Msaada wa kimawazo

Msaada wa kimawazo

Habari yako mwana jf

Baba yangu alibahatika kuwa na mali nyingi sana na kwetu tumezaliwa wachache watu wa nne tu,

Sasa mzee ili kuondoka utata ameamua kugawa mali ingali yupo hai Mimi nimepata mgao wa nyumba ya kuishi pamoja na kiasi kama million 50

Kwa upane wa elimu nina degree ya agribusiness kutokea SUA
Pia binafsi sina background yoyote ya kufanya biashara maana mda mwingi nimetumia shuleni

Niliwaza hii pesa niiweke UTT baada ya kuisoma na kuifatilia Sana lakini changamoto inakuja nahofia usalama wa pesa yangu huko UTT hasa hasa kwenye nchi yetu hii ambayo kiongozi anaweza amua chochote mda wowote.

Naombeni ushauri je naweza anzia wapi katika uwekezaji.
Na je UTT ni salama mathalani kwa miaka 30 ijayo. Umri wangu ni miaka 25.

Pia ningeomba Kwa wenye kujua zaidi ni mkoa gani au eneo gani Tanzania ni zuri Kwa mtu mwenye mtaji kuanza biashara na biashara ipi inaweza kuwa na rejesho zuri.
Asanteni


Wanasemaga usiweke mayai yote kwenye kikapu kimoja
Ila kwa umri huo kama sio chai na unaogopa UTT basi kaweke hata fixed account for 10 yrs

Usisubutu kufanya biashara
Yaani usifanye biashara yoyote
 
Usirogwe utt it's better uweke fixed account kama 40mil then 10mil nenda tabora miezi ya kwanzia mwez wa 3 mpka 5 ununue tumbaku ikiwa tayr imekaushwa ipo kwenye vishada nunua kwa kupoint then uiuze kwenye masoko mda wa masoko ukifika ni uhakika haina ugai gai unapiga pesa zako unatulia
Unamaanisha Fixed ni bora kuliko UTT, Kwanini?

#YNWA
 
Hongera sana ni wachache sana wenye bahati kama yako. Una pesa nzuri, umri mzuri, ukitulia vizuri baada ya miaka 10 utakuwa mbali sana. Kuwa makini sana mdogo wangu na kila la kheri.
 
Usirogwe utt it's better uweke fixed account kama 40mil then 10mil nenda tabora miezi ya kwanzia mwez wa 3 mpka 5 ununue tumbaku ikiwa tayr imekaushwa ipo kwenye vishada nunua kwa kupoint then uiuze kwenye masoko mda wa masoko ukifika ni uhakika haina ugai gai unapiga pesa zako unatulia
Huu ushauri mzuri zaid
 
real hustler , msomi mwenzangu, nakushauri sana kwa vile hauna experience na biashara sana ila unataka kufanya biashara

Fanya hivi, Hio hela 50% iwekeze kwenye Ununuzi wa Ardhi.

Nunua viwanja Kwa Bei ndogo maeneo mazuri kama Goba, Kibaha kwa Matias huko ama Picha ya ndege (mimi niko Mwanza ila naona Mitandaoni wanauza viwanja huko)

Mfano ukinunua Kiwanja Tsh milioni 5, wewe anza kusaka wateja kwa Bei kubwapo kidogo.

Chunguza kwanza kabla hujanunua ardhi maana huko pia kuna seleka zake
 
Habari yako mwana jf

Baba yangu alibahatika kuwa na mali nyingi sana na kwetu tumezaliwa wachache watu wa nne tu,

Sasa mzee ili kuondoka utata ameamua kugawa mali ingali yupo hai Mimi nimepata mgao wa nyumba ya kuishi pamoja na kiasi kama million 50

Kwa upane wa elimu nina degree ya agribusiness kutokea SUA
Pia binafsi sina background yoyote ya kufanya biashara maana mda mwingi nimetumia shuleni

Niliwaza hii pesa niiweke UTT baada ya kuisoma na kuifatilia Sana lakini changamoto inakuja nahofia usalama wa pesa yangu huko UTT hasa hasa kwenye nchi yetu hii ambayo kiongozi anaweza amua chochote mda wowote.

Naombeni ushauri je naweza anzia wapi katika uwekezaji.
Na je UTT ni salama mathalani kwa miaka 30 ijayo. Umri wangu ni miaka 25.

Pia ningeomba Kwa wenye kujua zaidi ni mkoa gani au eneo gani Tanzania ni zuri Kwa mtu mwenye mtaji kuanza biashara na biashara ipi inaweza kuwa na rejesho zuri.
Asanteni


Hongera sana kwa kupata mgao kutoka kwa mzee wako. UTT ni wazo jema sana. Nipo huko kwa zaidi ya miaka mitano sasa na hakuna ubabaishaji. Ukiweka hiyo mil 50 ndani ya miaka 30 una zaidi ya 700m. Ni vema kufanya hivyo na kuisahau hela. Naweza kukupa uzoefu wangu zaidi. Kila la kheri
 
Back
Top Bottom