Msafara wa Waziri huku Kigoma, ulimgonga mjomba wangu lakini cha ajabu hawakusimama kumuangalia. Hivi ni kweli hii ndo Tanzania tunayoitaka?

Msafara wa Waziri huku Kigoma, ulimgonga mjomba wangu lakini cha ajabu hawakusimama kumuangalia. Hivi ni kweli hii ndo Tanzania tunayoitaka?

Watanzania wenzangu, sina huzuni kwa sababu sipo Kati ya washindi wa stories of change, Ila huzuni hii niliyonayo imeniumiza mno. Jana kulikua na msafara wa waziri huku kigoma, msafara ule najua ni kwa bahati mbaya wakamgonga mjomba angu na akafariki palepale, Cha ajabu Wala hawakusimama kumuangalia. Hivi ni kweli hii ndo Tanzania tunayoitaka miaka 25 ijayo.

Hakika inaumiza Sana, Ila kwa kuwa sio ndugu yako itakua Ni ngumu kutoa Hata pole. Basi naomba wakuu wa jamiiforums Kama mkiona post Yangu, Jambo hili naomba lisifumbiwe macho. Raia wanabaki wajane na mayatima kwa sababu ya Mambo ya ajabu.

Mwezi wa 7 tu nimempoteza mtu sababu ya pf3 na leo napigwa Tena na tukio hili. Hakika inaumiza. Kupitia jamiiforums natumaini wahusika watapata taarifa na kubadili na kuboresha mienendo yao. Asanteni.
CCM ni wanyama sana tuwakatae!
 
Alikua kwenye mishe zake na Alikua anapaki bodaboda kando. Swala sio kwamba kwa Nini wamemgonga. Ila shida Ni Ile utu wa kwamba umesababisha ajali inahitaji uonyeshe ushirikiano wowote Hata wa kumjulia Hali muathiriwa. Unafikiri aliyemgonga aliwaza Nini, Kama sio kusema tu "achana nae" ndo maana wakaendelea na safari zao. Hakika utu umetoweka.
Motorcades zikiwa kwenye msafara usijichanganye utapigwa tairi no compensation at all ndg achana nayo Ila mwende kwa rto Kigoma atakuwa kapewa maelekezo kuhusiana na tukio ili mjue nn Cha kufanya Ila nachojua onyo Kali atapewa marehemu kwa uzembe
 
Ndugu pole kwa msiba lakini kwa nijuavyo mimi miongoni mwa vitu unapaswa kuwa navyo makini ni misafara ya viongozi wakuu wa Kitaifa!
 
Tusha ambiwa kifo ni kifoo tu ata ufungwe jiwe urushiwe kwenye maji ili mradi ufe tu
 
Back
Top Bottom