Msaada wenu: Baba yangu mzazi anataka kunitimua kwenye nyumba ya babu yetu

Afadhali baba yako hiyo hela aliyokusomesa angenunua ng'ombe wengi afuge apate maziwa , kuliko kusomesha ling'ombe limoja ambalo halitoi hata maziwa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Umekuja kumshtak baba huku naenda kumuonesha ili akufukuze kabsa unatudhalilisha sisi wadogo zako hutak kumsikiliza baba
 
Kwa hio wewe unatumika na CCM sio?Nenda kalale Magogoni.
 
pole sana mkuu,,, nakushauri uende kwenye tawi lolote karibu na kwenu walipo makamanda wa green guard waje wamuresti dingi ako,
kazingua sana kudadadadadekiiii zake!
 
Habari hii inasikitisha kwa sababu nyingi sana.

1. Familia inafarakana.

2. Kijana wa miaka 28 anaishi nyumbani na baba yake.

3. Baba wa kijana mwenye miaka 28 naye anaishi nyumba ya baba yake.

4. Kijana wa miaka 28 anataka kula vichwa vya nyumbani ili apate faida.

5. Siasa zinafarakanisha familia.

6. Wahitimu wa vyuo hawana kazi za kueleweka.

7. Mafarakano ya kifamilia yanataka kupelekwa polisi.

8. Kijana wa miaka 28 anapangiwa kutoshiriki siasa, haki yake ya msingi ya kikatiba.

9. Vyama vya siasa vinatumia hela na ukosefu wa ajira kama mtaji wa kisiasa.

10. Umasikini mwanzo mpaka mwisho. Wa akili na mali.
 
Penye ugumu ndipo hapo hapo unatakiwa ukaze .Pambana utafute vyako mzee ajafa unataka kumrithi
 
Kaka achana na siasa kama inakuharibia udugu. Kwanza ccm inakutumia kwa muda huu uchaguzi ukiisha utatupwkama dekio baada ya kupiga deki.
 
Miaka 28 ni mdogo [emoji3][emoji3][emoji3][emoji23]
 
Una miaka 28 na umemaliza chuo kikuu na umekosa kazi alafu unataka kumletea ccm baba yako nyumbani!! Really? Babako anajua kua sababu ya msingi ya wewe kukosa kazi ni ccm. Nyambafu wewe.
 
Maisha haya magumu. Unaanzaje kuchagua kazi? Hata kama unaichukua CCM siyo suala la kugombezana na mtoto kisa kujiingiza kwenye CCM. Watu siku hizi wanatafuta pesa na siyo chama. Popote pale kwenye pesa watu wataenda kufanya kazi. Huyo dingi hajatumia busara kabisa
Niko upande wa baba ako, hivi kweli hufikirii chanzo cha wewe kukosa ajira ni c.c.m? Watu wanapotea, wanakufa na wanatumbuliwa hovyo kila siku huoni? Ungekaa na baba ako vizuri akakueleza sababu kuliko kujimwambafai na degree yako
 
Nenda chato ukaishi kwenye gesti za ccm.
 
Huyo Mzee wako kakuchoka tu likely utakuwa kula kulala hayo mambo ya siasa kaona ndo nitoke vipi!

Toka kapigane wapo wengi tu walioletewa hila na wazee wao na leo wana maisha yao.

Kikubwa ukitusua halafu akaja kujilizaliza mfungie vioo liwe fundisho kwa wazee wengine wasiojielewa.

Mtu upo uzeeni halafu una-entertain mifarakano kwa watakaokulea muda si mrefu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…