Msajili wa vyama vya Siasa unasubiri nini kuifutia usajili CHADEMA wakati inaendelea kukiuka sheria na kuchochea chuki na ubaguzi?

Msajili wa vyama vya Siasa unasubiri nini kuifutia usajili CHADEMA wakati inaendelea kukiuka sheria na kuchochea chuki na ubaguzi?

CHADEMA wanahamasisha na kuchochea ubaguzi kati ya wananchi wa Zanzibar na Bara,wanasema wazanzibari hawana haki huku Bara,wanasema hawastahili kushika uongozi ikiwepo Urais ,wanataka na kudhamiria na kutaka kuhamasisha kuuvunja muungano.
Je mtanganyika wa bara anaruhusiwa kuwa hata balozi wa nyumba kumi huko zanzibar? Tuonyeshe kiongozi mmoja tu huko zanzibar ambaye ni mtanganyika, huu ujinga sijui utawatoka lini.
 
Sijajua kama ni ubaguzi kusema Fulani ni mzanzibar.

Nchi hii ina watanzania na Wazanzibar na Tunakatiba ya Tanzania na ya Zanzibar.

Hivyo kuna watanzania na kuna Wazanzibar kwamujibu wa katiba ya nchi ya Zanzibar. Nl katiba ya Zanzibar Sura ya 1(1) inaeleza kuwa Zanzibar ni moja ya nchi zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ikiwa Zanzibar ni nchi maana yake ina raia wake kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar na raia wake wanaitwa Wazanzibar. Mpaka hapa swali linakuja Je ni katiba ya ZanzIbar yenye ubaguzi au ni raia wa Tanganyika wanapoamua kuifuata na kuitumia kwenye mazungumzo wanakua na ubaguzi.

Nadhani shida ni Aina ya muungano na kero za muungano ambazo utatuzi wake bado mpaka sasa. Tuungane iwe nchi moja yenye serikali moja au serikali tatu ili kusiwe na ubaguzi.

Tatizo linahitaji utatuzi sio watu wakilizungumzia kwa uwazi ionekane ni wabaguzi. Kwanini kuwe na serikali ya Zanzibar ikiwa sisi ni wamoja na hatubaguani?

Ukiuliza mambo ya Tanganyika kwa sasa yasiyo ya muungano yanasimamiwa na Kiongozi gani?? Unaweza kuchanganyikiwa na usijue kabisaa.
 
Sijajua kama ni ubaguzi kusema Fulani ni mzanzibar.

Nchi hii ina watanzania na Wazanzibar na Tunakatiba ya Tanzania na ya Zanzibar.

Hivyo kuna watanzania na kuna Wazanzibar kwamujibu wa katiba ya nchi ya Zanzibar. Nl katiba ya Zanzibar Sura ya 1(1) inaeleza kuwa Zanzibar ni moja ya nchi zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ikiwa Zanzibar ni nchi maana yake ina raia wake kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar na raia wake wanaitwa Wazanzibar. Mpaka hapa swali linakuja Je ni katiba ya ZanzIbar yenye ubaguzi au ni raia wa Tanganyika wanapoamua kuifuata na kuitumia kwenye mazungumzo wanakua na ubaguzi.

Nadhani shida ni Aina ya muungano na kero za muungano ambazo utatuzi wake bado mpaka sasa. Tuungane iwe nchi moja yenye serikali moja au serikali tatu ili kusiwe na ubaguzi.

Tatizo linahitaji utatuzi sio watu wakilizungumzia kwa uwazi ionekane ni wabaguzi. Kwanini kuwe na serikali ya Zanzibar ikiwa sisi ni wamoja na hatubaguani?

Ukiuliza mambo ya Tanganyika kwa sasa yasiyo ya muungano yanasimamiwa na Kiongozi gani?? Unaweza kuchanganyikiwa na usijue kabisaa.
Jaribu kujielisha kufahamu muundo wa muungano wetu ulivyo na sababu ya kuwa hivyo.
 
Kuwaza kufuta CHADEMA ni upeo mfupi wa kufikiri, huwezi kuwa Greet thinker usijue ukubwa wa kazi zilizofanywa na Chadema kuibua mambo nchi hii, nachelea kusema
'Ushabiki' ni neno sawa na 'uhuni'
Kuchochea ubaguzi ndio kazi kubwa? Kupandikiza chuki ndio kazi kubwa.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nauliza kwa uchungu mkubwa sana kuwa ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ipo wapi? Inafanya kazi gani? Imelala wapi huko usingizi wa pono mpaka inashindwa kuona hatari kubwa inayoletwa na CHADEMA hapa nchini? Msajili unaendeleaje kupokea mshahara ambao ni kodi zetu watanzania wakati unatuweka hatarini watanzania na amani ya Taifa letu?

