Msamaha kubutuliwa, Ndugai aungwe mkono

Msamaha kubutuliwa, Ndugai aungwe mkono

Ndugai ana wakati mgumu sana;
-Wananchi hawawezi kumsamehe kwa jinsi alivolifanya BUNGE
-Raisi hawezi kumsamehe kwa kumzodoa kuhusu MIKOPO
-Mungu hawezi kumsamehe Maana alimsingizia Mwanae(Yesu) kuwa alikua na Mke
- Watu wa Ikungi hawatamsamehe, alimyima Tundu Lissu mshahara, matibabu na kumfukuza ubunge
~Hana pa kutokea amebakiza kwa Shetani tu

Pamoja na yote imeandikwa - dhambi hata kama ni nyekundu kama bendera zitakuwa nyeupe kama theluji.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Kuomba msamaha bila kujua kosa lake ndio kosa alilofanya Ndugai, mwenyewe anasema alitoa maoni yake kwa nia njema, matokeo yake kumuomba kwake msamaha mjinga ndio malipo yake ameyavuna leo.

Mjinga siku zote huwa haombwi msamaha, kwani kwa kufanya hivyo atazidi kuwa mjinga kwa kuamini ujinga wake ni maarifa, na atazidi kuwadharau waliomzidi maarifa matokeo yake atazidi kuwatumbukiza shimoni anaowaongoza kwa ujinga wake.

Naungana nawe mleta mada kwenye kutumia issues zinazoleta mpasuko upande wa pili zenye tija kwa jamii, kujidai special tunaoweza kujifanyia kila kitu peke yetu ni kuzidi kujichimbia kaburi letu, let brave mind play some tricky games, hakuna siasa isiyounganisha hitaji la makundi tofauti.
 
Kutotambua katika siasa kuna agenda za kudumu si marafiki wala maadui kwa hapa kwetu kuna tuangusha.

Kwa hakika la Ndugai na Polepole linaanguka kwenye agenda za muda mrefu za upinzani.

Palitakiwa mipango mikakati ya kucheza na mipira "lose" kama hii.

Timu ya mpira inataka mabao siyo kuwa yamepatikana je.

Hizo ajenda zote wapinzani tunaweza kuzisimamia bila kutegemea mshikamano wowote na hao wachumia tumbo. Hatuko tayari kuungana na wahuni, kisa ajenda zetu kwa bahati mbaya na wao wameziangukia. Hao wahuni wapambane na hali zao, lakini sisi sio wa kuwapa ahueni kwenye vita yao ya madaraka.
 
Ndugai kama binadamu alitoa mawazo yake kwa mtazamo wake. Hata hivyo bila shaka nje ya alichokiamini, kwa nia njema alilazimika kuomba msamaha.

Pamoja na kuomba msamaha kwa nia ya kuwaridhisha wakubwa kinyume cha utaratibu kumbe vita ndiyo bado asubuhi.

Alitoa mawazo yake pia Polepole kwa wakati wake. Huyu kaishia kuwekwa kufuli baada ya kujaribu kukomaa:

View attachment 2068711

Mtu mzima hatishiwi nyau!

Ndugu waungwana wenye kuzielewa hoja za bwana Ndugai - Aluta Continua.

"Bungeni kuna kura ya kukosa imani na mtaani kuna tuojisikia kuzibwa midomo."

Vyama vya siasa agenda zenu kuhusu uhuru wa maoni zinasema je? Kwani nyie mko na uadui wa kudumu na watu? Misahafu si inasema adui yako mpende?

Haipo namna ya kuchachandua uwezekano wa kupatikana katiba tofauti hapa yenye kutufaa sote?

Au kwetu ushabiki ndiyo dili na kila apambanae ni mchuma janga tu kwa wakati wake?

"Ndugai vs uliojichimbia zaidi ngoma bado mbichi."

Tanzania bora zaidi yaweza kuzaliwa hapa!
Chadema watakuwa wajinga wakirudia makosa waliyofanya kwa Lowassa, Sumaye na Nyalandu.
 
vyovyote iwavyo, kukopa trillion 10 ndani ya miezi 9 kwa ajili ya madawati hatuwezi kukubali, hili lazima liondoke na mtu!
Poleni sana, leo ndio ameamua kuwapa za uso sukuma gang!!hayo mamiradi lukuki yaliyoanzishwa kwa kukurupuka pesa zake za kuyaendeleza ujenzi zinatoka wapi?eti trilioni 10 kwa madawati!!huyo shujaa wenu aliyekuwa anasema hakopi , ila daa mungu fundi sana, kwani ametuepushia mengi!!
Leo sasa ndio ametangaza vita ni vita mula, kama mlimtuma Ndugai ujumbe mmeupata.
 
Ndugai kama binadamu alitoa mawazo yake kwa mtazamo wake. Hata hivyo bila shaka nje ya alichokiamini, kwa nia njema alilazimika kuomba msamaha.

