Msaada: Wanauchumi nitawezaje kusave mshahara wa laki moja na ishirini, ili nami niwe na mafanikio?

Hapo cha kufanya,
Tafuta mchumba kisha mchumbie ili awepo nyumbani awe anakutunzia kibubu chako,

Apo utaona mwenyewe savings zako zinaenda vizuri sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuwa mama ntilie, mimi na wadada wangu wa biashara wote tunakula hapo hapo na faida ipo na msingi upo.
Kwetu pia mama ntilie ndo biashara iliyonilea na kunisomesha na bajeti ya kula wote hapo hapo.
Mimi nakumbuka tunatembea kwa miguu na wanafunzi wenzangu tunawahi kwetu kula ukoko na maharage, aiseee hawasahau mpaka kesho ulivyokuwa mtamu.
Aiingii akilini kula unachouza!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Laki 5 ya robota la mashati utampa kaka?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unatakiwa ufanye maamuzi magumu.
Kama hiyo kazi ya kufundisha ni kazi ya ndoto yako endelea nayo huku unatafuta shule nyingine, lakini muhimu utafute nyumba karibu na eneo la kazi gharama ya nauli uepuke kama shuleni kwenu wanaruhusu biashara ndogondogo tafuta sehemu wanapouza asikirimu kwa jumla chukua zako. Mara nyingi la. Kuwekea anakupa mwenye asikirimu ukichukua piece 100 hukosi 3,000 kwa siku, ukiuza piece mia mbili hukosi 6,000.
Kama kufundisha unafanya tu ili mradi mkono uende kinywani chukua maamuzi magumu yakiume haswa pokea mshahara wako acha kazi.
120,000 inatosha kuingia nayo mtaani kupambana kwa biashara ndogo ndogo funga moyo pambana aiseeee ujiajiri utatoboa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshahara wa 120k:

Tafuta chumba sehemu yakaribu; kama si mbali usafiri wa miguu unatosha sana (30000-natumaini bei itapungua maybe, usiangalie ubora wanyumba wewe sio mtarii bali mtafutaji)

Punguza milo, mlo mmoja unatosha sana na maji yakutosha (mchana) kama si kazi ngumu..2000*30= 60000/=Tsh
inabaki kama 30000/= Tsh
Toa 10000/=Tsh kama kusave

Then 20elfu inayobaki;
maji na umeme(10000/=Tshs)

10000/=Tshs: vocha kwa case maalumu tu,,, 1000/=Ths sms zamwezi kwa haloteli au1500/=Tshs sms mwezi halotel, 1500/Tigo au 2000/sms Vodacom {Maximum 2000) kwa mwezi.

...inabaki kama 8000/=Tshs (kilinda mfuko,pia kama mgonjwa mgonjwa hapa panadol vs dawa yabei rahisi).

NB;kama umeweza pata chumba eneo la karibu nabei pungufu pesa itayobaki utajazia sehemu zamatumizi kama mlo, nauli n.k kwa case yamuhimu na haraka.
 
Huoni kwamba hayo yanaweza kua mazingira rafiki ya kujifilis?
 
Ndugu huo msaada zaidi ungeandika hapa ingekuwa jambo muhimu sana
Sent using Jamii Forums mobile app
 
ku-save hiyo ni ngumu sana mkuu, kwa kipato cha milioni moja kwa mwezi unaweza ku-save angalau elf 50 kibishibishi, na hapo inategemea kama huna ndugu na marafiki wa kupiga mizinga.
Yaani kwa kipato cha 1M unasevu 50K tena kibishi kweli tunatofautiana mimi hapo nasevu 800K tena sio kibishi na hao wazazi nimewasaidia vilevile 800K ndani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Talking from Experience
nilishawai kuishi na 40,000/= kwa muda wa miezi 4...nilikuwa nakula 1200/= kwasiku siku nimefeli 1500/= siku nimefeli zaidi njaa kali 2000/= na udalaliudalali ukini boost.

1200/= ilikuwa simple 1000/= nilikuwa nanunua wali mchana then usiku nakula Scones 2 ambazo nanunua package 1000/= zinakaa 10 So nikila 2 inakuwa sawa nimetumia 200/=

So hapo mlo nilikuwa natumia 1200 kwasiku...Hii sio rahisi wewe unaweza kula Scones ×2 kwasiku asubui na usiku Sawa unatumia 1400/= kwasiku.


