Msanii Ditto afungua kesi ya Madai ya Tsh. Bilioni 6 dhidi ya Multi Choice (DSTV)

Msanii Ditto afungua kesi ya Madai ya Tsh. Bilioni 6 dhidi ya Multi Choice (DSTV)

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1700765387319.png

Mwanamuziki, Lameck Ditto amewasilisha vielelezo tisa wakati akitoa ushahidi katika kesi ya madai dhidi kampuni ya Multichoice Tanzania Limited, akiituhumu kutumia wimbo wake bila ridhaa yake katika kipindi cha kampeni ya Afcon 2019.

Ditto ambaye jina lake halisi ni Dotto Bernard Bwakeya ameiomba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam iamuru kampuni hiyo imlipe fidia ya Sh6 bilioni kwa kutumia wimbo wa 'Nchi Yangu' aliodai ni wake kwenye matangazo yao ya biashara bila ridhaa yake.

Pia ameiomba Mahakama iamuru alipwe Sh200 milioni kutokana na madhara ya jumla, lakini pia alipwe riba ya asilimia 25 tangu siku alipofungua shauri hilo.

Akizungumza na wanahabari mara baada ya shauri hilo, Wakili wa Ditto, Elizabeth Mlemeta amesema kesi hiyo imeanza kusikilizwa na upande wa mdai una mashahidi watano.

Pia, Soma=> Lameck Ditto achemka madai ya bilioni 6 dhidi ya DStv, Mahakama yasema ilitumika 'second version' na si 'original' yake
 
Kiutani utani anaweza kuambulia hata Bilioni 1

Mwan a Fa na Ay waliwahi kuwashtaki Tigo kutumia nyimbo zao kwenye miito ya kupiga simu, Tigo waliwalipa bilioni 2.15 lakini kiuhalisia huenda walibaki na bilioni 1.5 (kila moja milioni 750), Huenda walimlipa mwanasheria wao Albert Msando milioni 150 na wazee wazito wakapiga mchinjo wa milioni 500.

Ay naskia aliwekeza kwenye biashara ila kwa Fa itakuwa alitia hata milioni 200 kwajili ya kampeni za ubunge, kuwatuliza wajumbe, n.k
 
Naitwa Dittooo ooohh naitwa Dittooo ohhh🎶
Kutoka bongo records🎶
Dunia ina mambo toka kitamboo🎶
Dunia hii imejaa chuki na masimangoo🎶
Oona sasa brazamen chupuchupu apewe kisagoo🎶
Kakopa nguo kwenye malipo kageuka mbogoo🎶


Ditto alikua anaflow kinoma enzi hizo kwenye dunia ina mamboo na afande sele
 
Naitwa Dittooo ooohh naitwa Dittooo ohhh🎶
Kutoka bongo records🎶
Dunia ina mambo toka kitamboo🎶
Dunia hii imejaa chuki na masimangoo🎶
Oona sasa brazamen chupuchupu apewe kisagoo🎶
Kakopa nguo kwenye malipo kageuka mbogoo🎶


Ditto alikua anaflow kinoma enzi hizo kwenye dunia ina mamboo na afande sele
Wanamuita dogo na kweli ni mdogo ila cha ajabu anatembea na vigogo.
 
Kiutani utani anaweza kuambulia hata Bilioni 1

Mwan a Fa na Ay waliwahi kuwashtaki Tigo kuweza nyimbo zao kwenye miito ya kupiga simu, Tigo waliwalipa bilioni 2.15, nahisi wao kila moja alichukua bilioni 1 na hio milioni 150 wakalipa wanasheria na gharama zingine.

Ay naskia aliwekeza kwenye biashara ila kwa Fa itakuwa alitia hata milioni 200 kwajili ya kampeni za ubunge, kuwatuliza wajumbe, n.k
Ile kesi ya akina AY gharama zake na mgawo kwa wanasheria haikuwa 150M pekee. Hao kina AY walishikwa sikio na kuna watu nyuma walisaidia tena wengine within, mchinjo waliokatwa unaweza vuka hata 500M.
 
Ile kesi ya akina AY gharama zake na mgawo kwa wanasheria haikuwa 150M pekee. Hao kina AY walishikwa sikio na kuna watu nyuma walisaidia tena wengine within, mchinjo waliokatwa unaweza vuka hata 500M.
Ok lets say mchinjo ulikuwa ni 650 M

2.15 Bilion - 650 Milioni = 1.5 B

Kama waligawana KIasi hicho pasu kwa pasu ni milioni 750 kila moja, Ni pesa sana kwa msanii wa Tanzania,
 
Ile kesi ya akina AY gharama zake na mgawo kwa wanasheria haikuwa 150M pekee. Hao kina AY walishikwa sikio na kuna watu nyuma walisaidia tena wengine within, mchinjo waliokatwa unaweza vuka hata 500M.

Inasemekana bilioni 1 walichukua wadau waliofanilisha dili. Na bilioni 1.1 wakapewa mwana Fa na Ay wagawane
 
Kiutani utani anaweza kuambulia hata Bilioni 1

Mwan a Fa na Ay waliwahi kuwashtaki Tigo kuweza nyimbo zao kwenye miito ya kupiga simu, Tigo waliwalipa bilioni 2.15, nahisi wao kila moja alichukua bilioni 1 na hio milioni 150 wakalipa wanasheria na gharama zingine.

Ay naskia aliwekeza kwenye biashara ila kwa Fa itakuwa alitia hata milioni 200 kwajili ya kampeni za ubunge, kuwatuliza wajumbe, n.k
AY mbona kama kachoka Sana na mke kamkimbia? Anaweza kweli kuwa alipata 2bn?
 
AY mbona kama kachoka Sana na mke kamkimbia? Anaweza kweli kuwa alipata 2bn?
Mke wake ni wa Rwanda, itakuwa hakuzoea maisha ya ndoa za kibongo, licha ya hivyo matatizo ya ndoa hata kina bill gates yamewapata.

Sio yeye pekeyake alipata hio bilioni 2 na milioni 150, ni yeye na mwana Fa, mwanasheria wao aliewasimamia Albert Msando nae hakutoka mtupu.
 
Back
Top Bottom