Pamoja na kuomba msamaha kwa nia ya kuwaridhisha wakubwa kinyume cha utaratibu kumbe vita ndiyo bado asubuhi.

Alitoa mawazo yake pia Polepole kwa wakati wake. Huyu kaishia kuwekwa kufuli baada ya kujaribu kukomaa:

View attachment 2068711

Mtu mzima hatishiwi nyau!

Ndugu waungwana wenye kuzielewa hoja za bwana Ndugai - Aluta Continua.

"Bungeni kuna kura ya kukosa imani na mtaani kuna tuojisikia kuzibwa midomo."

Vyama vya siasa agenda zenu kuhusu uhuru wa maoni zinasema je? Kwani nyie mko na uadui wa kudumu na watu? Misahafu si inasema adui yako mpende?

Haipo namna ya kuchachandua uwezekano wa kupatikana katiba tofauti hapa yenye kutufaa sote?

Au kwetu ushabiki ndiyo dili na kila apambanae ni mchuma janga tu kwa wakati wake?

"Ndugai vs uliojichimbia zaidi ngoma bado mbichi."

Tanzania bora zaidi yaweza kuzaliwa hapa!
Mwacheni kila mtu apambane na hali yake mwenyewe.
 
Kwa kauli zile za Mama, hata huo msamaha wa JN inaonekana amefanya kwa shinikizo baada ya kutonywa kwa yajayo. Lazima kuna mtu kavujisha siri ili amuokoe Mzee wa Galilaya. Wakaona kuomba radhi hadharani inaweza kunusuru.
Ila Mama anaenda kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye na ndiyo utakuwa mwisho wake na wanaweza kumshitaki akafungwa.
 
Kuomba msamaha bila kujua kosa lake ndio kosa alilofanya Ndugai, mwenyewe anasema alitoa maoni yake kwa nia njema, matokeo yake kumuomba kwake msamaha mjinga ndio malipo yake ameyavuna leo.

Mjinga siku zote huwa haombwi msamaha kwani kwa kufanya hivyo atazidi kuwa mjinga kwa kuamini ujinga wake ni maarifa, na atazidi kuwadharau waliomzidi maarifa matokeo yake atazidi kuwatumbukiza shimoni anaowaongoza.

Chimbuko la kufikia kuomba msamaha yawezekana kuwa kaingizwa chaka, pengine na washirika wake hasa hasa baada ya kuendelea kuzodolewa na kukosa waungaji mkono wa hadharani.

Kama uzi huu unavyolenga kwa hakika "lose ball" hii ilipaswa kuchukuliwa kimkakati tangia ilipoanza kuzagaa zagaa bila mwenyewe kwenye lango la adui.

Kwa hakika tunapaswa kutambua ushindi ni magoli na adui si wa kudumu, ila agenda.

Tupigane "total football" na aina zote za silaha akili vichwani.
 
Chadema watakuwa wajinga wakirudia makosa waliyofanya kwa Lowassa, Sumaye na Nyalandu.

Makosa yapi yaliyofanywa kwa hao. Walikuja wakafanya sehemu yao. Walipoona nyimbo za sayuni haziimbiki wakaondoka. Shida iko wapi?

Slaa alipoona hakuimbiki aliondoka kama domokaya wa kule nanihii tu.

Hakuna rafiki wala adui wa kudumu. Ni lazima ku perfect kwenye hilo.
 
Hizo ajenda zote wapinzani tunaweza kuzisimamia bila kutegemea mshikamano wowote na hao wachumia tumbo. Hatuko tayari kuungana na wahuni, kisa ajenda zetu kwa bahati mbaya na wao wameziangukia. Hao wahuni wapambane na hali zao, lakini sisi sio wa kuwapa ahueni kwenye vita yao ya madaraka.

Siasa ni science mjomba. Siasa ni mikakati ikibidi hata infiltration kwa adui ni sehemu ya mchezo.

Hatuna ya kujifunza hata Kenya tu?

Bila kuufahamu mchezo huu kikamilifu, matokeo ya kupata wiki ijayo tunaweza yapata baada ya miaka 10.

Kwani ujinga utakuwa ni nini basi?
 
Ila Mama anaenda kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye na ndiyo utakuwa mwisho wake na wanaweza kumshitaki akafungwa.
Hahaaaa!!!hilo haliwezekani kamwe kwa siasa za kiafrika!!kwanza kwa michambo hiyo wote walio nyuma ya Ndugai wamesha kula kona!!na leo sasa ndio ametangaza kiama baina yake na sukuma gang!!ila Mungu anatisha kweli Ndugai wa mwaka mmoja tu uliopita alivyokuwa anawafanyia wenzake leo ni ya kumkuta haya?!!
 
Back
Top Bottom