Msafara wa uapisho wa Ruto, hakuna kufunga barabara!

Msafara wa uapisho wa Ruto, hakuna kufunga barabara!

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Ninaangalia matangazo LIVE kupitia luninga za Kenya.

Jambo moja ambalo limenishangaza Sana ni kuona msafara wa Rais mteule, William Ruto, ukienda kwenye kiwanja cha Kasarani, ambako ndiyo kunakotarajiwa kwa shughuli hiyo ya uapisho, akipita barabarani bila kuzifunga barabara hizo, kwa maana nyingine ni kuwa, msafara huo umekuwa ukipishana na magari mengine, yalioko kwenye shughuli nyinginezo!

Nimekuwa nikijaribu ku-imagine, kama shughuli hiyo ingekuwa hapa kwetu Tanzania, barabara ambazo angepita huyo Mheshimiwa, barabara zingefungwa kwa masaa kadhaa na kuathiri shughuli mbalimbali za wananchi hao!

Tumeshuhudia kwa safari za kawaida za Mheshimiwa Rais wa nchi hii, barabara huwa zinfungwa hata kwa zaidi masaa 2, akipishwa Mheshimiwa Rais apite yeye tu na hakuna kubughuziwa na waendesha magari yoyote wengine hapa nchini!

Hebu tujiulize, hivi huu ulinzi wote tunaowapa Hawa viongozi wetu hapa TZ, tafsiri yake ni nini hasa?🥺
 
Wenzetu wanaheshimu walipakodi ambao huchangia wese za gari za ikulu.

Hapa nchini Ikulu ina utaratibu wake kana kwamba wanatoa hela mifukoni mwao
 
Kuna baadhi ya nchi(fulanifulani)watu wakipata madaraka na muda huohuo wanaanza kuwa walemavu/wadumavu wa akili.Hata kama walikuta mambo yapo hivyo,kwa nini wao wasione kero kwa jamii na kufanya mabadiliko?
 
Kuna baadhi ya nchi(fulanifulani)watu wakipata madaraka na muda huohuo wanaanza kuwa walemavu/wadumavu wa akili.Hata kama walikuta mambo yapo hivyo,kwa nini wao wasione kero kwa jamii na kufanya mabadiliko?
Tujaribu tu kuwauliza Hawa watawala wetu wa hapa TZ, hivi hawaoni hayo mateso, wanayowapatia hao wananchi wao, kwa kuwagandisha barabarani, kwa masaa kadhaa?🥺
 
Bora asichelewe kufika uwanjani manake akikosa kuapishwa kabla saa nane leo itabidi arudi nyumbani ajaribu tena kesho
 
Back
Top Bottom