mkabidhi duka.
hesabu kila kitu weka na bei halafu muachie ukiwa unajua bei ya kununua na kuuza,idadi ya bidhaa,faida inayopatikana katika kila bidhaa halafu mwambie aendelee kila matumizi anayofanya akuandikie na kila anachouza akiandike utagundua kama unauza kwa hasara au kuna faida imefichwa.
Weye! stocktaking za muda mrefu hivyo? Ukifanya hivyo utakuta tu mavumbi kwenye shelves na hela haionekaniInabidi uwe unafanya stock taking kila baada ya miezi 6. yaani kwa mwaka mara 2.
ila kama unahisi mambo sio sawa jitahidi kuweka msimamizi wa dukani makini.
Weye! stocktaking za muda mrefu hivyo? Ukifanya hivyo utakuta tu mavumbi kwenye shelves na hela haionekani
Habari zenu wana jamvi hasa wajasiriamali wenzangu. Mimi nafanya biashara ya vipodozi pamoja na saloon ya kike lakini kadiri siku zinavyoenda sioni maendeleo na duka lipo sehemu nzuri ya biashara, ninavyoona ni kama niliyemueka pale dukani ananiibia sasa naomba ushauri wenu pia naomba kuelekezwa namna yakupiga mahesabu ya thamani ya vitu vilivyopo ili nijue nina hasara kiasi gani.
Nawasilisha msaada wowote nitashukuru.
Habari zenu wana jamvi hasa wajasiriamali wenzangu. Mimi nafanya biashara ya vipodozi pamoja na saloon ya kike lakini kadiri siku zinavyoenda sioni maendeleo na duka lipo sehemu nzuri ya biashara, ninavyoona ni kama niliyemueka pale dukani ananiibia sasa naomba ushauri wenu pia naomba kuelekezwa namna yakupiga mahesabu ya thamani ya vitu vilivyopo ili nijue nina hasara kiasi gani.
Nawasilisha msaada wowote nitashukuru.
mkuu hebu tuwasiliane nikuonyeshe software ambayo itakurahisishia kazi ya kuweka stock,kujua mauzo ya 8siku,wiki,mwezi,kujua madeni kiasi gani unadai au kudaiwa,malipo yamefanyika lini na nani kafanya malipo,nani kauza na kauza nini na tarehe ngap kwa sh ngapi...kama upo dar tuwasiliane 0714281313,kuonyeshwa ni bure kabisa.
StockPointNinaomba jina LA software
StockPoint
stock and sales management system
Ilishaletwa mada hapa Jf mtu mmoja analalamika kwamba kwa nini mahoteli yetu ya kitalii hayaajiri watanzania ila huajiri wakenya kwa wingi. Mtu mmoja akajibu kwamba watanzania hawaajiriki kwa sababu ni wavivu,na wadokozi.
Kwa udokozi na wizi kwa kweli watanzania ni wataalamu, mpaka jambia la IGP wamelikwapua! Kwa hiyo ndugu yangu wa duka la vipodozi, kama huwezi kukaa huko dukani mwenyewe, basi imekula kwako. Hata umweke ndugu wa damu au sijui nani, atakuchomoa tu!
Mimi binafsi ilinibidi nifunge hoteli yangu baada ya kuandamwa na wizi/ udokozi wa niliowaajiri. Wa kaunta alidokoa hela za mauzo, wa jikoni ndo kabisaa walijichotea mavyakula na kupeleka nyumbani.
Ukimkamata mmoja, anavyopiga magoti na kuomba! Nikaona isiwe shida nikafunga hoteli!
Unatakiwa kila siku jioni pitia fanya stocking na chukua mauzo kabidhi hela ya mahitaji ya kesho au nunua kabisa. Mara moja kwa wiki kaa wewe pia uone siku ktk biashara yako inakuwaje usijekuwa unalaumu bure. Hakuna biashara ya kufanyiwa siku zote lazima nawe uwepo
kama umeajiriwa nakushauri uchukue likizo japo ya mwezi mmoja then kwa kipindi hicho usimamie biashara kwa kuwepo mwenyewe. hapo utajua hali halisi ya biashara yako na utapata akili uchukue hatua zipi baada ya hapo. otherwise jiandae kufilisika, kama ulikopa mkopo jiandae kufilisiwa kwa kuuziwa nyumba. na usishangae wanaokuuzia biashara zako baada ya muda ukawaona wamefungua biashara zao na wamekukimbia!Habari zenu wana jamvi hasa wajasiriamali wenzangu. Mimi nafanya biashara ya vipodozi pamoja na saloon ya kike lakini kadiri siku zinavyoenda sioni maendeleo na duka lipo sehemu nzuri ya biashara, ninavyoona ni kama niliyemueka pale dukani ananiibia sasa naomba ushauri wenu pia naomba kuelekezwa namna yakupiga mahesabu ya thamani ya vitu vilivyopo ili nijue nina hasara kiasi gani.
Nawasilisha msaada wowote nitashukuru.