Msemaji Mkuu wa serikali atoa uamuzi wa Baraza la Mawaziri kuhusu Ajali ya ndege Bukoba

Msemaji Mkuu wa serikali atoa uamuzi wa Baraza la Mawaziri kuhusu Ajali ya ndege Bukoba

pamoja na kupata promosheni lakini kuwa mkuu wa idara ya habari na mawasiliano ikulu ni kitu kikubwa kuliko kukaa pale kwenye zile ofisi karibu mnara wa askari.
Mkuu bandeko andeko, kwanza, mkuu wa Idara ni mkubwa kuliko mkuu wa kitengo!. Pili Ofisi za Idara ya Habari Maelezo ziliisha hama pale Samora, karibu na picha ya Askari, kitambo!. Makao Makuu ni Dodoma, ofisi ndogo ni pale JNICC.
P
 
Kwa navyoelewa bongo, hio ndio biashara imeisha
 
Huyu si walimuondoa Ikulu, sasa baraza linasemewa na msemaji wa Ikulu au wa serikali kwa ujumla, hiki kikao ni cha Ikulu nilidhani msemaji wa Ikulu ndio angejitokeza
Watanzania bado tunahitaji civic education kuhusu uendeshaji wa nchi, Bunge, Mahakama na Serikali, kupitia kipindi maalum cha "kwa Maslahi ya Taifa", kinachorushwa na ITV, TBC, Star TV, Channel Ten na Azam TV, nimejitolea kusaidia hili.

Kikao cha BLM sio kikao cha Ikulu, hiki ndio kikao kikuu cha serikali, hivyo kinasemewa na Msemaji Mkuu wa Serikali kwa maelekezo ya Katibu wa Baraza la Mawaziri. Msemaji Mkuu wa Serikali na Mwanasheria Mkuu ni ma ex official wa cabinet meeting, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu haingii cabinet!.
P
 
Kama ikibainika kuwa ndege ya ajali ilikuwa haina hitilafu yoyote kwenye mifumo yake, basi lawama imwangukie Rubani Mkuu aka Captain, sababu alikuwa briefed kuhusu hali ya hewa inayozunguka Bukoba Airport wakati ndege imetua Mwanza, lakini akaamua kuendelea na safari hadi Bukoba.
Huu ni UONGO MKUBWA, wewe umeiona weather report ya Bukoba airport ya wakati ule wa ajali?,kuwa mwangalifu mkuu hapa kuna binadamu wenzetu wamepoteza maisha
 
Mkuu bandeko andeko, apokwe vipi wakati ni promosheni, amekuwa bosi kubwa!, Msemaji Mkuu wa Serikali pia ni Mkuu wa Idara inayojitegemea, Idara ya Habari Màelezo, ina vote yake, independent, na ndie bosi wa maofisa habari wote wa serikali, idara na wakala, akiwemo Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu ambacho ni kitengo tuu!. Gerson ni bosi wa Venus!.
P
Nimemkumbuka Ile siku ya royal Tour kule New York akitangaza mubashara
 
Ni hadithi za kila siku. Serikali inawafanya wananchi wote hawana akili:

1) Report ya wizi wa fedha BOT mara baada ya kifo cha Magufuli iko wapi?

2) Report ya Polisi waliomwua mfanyabiashara Mtwara iko wapi?

3) Report ya moto uliounguza soko iko wapi?

Hata hii itaishia hivyo hivyo. Labda report itakayopatikana ni ile ya kampuni ya ATR, maana hiyo haitakuwa chini ya Serikali ya Tz.
Inasikitisha sana.
 
"Serikali inawaomba wananchi wote kuendelea kuwa watulivu wakati uchunguzi huu unafanyika na baada ya uchunguzi kukamilika watajulishwa.
ushahidi wote ulimalizwa na kijana Majaliwa, cha msingi ni utekelezaji tu wa kuwajimbishana nani alizembea wapi hadi tukapoteza ndugu zetu.
 
Huyu mama sijui ana shida gani, hiyo kauli si ingetolewa bila kikao Cha dharula. Unavuta attention ya watu halafu unaleta utumbo. Huyu mama akae pembeni tupate Rais mwingine atakaye kuwa na maamuzi ya maana unaita kikao Cha dharula kuwaambia wananchi wawe watulivu.
Bibi kachemka vibaya sana.
 
Back
Top Bottom