Nyenyere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 14,804
- 10,715
Wakuu, nimetakiwa kumsimamia mama mjane juu ya haki zake. Mama huyu aliolewa mwaka 1997 huko Mpanda na mume aliyekuwa na watoto wanne wakubwa. Baada ya mwaka mmoja mume aliyekuwa mfanyakazi alipewa redundance.
Wakaamua kuhamia DSM. Alitangulia mwanamume akatafuta nyumba ya kupanga. Wakati huo walikuwa na mtoto mdogo ambaye alifariki baadaye. Mume alimfuata mke wakaja kuishi DSM ambapo walizaa mtoto mmoja aliye sekondari hata sasa.
Mume alipata kazi ya korokoroni aliyokuwa akiendelea nayo hadi mauti ilipomkuta.
Wakiwa DSM walifanikiwa kujenga nyumba huko mbagala ambapo walikuwa wakiishi hadi mauti yalipomfika mume. Kazi ya mwanamke ni mganga wa tiba za asili.
Shida ni kuwa watoto wale wa mama wa kwanza pamoja na shehe (mume alikuwa mwislamu) wanadai kuwa nyumba waliyoijenga ni mali ya watoto pamoja na vitu vingine vyote. Huyu mama wanasema akabidhiwe kwa ndugu zake wao wauze nyumba watoto wagawane pesa. Wanasema huyu mama akaolewe tena huko kwao ilhali kajijengea nyumba na mumewe ili waishi hati mpaka mauti yawafike.
1. Je, sheria ya kiislamu inasemaje juu ya hili? Huyu mama aliyetumia muda na nguvu zake kujijenga na mumewe ni sahihi afukuzwe hapo?
2. Sheria za nchi zikoje katika hili? Mwanamke keshanyang'wa hati za nyumba na watoto, ingawa anao ushahidi tosha kuwa hiyo nyumba kaijenga na mumewe.
3. Leo ndio kuna kikao cha ukoo cha maamuzi, nahitaji msaada wa haraka katika hili.
Belo Daudi Mchambuzi zumbemkuu
[MENTION] Yericko Nyerere[/MENTION] Bujibuji Makoye Matale, Kaa la Moto, Sikonge Eiyer FaizaFoxy
Cc. Nguto, Buntungwa, GEBA2013, Power to the People, Majigo, rodrick alexander, Doppelganger, Makoye Matale, Yericko Nyerere, Daudi Mchambuzi, Sikonge, Eiyer, FaizaFoxy
Wakaamua kuhamia DSM. Alitangulia mwanamume akatafuta nyumba ya kupanga. Wakati huo walikuwa na mtoto mdogo ambaye alifariki baadaye. Mume alimfuata mke wakaja kuishi DSM ambapo walizaa mtoto mmoja aliye sekondari hata sasa.
Mume alipata kazi ya korokoroni aliyokuwa akiendelea nayo hadi mauti ilipomkuta.
Wakiwa DSM walifanikiwa kujenga nyumba huko mbagala ambapo walikuwa wakiishi hadi mauti yalipomfika mume. Kazi ya mwanamke ni mganga wa tiba za asili.
Shida ni kuwa watoto wale wa mama wa kwanza pamoja na shehe (mume alikuwa mwislamu) wanadai kuwa nyumba waliyoijenga ni mali ya watoto pamoja na vitu vingine vyote. Huyu mama wanasema akabidhiwe kwa ndugu zake wao wauze nyumba watoto wagawane pesa. Wanasema huyu mama akaolewe tena huko kwao ilhali kajijengea nyumba na mumewe ili waishi hati mpaka mauti yawafike.
1. Je, sheria ya kiislamu inasemaje juu ya hili? Huyu mama aliyetumia muda na nguvu zake kujijenga na mumewe ni sahihi afukuzwe hapo?
2. Sheria za nchi zikoje katika hili? Mwanamke keshanyang'wa hati za nyumba na watoto, ingawa anao ushahidi tosha kuwa hiyo nyumba kaijenga na mumewe.
3. Leo ndio kuna kikao cha ukoo cha maamuzi, nahitaji msaada wa haraka katika hili.
Belo Daudi Mchambuzi zumbemkuu
[MENTION] Yericko Nyerere[/MENTION] Bujibuji Makoye Matale, Kaa la Moto, Sikonge Eiyer FaizaFoxy
MREJESHO
Wakuu nashukuru sana kwa msaada wenu wa ushauri. Baaada ya jana kufika kwa mjane yafuatayo yalifanyika:
>> Alikuja shehe kusimamia hili zoezi la kugawa mali. Shehe huyu alitumia hekima ya hali ya juu kunusuru mambo.
>> Samani zote za ndani aliachiwa marehemu kwa ushauri wa shehe baada ya baadhi ya ndugu katika kuchukua kila kitu.
>> Mpango wa kuuza nyumba aliukataa shehe akidai maadam mama yupo na mwanae wataendelea kuishi hapo. Kisha akaelekeza kuwa suala la nyumba ni la kisheria, hivyo utayarishwe muhutasari utakaoteua msimamizi wa mirathi kisha upelekwe mahakamani. Taratibu nyingine zitafuata huko.
>> Alisisitiza kuwa anafanya hivyo kwa vile hataki kuanza kuitwa kwenye kesi za unyang'anyi wa mali za mjane. Pia alimuuma sikio mjane kuwa msimamizi wa mirathi ni mjane mwenyewe labda kama ataamua vinginevyo.
>> Wakati haya yakifanyika alifanya mgawanyo wa vyumba kwa watoto wote wa marehemu. Nyumba kubwa ina vyumba vitatu na sebule. Chumba kimoja cha mjane, viwili vya mtoto wa mjane. Nje kuna nyumba ya vyumba vitatu vinavyojitegemea (behewa). Watoto watatu wa marehemu kila mmoja akapewa chumba kimoja wakati shauri la mirathi likisubiriwa.
>> Mjane aliridhia maamuzi haya na hivyo taratibu za matatizo zinasubiriwa. Lengo la shehe ni kuleta mshikamano kati ya mama na watoto. Maamuzi haya yamezua chuki kubwa kwa baadhi ya watoto wa marehemu.
>> Huu mwelekeo mnauonaje wakuu?
Katika tukio jingine mtoto wa mjane (bado ni mwanafunzi) yuko mahututi. Aliugua kichaa ghafla siku ya pili ya msiba. Baada ya dada yake (wa mama mwingine) kufika alimchukua pembeni na kumwambia aache kujidai analia kwa uchungu sana, kisha akampitishia viganja vya mikono yake usoni mithili ya kumfuta machozi. Tangu dakika hiyo binti huyu wa mjane alianza kuchekacheka hovyo na kuongea maneno ya ajabu ajabu. Sijamuona huyu binti kwani wamempeleka kwa sangoma. Nimepanga kwenda kumjulia hali nakuangalia namna nyingine ya kumsaidia
Cc. Nguto, Buntungwa, GEBA2013, Power to the People, Majigo, rodrick alexander, Doppelganger, Makoye Matale, Yericko Nyerere, Daudi Mchambuzi, Sikonge, Eiyer, FaizaFoxy
Last edited by a moderator: