Msemaji wa Serikali umedanganya; tuzo ya Nobel haijaenda kwa Raia wa Tanzania

Msemaji wa Serikali umedanganya; tuzo ya Nobel haijaenda kwa Raia wa Tanzania

Na aliondoka Visiwani Zanzibar hata Lanka ya Muungano, Means Tanzania haikuwepo

Ma CCM yanapenda sifa za Kijinga sana
Mno. Wanapenda sana kujimwambafai, kwa masuala ambayo wala hawahusiki nayo. Wamekataa dual citizenship, ila wanatamani matunda ya dual citizenship. Nawaita CHICHIDODO
 
Tumheshimu Gurnah mwenyewe. Pamoja na kuikimbia Zanzibar, bado anajihisi kuwa ni Mtanzania, na sisi tufurahie hisia zake kuwa ni mwenzetu. Tusiwahukumu watu binafsi waliojikuta kuwa wakimbizi kutokana na mapinduzi ya 1964. Mapinduzi yo yote yana uzuri na ubaya, na yanaathiri watu kwa utofauti. Hatujatajiwa kama alichukuwa uraia wa nchi nyingine. Lakini hata akiwa na uraia tofauti, hayo ni matakwa ya kuishi na kusafiri bila bugudha; ni wazi kwamba si chaguo la roho yake.
😍
 
Huyo mtu ameondoka Tanzania mwaka 1960. Wakato anaondoka hakukuwa na nchi inaitwa Tanzania. Kulikuwa na nchi za Zanzibar na Tanganyika
Hiyo 1960 umeitolea wapi? 1960s ndio 1960? Jifunze kizungu basi kama huwezi elewa kiingereza.
 
Kuna watu wamezoea uongo kwa kila jambo hata kama halina umuhimu wa kudanganya.
MATAGA ni shiidaa kwa fix..!!
 
Prof. Gurnah aliyeshinda tuzo ya Nobel siyo raia wa Tanzania Kama serikali na viongozi wengi pamoja vyombo vya habari vilivyoripoti. Huyo ni raia wa Uingereza Mwenye asili ya Tanzania.

Msemaji wa Serikali hapaswi kuandika kwa kuangalia mitandao bali anapaswa kufanya utafiti. Haina haja kuwa na msemaji wa serikali na viongozi wa serikali wanaodanganya umma au kuripoti habari bila kujirizosha. Nadhani tuwe watu wakufanya utafiti.
mtanzania wa kwanza kupewa uraia wa nchi mbili huyo 😀
 
Revisiting Gurna.
IMG_0155.JPG
 
Prof. Gurnah aliyeshinda tuzo ya Nobel siyo raia wa Tanzania Kama serikali na viongozi wengi pamoja vyombo vya habari vilivyoripoti. Huyo ni raia wa Uingereza Mwenye asili ya Tanzania.

Msemaji wa Serikali hapaswi kuandika kwa kuangalia mitandao bali anapaswa kufanya utafiti. Haina haja kuwa na msemaji wa serikali na viongozi wa serikali wanaodanganya umma au kuripoti habari bila kujirizosha. Nadhani tuwe watu wakufanya utafiti.
Ngoje aibuke kwenye vyombo vya habari aseme haitambui Tanzania. Alipoondoka hakukua na pirika za Nyerere na vugu vugu la maji maji. Kipindi hiko ni Zanzibar na Tanganyika. Kiilivyo hata sie wengine tumezaliwa na kufumbua macho tunaitwa watanzania, bado tunajitambulisha wazanzibari ...

👉 angalizo tuu muungano huu bado hauna ridhaa za wazanzibari.
 
Angekua bongoland labda angeishia kuitwa mchochezi au gaidi kwasababu hatunaga tamaduni yakuheshimu mawazo makubwa ya mtu.Ata hivyo haishangazi sana kwa hii nchi kujipendekeza kwa mtu aliyepata mafanikio kwa jitihada zake binafsi au nje ya nchi kwa sisi kujipendekeza kwake nakujifanya niwakwetu wakati kabla ya hapo hatukua na mpango naye.Hii tabia inadhihirisha jinsi ambavyo hatupendi kuandaa vya kwetu bali tunasubiri viandaliwe na wengine alafu sisi tudandie kwa mbele.
 
Wamesema mwenye asili ya kitanzania na siyo mtanzania. Aliondoka Zanzibar 1960 kwenda uingereza Kama mkimbizi na alipata uraia wa uingereza. Tanzania hairuhisu uraia pacha hivyo ni wazi ilimlazimu kuukana uraia wa Tanzania.
Uraia wa Tanganyika iliyojipa jina Tanzania ndio alioukimbia.
Katuacha sisi tukilazimishwa tuwe wa Tanganyika kwa jina la Tanzania kwa marisasi Na viboko kila unapokuja uchafuzi unaopewa jina la uchaguzi
 
Huyo mtu ameondoka Tanzania mwaka 1960. Wakato anaondoka hakukuwa na nchi inaitwa Tanzania. Kulikuwa na nchi za Zanzibar na Tanganyika
Kwa hiyo waliozaliwa kabla ya muungano sio Watanzania?
 
