Habari za maisha?
Nilimpeleka mke wangu hospitali hivi karibuni. Alikua na vipele vidogo vidogo pembeni na kwa ndani ya sehemu zake za siri. Kabla hatujaenda hospital tuli-google kidogo tunajua ni
Genital Warts au
Pearly Penile Papules (
PPP). Tulipofika kwa wataalamu wakampima na wakasema ni Genital Warts za mwanzoni maana alikutwa na
HPV virus +ve.
Tukaandikiwa dawa hizi tatu tukazitafute:
- Cobdilox Podofilox Gel 0.5%
- Salicyclic acid na
- Silver Nitrate
Mtaalamu alisema moja kati ya izo dawa itamsaidia.
Tumezunguka sana hapa mjini maduka makubwa makubwa ila hadi sasa hatujapata. Mtaalamualisema iyo ya kwanza ndio best ila hadi sasa tumekosa. Kwa sasa tunatumia dawa ya
Diplosalic Oinunent ina mchanganyiko wa Betamethasone Dipropionate na
Salicyclic Acid. Tumeitumia hii ndio tuliyoipata pharmacy kwakua ina Salicyclic Acid kamaalivoagiza mtaalamu.
Naomba msaada ambae anaweza kutusaidia wapi tunaweza ipata hiyo dawa. Na pia kama kuna mtu ana ujuzi zaidi wa huu ugonjwa anaweza kutupatia ushauri zaidi. Asanteni.