Msaada wa namna ya kutumia ebay

Msaada wa namna ya kutumia ebay

Konzogwe thumbs up your of great help
Nmeshaingia alibaba kwa mobile ila silijui logo la paypal au ni lipi kati ya hizo
Kama hakuna ulisema escrow pia ni safe na kama nikitaka kulipa kwa escrow inabidi niende kusign up kwenye website yao?

Thanks for appreciation!..katika alibaba utatakiwa ku sign up! Uwe na account ya alibaba ili uweze kufanya lolote. Baada ya kuwa na account sasa utafanya sourcing na ukipenda bidhaa angalia terms of payment na utaona supplier kaweka terms zake sijui T/T, WU, PayPal, Escrow etc. Ukishaona PayPal na/au Escrow amini huyo ni seller wa ukweli. Hatua inayofuata wewe angalia kama kuna link ya "BUY NOW", ukibofya hapo basi itaprompt uchague unalipa kwa VISA au MasterCard au Maestro au Western Union nk. Kwa njia yoyote utakayochagua elewa utakuwa protected na Escrow.

Na kama hautaona BUY NOW basi utaona "CONTACT SUPPLIER", hapo utaletewa dialog ya message utaandika hitaji lako na quantity ya vitu unavyohitaji. Supplier atakujibu na ndio utakua mwanzo wa Bargain yako. Mkikubaliana, atatengeneza CONTRACT kupitia Escrow ambayo wewe baada ya kuikagua kwa makini mfano jina lako, address, product name, specifications,quantity,...shipping terms je ni CNF,CFR au CIF uta sign/confirm online, then uta make payment online na utakua protected na Escrow. Ila kama seller atakwambia umlipe mojakwa moja kwa akaunti yake ya Bank (TT) au WU achana nae utaibiwa. Ila kama unalipa kwa WU,TT kupitia Escrow bado utakua safe! Hatari ni kulipa nje ya alibaba (Escrow).

Basi jitahidi kwa kutumia maelekezo hayo. Na ukikwama uni PM nikupe phone number yangu utanipigia maana si wakati wote nitakua na nafasi ya kukujibu hapa JF.
 
Asante sana na siwezi sema ni kwa vipi umekua msaada kwangu
 
thanx kwa darsa yako kaka mungu ndie atakae kulipa

Thanks for appreciation! Nimesaidiwa sana hapa JF hivyo sina kinyongo ku share chochote ninachokifahamu hapa JF....kwa hilo la Mungu nasema Amina nawewe Mungu akubariki zaidi yangu! Tupo pamoja, ukitaka msaada zaidi waweza uka PM ntakupa phone number yangu maana is wakati wote ntakua na nafasi kutiririka hapa JF
 
na mi nimefaidi kidogo!
ubarikiwe ww uliyetoa maelezo
 
Thanks for appreciation! Nimesaidiwa sana hapa JF hivyo sina kinyongo ku share chochote ninachokifahamu hapa JF....kwa hilo la Mungu nasema Amina nawewe Mungu akubariki zaidi yangu! Tupo pamoja, ukitaka msaada zaidi waweza uka PM ntakupa phone number yangu maana is wakati wote ntakua na nafasi kutiririka hapa JF

bro bac bora unipe no yako coz naweza kupata tatizo la haraka nikashindwa kulitatua coz hadi uingie JF
 
Kwa kawaida seller atakwambia njia zipi anatumia kulingana na nchi aliyopo,mfano Marekani kuna USPS (united states postal service), UPS Expedited, DHL and EMS. Hizo zote isipokuwa USPS ni international shipping companies na zipo karibu nchi zote.

Sasa basi, kwa kutegemea company gani inasafirisha mzigo wako ndo itadetermine wapi utapokelea mzigo, Mfano mimi nikitumiwa kwa DHL huwa wananiletea hadi nyumbani/ofisini maana wao hawatumii anuani za P.o. Box, wanataka anuani watakayokuletea hadi mlangoni, utaandika jina lako, ofisi gani upo au mtaa gani, nyumba namba ngapi, jiji na nchi ulipo unamalizia na namba za simu. Na kama utatumia anuani ya P.o.Box kuna garama inaitwa remote area charge USD30 itaongezeka, na wakiona vipi watakupigia simu ukachukue kwenye ofisi zao zitakazokuwa karibu. Huo utaratibu wanao pia UPS ila EMS wao wanatumia hata P.o. Box hivyo utachukulia kwenye sanduku lako la posta.

USPS, China Post, HongKong Post na mashirika mengine ya posta ya taifa huwa yanaleta kwa kupitia anuani za P.o.Box ila huwa zinachelewa ukilinganisha na express kama DHL,EMS na UPS.

Mimi huwa napokea mizigo karibu kila mwezi kwa kila aina ya shipping company hadi Bandari (sea freight), maana huwa naimport vitu vikubwa na vidogo yakiwemo magari na mitambo mbalimbali.

Kama una maswali zaidi endelea kuniuliza maana JF ni msaada wetu hata mimi nimesaidiwa sana hapa JF.

Shukrani mkuu
 
Back
Top Bottom