Msaada: Wafanyakazi wenzio kukushinikiza uoe ni ishara ya nini?

Msaada: Wafanyakazi wenzio kukushinikiza uoe ni ishara ya nini?

Accumen Mo

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2022
Posts
18,036
Reaction score
39,882
Za mda huu watu wa nguvu? Poleni na kazi !!

Iko ivi Kuna ishu hapa Ina utata Kuna dogo nilikutana nae maeneo fulani hapa dar kwa vile niliishia nae mkoa fulani huko nyuma alikuwa mdogo kwangu nikawa namkubali maana shule alikuwa safi sana, nilikutana nae kama mwezi wa 7 ivi hapa jijini basi tukabadilishana namba....

Sio mdogo kiivyo yuko age ya 25 kama sijakosea au 26 aliniambia chuo kamaliza 2019 ,kwa vile alijiandaa kisaikolojia basi baada ya chuo kuisha tu akarudi home kwao alikaa kama miezi miwili ...sasa akiwa home kwao alipigiwa simu na kampuni aliowahi kufanya field hapa dar kumbuka hapo matokeo hayajatoka kabisa ...Bahati nzuri matokeo yalipotoka alikuwa poa na ile kampuni ilimuhitaji afanye nao kazi walipenda performance ya nyuma na alifanya kama miezi kadhaa cheti alikipata baada ya graduation mwezi wa 12 mwaka huo huo.

Akapata kazi ile taasisi ni ya wazungu wanamlipa pesa nzuri maana ana kiwanja tayar !!! Kwao hawako fair nawatambua anategemeqa yeye ana dada zake wawili wazazi hawnaa kitu nyumba kamalizia kwao mambo hawezi kutuma chini ya laki 3 hata mpaka 4 kwa mwezi constant labda ipande kila mwisho wa mwezi watu wale anasomesha dogo zake wawili..dada zake wameolewa hata elimu hawaga ni mzigo hata huko kweny ndoa zao wanamuomba msaada.

Alishare changamoto ambayo anakutana nayo kazini kwao ni hii ,kwanza alipanda cheo ghafla mwezi wa saba mwaka huu means alishafika miaka 2 kasoro na anaaminiwa kinoma safari hakosi pesa anashika ndefu, Tatizo limekuja kuwa kwamba pale ofisini Kuna wanawake wengi na wamama wameolewa ila amekuwa akipigiwa kelele kwamba aoe kila siku anasema haswa wasichana wamezidi kumfosi Kil siku wanamuuliza "utaoa Lin" mara "wifi yetu hajambo"

Hiki kitendo nikamnyima raha coz anasema wako watu kibao wengine wamezidi umri hajaoa ila anaulizwa yeye kwa sana .Nikamwambia una malengo gani akaniambia "amepanga anyanyue nyumba kwanza na Kuna mradi wa wazazi wake amalize na awape mtaji kama mill 7 waendeleze kupunguza majukumu" ndio aingie kweny mambo ya ndoa

Dogo mambo ya mademu sio kwa sana ni mtu wa kanisani ni msabato status zake kwa sana mistari na quotes za kidini sana sana na Kwa Maisha naona yuko poa hata gari dogo analo la kupigia misele town .

Je Kuna nn juu ya huyu dogo yeya anaona kama anafosiwa na kuingiliwa katika Maisha yake na watu wa ofisini na anasema Kuna mademu makamo yake hawajaolewa ila wanamkazania aoe je Kuna kitu gani katika hilo?
 
Huyo jamaa wako mshauri awe makini Sana maana naona shetani ameanza kumjaribu.

Yeye afuate tu malengo Yake kwanza Kama alivyopanga.Akishayatimiza ndio suala la ndoa litakuja.
Namtakia kila la heri katika juhudi zake za kujijenga.
 
Huyo jamaa wako mshauri awe makini Sana maana naona shetani ameanza kumjaribu.

Yeye afuate tu malengo Yake kwanza Kama alivyopanga.Akishayatimiza ndio suala la ndoa litakuja.
Namtakia kila la heri katika juhudi zake za kujijenga.
Dah dogo ana wenge anaona kama anapangiwa Maisha na hao watu wa kazini kwao
 
Hajielewi huyo, yaani kutaniwa kuwa shemeji sijui wifi ndio unaona changamoto kubwa ya kusimulia watu?
Yaani hiyo ni changamoto kweli? 😂😂
Au unajitungia story kuchangamsha jukwaa
Kaka ni kweli nilimchek kwa simu maana ni dogo ana akili za kitoto bado nilimwambia utani ni lazima ,usikute hao wasichana kwao wanapigwa kelele nao waolewe
 
Atimize malengo yake asije akakimbilia kuoa akajutia aoe akiwa tayari kaamua kwa dhat,kuwa mume na baba sio lelemama kama hayupo tayari aache wenge Hao wanaosema haendi Kuishi nao nyumbamoja itakuwa yeye na mkewe tu
 
Huu uongo mtupu mtu anayekunja take home salary mil 2 hawez kuwaza ujinga Kama huu ulioandika acha kupost pumba dogo
Eti take home ya 2m ni ndefu nmeleta kupewa mawazo ya dogo ,we mhaya mil 2 ni pesa ndefu kwa kweli 😂😂😂nicheke
 
Hilo mbona liko wazi ndugu?

Dogo atakuwa anafanya kazi shirika la kisabato...

Na kama unavyowajua hao ndugu zetu hawapendagi shortcut sana kwenye mambo yao...

Hivyo kwa kuwa wanamuona dogo ana life la kuoa sababu ya uwezo wake, ndiyo maana wanamkazania sana aoe.
 
Back
Top Bottom