Msaada wa kujua suluhisho la kukabiliana na kuvimba na kubanduka kwa rangi katika kuta za ndani ya nyumba

Msaada wa kujua suluhisho la kukabiliana na kuvimba na kubanduka kwa rangi katika kuta za ndani ya nyumba

Joined
Nov 29, 2014
Posts
5
Reaction score
3
Nipo maeneo ya Zanzibar nahitaji sana msaada kwa anaefahamu jinsi ya kukabiliana na hili tatizo la kuvimba na baadae kubanduka kwa rangi katika kuta za ndani ya nyumba

home.jpg
 
Inasababishwa na unyevu unyevu na kusababisha fangasi za ukuta; utatatua nyakati hizi, baada ya muda tatizo linarudi. Ila kuna kemikali zinauzwa kwenye maduka ya vifaa vya ujenzi, unaweza tumia ili kupunguza tatizo.
 
hapo ni kubandua plasta na tofali kuitoa kuweka tofali jipya na plasta mpya ndani na nje... halafu skim na white cement halafu piga rangi upyaa...
 
bandua plaster iliyoharibika kuna dawa iko km unga unachanganya na cement unapiga plaster alafu baada ya hapo unachukua aina hiyo ya dawa ya maji unapaka kabla ya kuskim na white cement
 
Nyumba yako iko maeneo gani, karibu na bahari. Ukuta uliobanduka ni wa chumba gani/umeambatana na ukuta wa choo au ni ndani ya choo?
 
Kama plaster na skiming haikubanduka najuwa hao ni fangasi wanaosababishwa na unyevu nyevu, basi fanya hivi, nunu rangi inaitwa Binder paka harafu paka rangi harisi unayoipenda iwe nzito kidogo tatizo kwisha
 
Back
Top Bottom