Msaada wa Kisheria: Mdogo wangu ametapeliwa Ardhi na rafiki yake wa karibu

Msaada wa Kisheria: Mdogo wangu ametapeliwa Ardhi na rafiki yake wa karibu

Polisi wanamzungusha inaonekana jamaa yake ana ushawishi upande huo maana walimwambia alitakiwa awe na copy ya mikataba ya mauziano ndo wampe loss report
Aliyemuuzia si yupo, mashahid wakati wa ununuzi wapo, serikali za mtaa wapo
 
huyo rafikiye aliingiaje ndani(nyumbani)kwa mdogo wako na kuiba documents za hivyo Viwanja??alivunja mlango??alitumia funguo bandia au ilikuaje??jibu kwanza hilo tujue maana kama Jinai inabidi ianzie hapo kwamba documents muuzaji alizipata vipi??
Alikua na tabia ya kumwamini kwa hiyo mara nyingi tu kabla ya tukio alikua akimwomba ufunguo anampatia
 
Umempiga dogo wa watu kwa Tamaa za kishamba sasa unatafuta huruma sikia mi ukinipiga pesa ndefu siptezi mda maana pesa inatafutwa kama ni tapeli najua nasaba yenu yote ni matapeli what next najua waganga hatari wote huko kwa msisi laki tano nakufanya kichaa wewe pamoja na ukoo wako utajuta

Yaani mm niko loyal ila ukileta chenga nakuharibia
 
Aliyemuuzia si yupo, mashahid wakati wa ununuzi wapo, serikali za mtaa wapo
Wote wapo tatizo polisi wanaleta ugumu kutoa loss report pia inaonekana mmojawapo wa wanunuzi wapya ni ndugu yake mwenyekiti wa mtaa
 
1.Viwanja vyote havina hati vina mikataba ya manunuzi ambayo ndo hiyo jamaa yake aliiba akaenda kuuzia
2.Miongoni mwa mashahidi wakati anakinunua ni mimi kwa viwanja vyote viwili na huyo jamaa yake alieviuza
3.Document zilikua na majina ya dogo ila aliuza muuzaji akisema kuwa amepewa ruhusa na mmiliki na akafake kwa kupiga simu akiwa na viongozi wa mtaa
Kuna uwezekano huyo rafiki yake na yeye wanashirikiana kuwaibia wanunuzi na ww hujui..

OTHERWISE:
Hiyo kesi ni nyepesi sana, Atafute mwanasheria wakafungue jinai ya wizi wa nyaraka na kufoji identity kisha rafiki yake akamatwe.

Atafute polisi mmoja kuwapa taarifa wamiliki kuwa mmetapeliwa na aliyewauzia na wasitishe ujenzi, Hawawezi kubisha kwa sababu hawajawahi kuonana na ambaye jina halisi linasoma kwenye nyaraka walizopewa bali aliwakilishwa.
 
Wanajamvi naombeni msaada wenu wa kisheria katika hili.Iko hivi nina mdogo wangu wa hiari(tumekutana kazini sina vinasaba nae) mnamo mwezi wa nne alisimamishwa kazi.Hivyo kutokana na majukumu ya kifamilia akaamua ajiingize kwenye biashara ya kununua mahindi na kuuza .Changamoto ikawa mtaji maana mzigo upo ila mtaji haukidhi akajaribu kuomba mikopo ikashindikana akaamua kuuza baadhi ya vitu vyake vya ndan kama tv,fridge na kiwanja kimoja(alikua na viwanja viwili).Mambo yote hayo alikua anayafanya na rafiki wa karibu sana ambapo walifanikisha kuuza vitu vya ndani kwa haraka kuliko kiwanja.Hivyo ikamlazimu dogo arudi vijijini kutafuta mahindi akampa taarifa huyo rafiki yake kuwa wasitishe zoezi la kuuza kiwanja.Wakati akiwa kijijini jamaa yake aliingia nyumbani kwa dogo akaibia document zote za viwanja akaenda akauza na hela akaenda akanunua gari ya kutembelea.Dogo akiwa kijijini aliibiwa hela tsh milioni tisa .Akaamua arudi mjini kuuza viwanja vyake aongezee mtaji maana tayari umepungua anakuta kiwanja kimoja kuna mtu anajenga kufuatilia anaambiwa kwenye uongozi wa mtaa anaambiwa viwanja vyake vimeuzwa viwili na alipigiwa simu siku vinauzwa na akatoa ruhusa(yeye dogo anadai hakupigiwa simu ).Ameenda polisi wamemuambia kama hana copy za document za ununuaji wa viwanja akubali tu maumivu wao hawana cha kumsaidia.Amejaribu kukutana na wamiliki wapya wa viwanja kwa maongezi ya usitishaji wa ujenzi lakini huyo rafiki yake anawaambia nyie endeleeni na ujenzi huyo hana documnet zozote asiwatishe. Sasa dogo amekwama asijue nini cha kufanya hivyo naomba kwa wenye ujuzi mtusaidie msaada wa kisheria hapa tunafanyaje.
watu wana uelewa hafifu sana juu ya sheria ya ardhi kwa maelezo ya hapo juu ni wazi kuwa huyo jamaa hana hati ni mikataba ile ya kiswahili tena inapigwa mihuri na muumbe hata serikali za kitaa hamuendi

