ata-hit af kweli bora amchukue huyo singo gelo
ka kwangu...wataka tuunganishe undugu???Hivi hako katoto kamalaika hapo ni ka kwako? Au una undugu nako Evelyn Salt?
ka kwangu...wataka tuunganishe undugu???
Muziki ni biashara huria sasa kua na bidhaa bora hakukupi guarantee Ya kufanya vizur moja kwa moja.
Lazma ufanye jitahda na maarifa ya kushawish wateja ubora wake ili pale watapoipata inakua rahs kuikubali na kukupa faida wewe.
Belle 9 kafeli hapa... anatoa mzki mzur lakn anakosa nguvu ya ushawish juu ya mzk wake..HITIMISHO:USIMAMIZI MBOVU
Hapa naona ni management!
Muda mwingine nafikiria kama amejitenga sana..na hafanyi juhudi binafsi kujipromote..
Mkuu katika hili ntakupinga kidogo..mimi sifikiri kama clouds wanapaswa kupewa lawama au media yeyote kwa kuwa wao wanawapa walaji wanacho kitaka!
Kwa hiyo unataka kusema Clouds hawapigi nyimbo yake? Clouds wataipaje nyimbo air time ambayo haichaguliwi na walaji? Mbona kuna radio nyingi bongo na hata huko air time hazipewi vyakutosha?
Huyu si ndio kamtoa Masogange ? basi ana nyota ya Punda ya kung'arisha wengine.
Ila labda kazi zake zinakuwa nyepesi sana...au hajishughulishi vya kutosha baada ya kutoa kazi...akishatoa ngoma anajifungia ndani na kubaki anasubiria zali.
Mkuu kuna ukweli katika hili kataa ukubali
Mziki wa Tz unashikiliwa na watu walijijengea mtandao fulani yaani bila wao utaishi patupu
Clouds ni wamojawapo wa hao madon wa Muziki tz
Belle9 alipoteza vibaya tu alipogombana na Cloud, kumbuka clouds inashirikiana na wanamtandao wanaoshirikiana kuendesha muziki wa bongo kwa maslahi yao
Sio belle9 tu, Juma nature yupo wapi? Unadhani akina temba ni wakali kuliko akina Juma neture?
Muziki wa bongo unafitna kubwa sana kuliko unavyodhaniwa wote wanaopotea wakati ni wakali wengi wao ni wale wanaopingana na mfumo huu gandamizi
Mfano Ay, Fa dimpoz chibu na wasanii wote wakali nk wakitoa ngoma lazima wawalipe fela na babutale eti ndio wasambazaji wa kazi kwenye media, jifanye kichwa ngumu sasa na upeleke mwenyewe uone kama zitapigwa hata mashabiki waombe marangapi,,,,,,, hazitapewa airtime ya kutosha
Prof Jay alitoa ngoma kali sana mbili kwa mpigo mwaka jana na tena alimshirikisha Chibu lakini kwasababu tu alikua upande wa Jide matokeo sote tunayajua
Mtu kama Tid mnyama na ujanja wake wote aliwaletea Clouds ujinga wakambania miezi kadhaa tu alirudi mbio kuwaomba msamaha na kwa jeuri wakamwambia ulitutukana habari maelezo rudi huko huko ukaonbee msamaha huko, na alirudi kweli
Tatizo hapa ni media zingine kushindwa kutumia fursa na kuwaacha clouds kumiliki wadau wote wa muziki kuanzia wadhamini hadi maboss wanaotoa shows na matangazo
Sasa kama nyimbo yako kali lakini haipigwi vyakutosha na haupati shows wala matangazo unategemea nini
Sikuhizi media zinalazimisha hata kama wimbo wa kawaida uonekane mzuri, utatangazwa utadhani nini na muhusika atapata shows na endorsements za kutosha iwapo tu atakubaliana na washika dau
Mimi naona ni makosa kudhani sisi watz ndio tunawaangusha wasanii bali ni mfumo fulani ambao wasanii wenyewe wanatakiwa wajitoe muhanga kupambambanao na sio sisi wlaji maana hatuna redio station wala hatundai shows
Wana jamvi wasalaam...
Wana jamvi katika adhabu ambayo anaweza kupewa mtu na ikamuumiza sana na akashindwa kujua la kufanya au suluhu ni adhabu ya kupuuzwa.
Adhabu ya kupuuzwa ndio aliyo pewa msanii Bell 9 na watanzania walio wadau wa muziki!
Bell 9 ni mmoja wa wasanii wenye sauti nzuri,mtunzi mzuri na mwimbaji mzuri lakini hakuwai kufurahia matunda ya kipaji chake kama wengine!
Bell 9 pamoja nakujua hayo yote na baadhi ya watanzania kusifu nyimbo zake lakini zimekuwa zikikosa muda wa hewani wa kutosha kama nyimbo nyingine na ni vigumu nyimbo kupata muda wa hewani kwenye radio station na Tv kama walaji hawauchagui wimbo husika!
Watanzania, Bell 9 amewakosea nini? Kwanini mna mpuuza kiasi hiki? Pamoja na msanii huyu kutoa wimbo mpya hivi karibuni lakini kwa utafiti nilio ufanya mapokeo yake ni madogo na ya kukatisha tamaa pamoja na wimbo husika kuwa mzuri sana.
Msanii Bell 9 anakosea wapi?
Aina ya studio anayo record?
Aina ya management aliyo nayo?
Aina ya utunzi anao utumia au nyimbo anazo imba?
Amejiweka mbali na mashabiki?
Kwakuwa hana kick au scandal?
Nimejiuliza maswali mengi lakini nimekosa majibu kabisa juu ya msanii huyu Bell 9 na huwa namuonea huruma pamoja na kuonesha juhudi lakini ana puuzwa sana ....hakika kwa jinsi anavyo puuzwa huyu msanii ningekuwa ndugu yake ninge mshauri atafute shughuli nyingine ya kufanya.
Kuna nyimbo zinapata air time ya kutosha hadi una shangaa huyu Bell 9 ana shida gani?
Msanii Bell 9 amewakosea nini watanzania? ni wapi ana kosea?
Karibuni wana jamvi.
Belle 9 kama matonya tu wanaimba vizuri ila ndo hivo...hadi nimehisi kuwaonea huruma