Sheria ya vyama vya siasa inakataza na kupiga marufuku kabisa kwa chama chochote cha siasa kufanya siasa zenye kuchochea ubaguzi kwa misingi ya Udini, ukabila na hata ukanda.sheria inakataza pia kwa chama cha siasa kunadi sera zinazohamasisha au zenye lengo la kuvunja muungano wetu au zenye lengo za kufanya siasa za upande mmoja tu wa muungano.

Lakini leo hii tunashuhudia CHADEMA kupitia viongozi wake wakichochea chuki kali sana na kupandikiza uasi wa kuuvunja muungano wetu pamoja na kuchochea ukanda pasipo kuchukuliwa hatua za aina yoyote ile.ni hatari sana hii inayokuja kwa Taifa letu ikiwa hali hii ya kupandikiza mbegu za ubaguzi itaachwa iendelee kuhubiliwa na kuenezwa na CHADEMA.hii siyo siasa tuliyoitaka watanzania.hatukutaka siasa za kuja kutugawa watanzania na kulipasua Taifa letu.

Tulihitaji siasa za hoja,siasa za sera mbadala, siasa za fikira na mawazo mbadala juu ya ujenzi wa Taifa letu,siasa za hoja ya namna bora ya kulipeleka mbele Taifa letu .Siasa za mawazo mapya ya namna bora ya kutumia rasilimali zetu kwa usahihi katika kuinua uchumi wa Taifa letu na kuboresha maisha ya watanzania wote pamoja na usambazaji wa huduma za kijamii pamoja na kupunguza utegemezi.

Lakini inaogopesha na kutisha sana tunapoona CHADEMA imebadili majukwaa ya kisiasa kuwa uwanja wa kuwasha moto wa kuchochea machafuko kwa Taifa letu.chadema wameishiwa hoja za kuwashawishi watanzania na sasa wameamua waanze kupandikiza mbegu za ubaguzi na chuki kwenye mioyo ya watanzania. Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana ,ni sawa na kula nyama ya mtu ambapo huwezi ukaacha ukishakula nyama hiyo.

leo CHADEMA wameanza kupandikiza mbegu ya ubaguzi ,jinsia , ukanda na mengine mengi.hawataishia hapo bali wataenda mbele zaidi kuanza ubaguzi wa mkoa na mkoa kwa kusema mkoa huu unachangia mapato makubwa sana na hivyo ujitenge na kupewa hadhi ya aina yake.

Msajili wa vyama vya siasa amka ofisini haraka sana uchukue hatua kali sana kabla nchi haijaingia katika matatizo ambayo yatalisambaratisha na kuligawa Taifa vipande vipande. Tumia sheria kuwaadhibu CHADEMA kwa kuwa tayari wameshavunja sheria zote za usajili wao .na sasa wanastahili kufutiwa usajili. Mambo yanaanzaga hivi hivi mpaka mwisho inakuwa donda ndugu litakalolitesa Taifa lote..

Kazi iendelee,Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa,.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Luca,lazima una homa ya bonde la ufa/the rift valley fever.Yule mwana CCM aliyediriki kuuambia umma wakiwapoteza wakinzani wasiwatafute ulimchukuliaje?Kwa nini msajili asianze na hicho chama cha aliyetamka hayo?
 
Luca,lazima una homa ya bonde la ufa/the rift valley fever.Yule mwana CCM aliyediriki kuuambia umma wakiwapoteza wakinzani wasiwatafute ulimchukuliaje?Kwa nini msajili asianze na hicho chama cha aliyetamka hayo?
Alishakemewa na kulaaniwa kwa kauli yake. Je ni wapi CHADEMA wamelaani kauli za viongozi wao kutoa maneno ya kibaguzi hadharani?
 