sasa apo km hana hati ni kesi ndefu mnO pia vitu km mikataba ya ardhi au nyumba lazima ziwe na copy na lazima zifungiwe kuacha nje ni uzembe
 
Kuna sehemu roho mbaya inahitajika, kama huna iazime hata kwa jirani, huyo kenge ni wa kumteka, unamuacha siku 4 bila kula siku ya 5 unamkata kiungo kimoja unampikia ale, siku 3 unamkata kiungo kingine, mpaka anaisha
 
Chai gani hii?
Mkuu hujaweka hata majani sasa itanywewa vipi?
 
1.Viwanja vyote havina hati vina mikataba ya manunuzi ambayo ndo hiyo jamaa yake aliiba akaenda kuuzia
2.Miongoni mwa mashahidi wakati anakinunua ni mimi kwa viwanja vyote viwili na huyo jamaa yake alieviuza
3.Document zilikua na majina ya dogo ila aliuza muuzaji akisema kuwa amepewa ruhusa na mmiliki na akafake kwa kupiga simu akiwa na viongozi wa mtaa
Hakuna kitu kama hicho.

Huwezi kufanya transfer ya ardhi bila hati.

Fuatilia hilo kwa wanasheria wakusaidie.
 
Polisi wanamzungusha inaonekana jamaa yake ana ushawishi upande huo maana walimwambia alitakiwa awe na copy ya mikataba ya mauziano ndo wampe loss report
Alienda ardhi wataitwa walionunua,, wataulizwa aliyewauzia wakimleta watataka kujua aliipataje hiyo hati Sheria zipo wazi
 
Atafute mwanasheria na wale waliomuuzia kabla ya kuuzwa na huyo rafiki yake. Maneno ya mdomo yanatosha tu mbele ya sheria.
 
Wanajamvi naombeni msaada wenu wa kisheria katika hili.

Iko hivi nina mdogo wangu wa hiari (tumekutana kazini sina vinasaba nae) mnamo mwezi wa nne alisimamishwa kazi.

Hivyo kutokana na majukumu ya kifamilia akaamua ajiingize kwenye biashara ya kununua mahindi na kuuza.

Changamoto ikawa mtaji maana mzigo upo ila mtaji haukidhi akajaribu kuomba mikopo ikashindikana akaamua kuuza baadhi ya vitu vyake vya ndan kama tv, fridge na kiwanja kimoja (alikua na viwanja viwili).

Mambo yote hayo alikua anayafanya na rafiki wa karibu sana ambapo walifanikisha kuuza vitu vya ndani kwa haraka kuliko kiwanja. Hivyo ikamlazimu dogo arudi vijijini kutafuta mahindi akampa taarifa huyo rafiki yake kuwa wasitishe zoezi la kuuza kiwanja. Wakati akiwa kijijini jamaa yake aliingia nyumbani kwa dogo akaibia document zote za viwanja akaenda akauza na hela akaenda akanunua gari ya kutembelea. Dogo akiwa kijijini aliibiwa hela tsh milioni tisa

Akaamua arudi mjini kuuza viwanja vyake aongezee mtaji maana tayari umepungua anakuta kiwanja kimoja kuna mtu anajenga kufuatilia anaambiwa kwenye uongozi wa mtaa anaambiwa viwanja vyake vimeuzwa viwili na alipigiwa simu siku vinauzwa na akatoa ruhusa (yeye dogo anadai hakupigiwa simu)

Ameenda polisi wamemuambia kama hana copy za document za ununuaji wa viwanja akubali tu maumivu wao hawana cha kumsaidia.

Amejaribu kukutana na wamiliki wapya wa viwanja kwa maongezi ya usitishaji wa ujenzi lakini huyo rafiki yake anawaambia nyie endeleeni na ujenzi huyo hana documnet zozote asiwatishe. Sasa dogo amekwama asijue nini cha kufanya hivyo naomba kwa wenye ujuzi mtusaidie msaada wa kisheria hapa tunafanyaje.
Anaweza kupata haki,utaratibu wa mauziano ulikuwa batili
 
Back
Top Bottom