Msanii Ray C azidiwa na Madawa ya Kulevya; asaidiwa na Polisi

Msanii Ray C azidiwa na Madawa ya Kulevya; asaidiwa na Polisi

Fanya mambo yako achana na dada wa watu,kinachokufanya ulie ni nini kwani uliombwa ufuatilie maisha yake? Mbona usililie mateja huko barabarani au vichaa au wafungwa huko jela?
Mind your own business, mtu hata hakufahamu we unadai eti 'nimelia sana' .
Moja ya mambo yangu ya kufanya ni hili, vipi kuna shida yoyote shogangu?
 
Bongo fleva wengi ni wapuuzi tu. Wakipata vihela kidogo wanajiona na kusahau maisha ni jinsi unavyoamua wewe.
 
Sukar ilivyopanda bei hujawalilia watanzani, serikali ilpokataza bunge live hujalia. Serikali kuja na burget yenye mzigo wa kodi pia hikulia. Hili tu ndo linakuliza

Huyu mungu kweli kaumba vitu vya ajabu
 
ClIbrLeUsAgPjv_.jpg
 
Jamani tumuombee Ray C kwa Mungu aweze kupona kwa hatua aliyofikia ni Mungu tu anayeweza kumuokoa. Nimeona clip yake akiwa kachanganyikiwa nimelia sana. Watu tunafanya makosa ila bahati nzuri gharama zake sio kama kosa la kuonja unga. Mungu msaidie Rehema. Amin!
Uhai na uzima uko katika ulimi wako.
 
Fanya mambo yako achana na dada wa watu,kinachokufanya ulie ni nini kwani uliombwa ufuatilie maisha yake? Mbona usililie mateja huko barabarani au vichaa au wafungwa huko jela?
Mind your own business, mtu hata hakufahamu we unadai eti 'nimelia sana' .
kweli kabisa mdau wako watu wengi wanashida hapa duniani kuna wafungwa,wagonjwa,wajane na yatima
 
Fanya mambo yako achana na dada wa watu,kinachokufanya ulie ni nini kwani uliombwa ufuatilie maisha yake? Mbona usililie mateja huko barabarani au vichaa au wafungwa huko jela?
Mind your own business, mtu hata hakufahamu we unadai eti 'nimelia sana' .
Unafiki tu,eti amelia saaaana,kwan ray c ndo teja wa kwanza bongo???kashalia kwa wangapi mpaka sasa???aache ukude
 
Ray C ni Mtu mzima lakini daah mimi nina roho ngumu lakini hapana namuonea huruma. Ray C amekamatwa akiwa kaharibika hajielewi, she really needs our help but what help wakati alisaidiwa ili aache akarudia? Ooh my, wanasema Police wamemkamata kwa kutaka kufanya Suicide attempt (hitting her self with knife).

Daah anatia huruma aisee, remember we are human not animals. Lakini Tutamsaidiaje labda awe Jailed.

Mbaya zaidi she failed to identify police amewambia WAHUNI/mateja wenzake eti anatekwa wamsaidie.

Sorry Kwa Kuweka Link ya Hii video uangalie.



=========
More:

Hali ya kiafya ya mwanamuziki mkongwe Rehema Chalamila ‘Ray C, imeonesha kuwa tata kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni matumizi ya madawa ya kulevya jambo lililoleta sintofahamu baada ya video inayozunguka mitandaoni ikionyesha akichukuliwa na Polisi huku akisema kuwa wanamteka.

Habari zinadai kuwa mama yake mzazi amekuwa akikesha kumtafuta mrembo huyo kutokana na kuzama kwenye vijiwe vya mateja wa madawa hayo na kushindwa kuonekana nyumbani kwani kwa siku kadhaa na watu kujitokeza kumsaidia bila mafanikio.

Sambamba na hilo, siku za hivi karibuni mwanamuziki Jay Dee, alionekana kuwa naye karibu na kudai kuwa Ray C, anahitaji marafiki wazuri na watu wavumilivu kuweza kumsaidia kwani kumlaumu pekee hakuwezi kumjenga bali ni kumzidi kumharibu kisaikolojia.

Mmoja wa wasanii wa Bongo Movie, Esha Buheti, kupitia mtandao wa kijamii ameweza kueleza jinsi gani alivyoguswa baada ya kumuoa Ray C akiwa chini ya ulinzi wa polisi akiwa hajitambui na kuongea maneno yasiyoeleweka na kudai kuwa awali alijua mrembo huyo anasingiziwa tuu.

Ameandika “Nashindwa hata niongee nini jamani, Ray C leo Kinondoni umenitoa machozi, jamani tufanye kitu tumsaidie Ray C, I mean it jamani siku zote nlikuwa najua anaonewa ila nilichokishuhudia leo nimeumia kutoka moyoni amedhalilika mwanamke mwenzetu, jamani tufanyeje?”

Akaendelea “Nilikua na Kabula, Kinondoni kwa wapemba tumefuata chips mara tukasikia mtu anasema me Ray C nataka kuvua nguo, nikajua utani kushuka ni Ray C anasema nishikeni kuna watu wanataka kuniteka, alikuwa na nguvu sana watu kumshika akaanza kuongea vitu havieleweki, akaanza kutafuta kisu ajichome, watu walimzuia sana walishindwa akaanza kugaragara kwenye matope akipiga kelele,”

“Kiukweli nilijikuta nalia, mara ikaja gari ya polisi ikambeba ila kwa tabu sana, alikua akipiga kelele jamani nisaidieni msiniache. Kiukweli mpaka Ray C anaondoka na ile gari ya polisi sikujua anapelekwa wapi, alikuwa kama mtu alopata kichaa, YARRAB TUNAMSAIDIAJE RAYC?”.
 
Nae haishiwi vituko. Kila siku anakarudia hako ka mchezo ka kula ngada!
 
duh huyo ili kusaidiwa inatakiwa afungwe kwenye zile sero tunazoonaga kwenye movie chakula kinapitishwa chini ya mlango kwa miaka mitatu atapona kabisa
 
mwacheni jk ataenda kumpa dhamana ndio maana anafanya hivyo si aljua ana kinga?
 
Back
Top Bottom