazi yake aliekua anaishi huku mkoani anifahamu ili tumbo likitokeza atleast kuwe na idea ya aliempa mimba. ( kwa huyu shangaz yake ndo alikokua anaishi alipokuja kuripoti kazini kabla ya kupanga na binti wa huyo shangazi). Nkamuambia sawa lakini sijawahi kwenda huko wala kwao mpaka leo.

Nilifanya uchunguzi wangu mkali lakini sikuona kama kuna dalili yoyote kama mimba si yangu. Nkaona mtoto akizaliwa tutajua. Ilivofika miezi saba nilimshirikisha mama. Mama akasema anataka amuone. Nkamuomba mama aje na kweli alikuja na akaonana nae. Alipojifungua alienda kwao na gharama zote mimi ndo nlihusika na mpaka sasa nahusika. Baada ya kumaliza uzazi wazee wangu hasa baba wakataka wamuone yeye na mtoto, uzuri wote ni wastaafu so walikuja wakamuona. Tunaishi mkoa mmoja wilaya tofauti so wanakuja na kuondoka siku hyo hyo.

Huyu binti alivoona wazee wangu ni wastaafu na sisi watoto wote tuna kazi zetu na tupo busy sana na maisha akajiweka karibu nao. Weekends anaenda kushinda huko full kuwapikia na kuwafanyia mambo mengi. Mimi nilikua sijui coz siishi nae na huwa niko busy sana. Ratiba yangu ya kuonana na wazee ni mara moja kwa mwezi au sometimes kwa miezi miwili naenda mara moja. Changamoto ni kuwa wazee wamemuelewa sana na wananilazimisha niishi nae, na yeye kakomaa muda wote analia anataka aje tuanze maisha, home kwao nao wamechachamaa wanataka nikajitambulishe na nitoe posa.

I feel conerned, coz haya mambo hayakuwa plani yangu na najua huyu binti kanitegeshea mimba makusudi ili aolewe na ana wanipulate wazee wangu ili wawe upande wake. Mtoto najua ni wangu coz tunafanana sana, kachukua kila kitu kwangu. Nawaza sana kuhusu hili swala mpaka nmeanza ku apply kazi nje ya huu mkoa nikaanze upya.

I wish nipate mawazo tofauti labda ntajua cha kufanya.
Mkuu nawaza hiyo depression uliyosema hapa labda ni ya furaha! Mwanamke ni wife material kabisa huyu sijui unataka wa Aina gani, mtoto umekiri unafanana naye unataka nini tena? Wazazi ni watu wazima na wanafahamu mengi sana hawajaona kasoro kwa huyu binti wamekwambia umchukue wewe unataka ushauri wa jamii forum kuliko wa wazazi wako? Mimi naona depression inajipatia mwenyewe. Nakushauri kwamba kama huna Mpango wa kuacha kuoa basi mchukue huyu binti haraka mtoto wako asiteseke.
 
Ukimuacha huyo mama wa mtoto wako hakika utamkumbuka sana... Take care bahati haibishi hodi inakuja nje ya mipango yako .. ndoa tamu sana acha uoga vaa ujasiri mkuu
 
Back
Top Bottom