Msaada: Wadudu wamekula mbao za dari, paa linataka kudondoka. Mtaalamu wa dawa anisaidie ushauri

Msaada: Wadudu wamekula mbao za dari, paa linataka kudondoka. Mtaalamu wa dawa anisaidie ushauri

Joined
Oct 11, 2014
Posts
8
Reaction score
3
Wakuu shikamoni,

Paa la nyumba yangu limeliwa vibaya na wadudu ambao siwafahamu, siyo mchwa, wako kama mende weusi wembamba kidogo kwa mende, wanapokuwa kwenye mbao wanakuwa viwavi (caterpilar) wanakula mbao ndani kwa ndani huku wakiacha matundu kama yanavyoonekana kwenye picha.

Wakishakula ndio wanageuka kuwa kama mende. wakila mbao inakuwa kama bua la muhindi yaani ndani ni hollow na linatoa unga wa njano.

Hawa wadudu wanakula mbao nzima na kuiacha kama unga wa njano.

Nimejaribu kupulizia dawa tofauti tofauti nilizokuwa napewa na wauzaji wa maduka ya pembejeo lakini haijasaidia, nimeona nijaribu hapa labda kuna mtu ameshakutana na kesi kama yangu anaweza akanipa uzoefu.

Hawa wadudu wanapokula mbao inalia kama msumeno unakata mbao.


DSC02372.JPG
DSC02368.JPG
 
Engine oil iliyotumika, inaweza kuwa suluhisho kwa tatizo lako, inavyoonesha ulitumia mbao ambazo huwa wanasema ni treated lakini mbao hizo haziwi treated ipasavyo. Cha kufanya chukua oil chafu na brash ya rangi, paka kwenye mbao kama vile unavyopaka rangi hakikisha pia unanyunyiza kwenye matundu, itasaidia sana. Oil chafu hukimbiza hata nyoka!
 
Mkuu tafuta oil chafu na upakae hizo mbao na enjoy life
 
Hizo zilizoliwa sidhani kama zina ufumbuzi zaidi ya kufumua na kuanza upya. Kwenye mbao mpya ndio hizo dizeli and whatever zifanye kazi. Vinginevyo tumia mbao treated. Kama itakuwa nafuu ununue za kawaida halafu ziwekwe dizeli angalia huo uwezekano.
 
Hizo zilizoliwa sidhani kama zina ufumbuzi zaidi ya kufumua na kuanza upya. Kwenye mbao mpya ndio hizo dizeli and whatever zifanye kazi. Vinginevyo tumia mbao treated. Kama itakuwa nafuu ununue za kawaida harafu ziwekwe dizeli angalia huo uwezekano.
Pia nami nakushukuru mkuu.
 
Mmmmh hata mimi ni hayohayo!!! Nashukuru kwa maelezo yenu.
 
Dragnet inatoka marekani...ni ngumu kuipata ajaribu DKO 30 c ipo kwenye hardware ni uhakika
 
Nilipata shida kama yako nikajaribu yote hayo haikusaidia, dawa ni kubadilisha mbao tu na kabla ya kubadilisha pulizia diesel, dragnet au oil. Waweza tumia mbao treated ingawa pia kwenye kutreat wengine huchakachua kuwa makini ila Sao Hill mbao Zhao ziko vizuri sana.
 
mimi ni fundi, ilikuwa rahisi kama ningekuwepo wakati wa kupaka hiyo dizeli, sio kupaka tu. kuna jinsi ya kufanya, mi nilijifunza kwenye kampuni ya wayugoslavia (partizansk put ya morogoro) wanatumia dizeli safi, mbao haichafuki na ina dumu
 
kama kwenu hakuna ghorofa huna haja ya kuwaza sana!! atadondoka toka wapi sasa!!
 
Ni Mbao za aina gani umetumia?kama ni Jamii ya crevilia au Mbao zenye Sukari ni bora kubadili Mbao zote za paa Kabila halijashuka.mimi nafanya kazi za carpentry,nimewahi kukutana na tatizo Kama Hilo almanusra nifunge Kiwanda sababu ilinichukua Mwaka mazima kufanya repair za bidhaa mbalimbali zilizokuwa zikirudishwa na wateja walionunua kwangu kwa kipindi cha miaka mitatu kabla na kukumbwa na tatizo hilo,nilijaribu dawa mbalimbali bila mafanikio mpaka nilipoamua kubadili mbao nilizotumia ndio ilikuwa suluhisho.Tabia ya huyo mdudu ni kwamba anakula mbao mpaka inapoisha ndio mwisho wa maisha yake,na ilivyo ni kama anajitengeneza tokana na mbao kama alivyo mdudu wa kokwa la embe,hivyo suluhu ya uhakika ni kubadili aina ya mbao ulizotumia,pole sana.
 
Back
Top Bottom