1400 × 30 = 42000/=

Kuhusu chumba 30000/= ni kutokuwa na nudhamu na pesa

Panga chumba cha 15000/= kalibu na kituo cha kazi.

42000(meal)+15000(kodi)= 57000/=

3000 ya mambo mengine


TZS 60,000/= SAVING

Ni miezi mitatu unakuwa na 300,000 mtaji

Miezi minne 4 ni 350,000/=

Ila pesa ndogo sana uwezo wangu wa mwisho wa kusevu.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Heshima yako madam!
 
Acha matumizi mabaya katika fedha.
ku-save hiyo ni ngumu sana mkuu, kwa kipato cha milioni moja kwa mwezi unaweza ku-save angalau elf 50 kibishibishi, na hapo inategemea kama huna ndugu na marafiki wa kupiga mizinga.
 
Yaani kwa kipato cha 1M unasevu 50K tena kibishi kweli tunatofautiana mimi hapo nasevu 800K tena sio kibishi na hao wazazi nimewasaidia vilevile 800K ndani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Dah! hiyo laki 2 na sometimes hadi laki 4 ndo nawasaidia wazazi na bado wanadai haiwatoshi, nikiamua kuendesha gari langu kwenda kazini kila siku ni laki 3 hiyo, hapo bado matumizi ya familia ya kila siku. kuna kipindi nilikuwa nalipwa viposho ambavyo ukiunganisha na salary inafika kama ml.4 kwa mwezi ndo nikajifaragua kujenga kakibanda ambako hadi leo kanadai finishing. Inaweza ikawa pesa nyingi kwa maisha ya chini na huna presha ya kusaidia wazazi na hawa ndugu wengine, mara utaambiwa mpwa wako shule zinafunguliwa toa pesa ya ada na matumizi. Nafikiri wazungu walifanikiwa hili swala la extended families, kila mtu anafanya kazi kwa ajili ya familia yake na serikali zao zinatoa social security za kueleweka. Wazee wakipoteza uwezo wa kufanya kazi wanapelekwa kutunzwa kwenye makambi. Ngozi nyeusi ukifanikiwa kidogo hata ka-salary ka 800K kwa mwezi utaandamwa na ndugu waomba misaada hadi utajuta..
 
Mkuu hayo unayoishi sio maisha siku ukisimamishwa kazi tu utaona maisha machungu.

Wazazi wanafunguliwa biashara yao hawasaidiwi cash endapo itatokea ×chache ila ukiwangulia inakupa unafuu.

Gari kuwa nalo si dhambi ila hapo inapokulia nshahala wako ili kulihudumia jitathmini maisha rahisi ukiwa na mikakati.

Mimi ningekuwa na salary hiyo I can't imagine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nawaza tu mkuu:

1. Nunua mahindi debe 1, kasage upate unga dona Tsh. 24,000/=

2. Nunua Kilo 5 mchele Tsh. 10,000/=

3. Mwanza hapo dili na dagaa standard/samaki wadogo, mboga weka Tsh. 30,000

4. Vocha ni vifurushi vya chuo tu weka Tsh. 5,000/=

5. Nauli weka ya kwenda tu Tsh. 15,000/=

Jumla Tsh. 69,000

NB: Haya mahitaji muhimu TU! Kwa sasa, habari ya wanawake na pombe au starehe weka kando kidogo au tafuta mwanamke mmoja.

Muhimu zaidi tafuta Bima rahisi ipo kila kata Tanzania kakate ni kama Tsh. 50,000/= kwa mwaka

Save bank/kwenye simu Tsh. 35,000/= kila mwezi ila baki na pesa ya dharura mkononi.

INAWEZEKANA KABISA UKIAMUA TU



VIIXCCCL GrandLodge,ARUSHA
 
Anachotakiwa kufanya ni kukata shauri tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hilo la line ni kitu practical??
Kwamba kuna mtu kashawah kujaribu??
Maana wasije wakafunga line halaf wakaigawa namba kwa mtu ikawa majanga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…