Wewe umepata chuki gani? unapigana na Katiba? Samia hatoki Zanzibar ni uongo? Zanzibar haina Rais wake? Kwanini Arusha, Dodoma au Morogoro haina Rais wake?
Dogo ungetulia tu uache wenye akili timamu ndio wajadili hoja hii maana wewe akili yako haiwezi ikaelewa
 
Dogo ungetulia tu uache wenye akili timamu ndio wajadili hoja hii maana wewe akili yako haiwezi ikaelewa
Amekueleza ukweli. Unamzungumziaje yule mbunge anayewakilisha watu kumi na tatu kutoka Zanzibar aliyesema watu wa Tanganyika wakitaka kwenda Zanzibar wawe na pasipoti?
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nauliza kwa uchungu mkubwa sana kuwa ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ipo wapi? Inafanya kazi gani? Imelala wapi huko usingizi wa pono mpaka inashindwa kuona hatari kubwa inayoletwa na CHADEMA hapa nchini? Msajili unaendeleaje kupokea mshahara ambao ni kodi zetu watanzania wakati unatuweka hatarini watanzania na amani ya Taifa letu?

Sheria ya vyama vya siasa inakataza na kupiga marufuku kabisa kwa chama chochote cha siasa kufanya siasa zenye kuchochea ubaguzi kwa misingi ya Udini, ukabila na hata ukanda.sheria inakataza pia kwa chama cha siasa kunadi sera zinazohamasisha au zenye lengo la kuvunja muungano wetu au zenye lengo za kufanya siasa za upande mmoja tu wa muungano.

Lakini leo hii tunashuhudia CHADEMA kupitia viongozi wake wakichochea chuki kali sana na kupandikiza uasi wa kuuvunja muungano wetu pamoja na kuchochea ukanda pasipo kuchukuliwa hatua za aina yoyote ile.ni hatari sana hii inayokuja kwa Taifa letu ikiwa hali hii ya kupandikiza mbegu za ubaguzi itaachwa iendelee kuhubiliwa na kuenezwa na CHADEMA.hii siyo siasa tuliyoitaka watanzania.hatukutaka siasa za kuja kutugawa watanzania na kulipasua Taifa letu.

Tulihitaji siasa za hoja,siasa za sera mbadala, siasa za fikira na mawazo mbadala juu ya ujenzi wa Taifa letu,siasa za hoja ya namna bora ya kulipeleka mbele Taifa letu .Siasa za mawazo mapya ya namna bora ya kutumia rasilimali zetu kwa usahihi katika kuinua uchumi wa Taifa letu na kuboresha maisha ya watanzania wote pamoja na usambazaji wa huduma za kijamii pamoja na kupunguza utegemezi.

Lakini inaogopesha na kutisha sana tunapoona CHADEMA imebadili majukwaa ya kisiasa kuwa uwanja wa kuwasha moto wa kuchochea machafuko kwa Taifa letu.chadema wameishiwa hoja za kuwashawishi watanzania na sasa wameamua waanze kupandikiza mbegu za ubaguzi na chuki kwenye mioyo ya watanzania. Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana ,ni sawa na kula nyama ya mtu ambapo huwezi ukaacha ukishakula nyama hiyo.

leo CHADEMA wameanza kupandikiza mbegu ya ubaguzi ,jinsia , ukanda na mengine mengi.hawataishia hapo bali wataenda mbele zaidi kuanza ubaguzi wa mkoa na mkoa kwa kusema mkoa huu unachangia mapato makubwa sana na hivyo ujitenge na kupewa hadhi ya aina yake.

Msajili wa vyama vya siasa amka ofisini haraka sana uchukue hatua kali sana kabla nchi haijaingia katika matatizo ambayo yatalisambaratisha na kuligawa Taifa vipande vipande. Tumia sheria kuwaadhibu CHADEMA kwa kuwa tayari wameshavunja sheria zote za usajili wao .na sasa wanastahili kufutiwa usajili. Mambo yanaanzaga hivi hivi mpaka mwisho inakuwa donda ndugu litakalolitesa Taifa lote..

Kazi iendelee,Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa,.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Mama na baba wa hayo ni CCM
Chama changu kimeasisi kila aina ya uovu. Na hata wewe ni sehemu ya disgrace ya nchi.

Kwanini Msajili asikifute?
 
Amekueleza ukweli. Unamzungumziaje yule mbunge anayewakilisha watu kumi na tatu kutoka Zanzibar aliyesema watu wa Tanganyika wakitaka kwenda Zanzibar wawe na pasipoti?
Alishakemewa na kupingwa hoja yake hadharani tofauti na hao nyumbu wa CHADEMA ambao wanaunga mkono ujinga wao.
 
Back
Top Bottom