Nimefuatilia sana hii issue... jamaa ka-trend ile mbaya!

Kama u-Tanzania wake ni uzushi basi itakuwa tunamuonea Msigwa kwa sababu, nimefuatilia sana hii habari! Wakati habari ya Msigwa, as of now, imekuwa posted Twitter 20 hours ago, Al Jazeera walitoa habari yao saa 24 zilizopita na wamemtaja kama Mtanzania.

New York Times, wao wanaonekana waliandika mapema zaidi, nao wamemtambulisha kama Mtanzania!!!

Media karibu zote kubwanchini UK , including Reuters, BBC, na The Economist ambazo ni za UK; wote hawa wamemtaja kama Mtanzania!!

Of course, The Guardian (UK) hawajamtaja kama Mtanzania bali wamemtaja kama "Zanzibari"!

Sijaona source HATA MOJA iliyomtaja kwamba ni Mwingereza!!

Hata zile ambazo hazikusema kwamba ni Mtanzania, ziliishia tu kusema "born in Zanzibar, based in UK", na source hizi ikiwa ni pamoja na Kent University alikozeekea!!

Hata wakati anatangazwa, aliyetaja jina hakusema ni Mwingereza bali "born in Zanzibar, active in UK"!

So, sitaki kuamini kwamba wote hao source yao ni Gerson Msigwa!!!

Na Wachangiaji wengine hapa wanadai katoka ZNZ kabla ya Muungano, na kwahiyo haiwezi kuwa Mtanzania!!!

Hapa sources nyingi zinaonesha "alikimbia" ZNZ mwishoni mwa 1960's!! Sources hizo ni pamoja na Kent University!!

Source pekee ambayo inaweza kuendana na hayo madai, ni New York Times ambao wameandika "Then, in 1964, a violent uprising forced Gurnah, at age 18, to flee to England." Hata hivyo, source zote zinasema amezaliwa 1948, na kwahiyo kama alikimbilia UK at the age of 18, ina maana alishakuwa Mtanzania!!

Hata hivyo, sources nyingi zinasema Mwamba alimbilia UK akiwa 20 years!! Na tukiacha hizi hypes za sasa, back 2001, The Guardian UK liliandika
In 1969, a young African fled persecution in Zanzibar for what he envisaged as freedom in Britain. Here, the novelist recalls what he found and reflects on what has happened in the years since.
Hayo yalikuwa ni mahojiano kati ya The Guardian na Abdulrazak Gurnah!! Na katika mahojiano hayo, The Guardian wanamnukuu Mwamba akisema"-
I arrived in Britain at around the same time, although I wasn't Asian. I came from Zanzibar, a small island off Africa which in 1964 had seen a violent uprising that led to catastrophic upheaval. Thousands were slaughtered, whole communities were expelled and many hundreds imprisoned. In the shambles and persecutions that followed, a vindictive terror ruled our lives. At 18, the year after I finished school, I escaped. Many others did the same; some were captured and disappeared, most got safely away.
Of course, ni contradicting kwa sababu kama alizaliwa 1948, na kwamba alitoroka when he was 18, it means it's 1966 and not 1969 as said above!!

Lakini makala/ripoti inaanza kwa kusema:-
They didn't call it asylum then. The phrase was illegal immigrant. When I came to England in the late 60s, Sergeant Pepper was ruling the land, de Gaulle was the Great Satan and it was only months before Enoch Powell made his classical allusion to the Tiber.
Sentensi hiyo inaendana na 1969, na kwahiyo sina shaka Dully aliondoka ZNZ wakati tayari akiwa Mtanzania!! That having been said, tuachieni Mtanzania mwenzetu, na kama hamtaki, juzi tu hapa mmekopeshwa Mtanzania mwingine aitwae Kibu Denis... mchukueni huyo ambae, Haji Manara amempa kabila la Makonde!!

But wait... mbona incontinency kwenye hiyo miaka?

Hebu waungwana naomba mnijuze....

Ule unyanyama wa during and after revolution kule ZNZ uliendelea hadi mwishoni mwa 1960's especially kwa watu ambao hawakuwa Politicians kama ilivyokuwa Braza Dully?!!

Sijui kwanini nahisi Babu Dully na yeye alikuwa mjanja mjanja tu kama Watanzania wengine kwa kuamua kujilipua hadi kwa Malkia kwa gia ya ukimbizi!! I know, by the time, Mzee Karume alikuwa Mafia kweli kweli kwa Wanasiasa Wasomi lakini kwa kavulana ka miaka 18-20?! Haya bhana....

Sema kama Babu Dully kama anajitangaza mwenyewe na kujiona ni Mtanzania, akitaka kujua kama kweli yeye ni Mtanzania basi autangazie ulimwengu kwamba "...hatimae nimeamua kurudi nyumbani kugombea urais ama wa ZNZ au Tanzania" kisha baada ya hapo aanze kutembelea pages za Msigwa na za Uhamiaji

Nachoipendea nchi yangu, wale wanaokupigia matarumbeta hii leo ndio watakaotangaza wewe sio Mtanzania na wale ambao leo wanasema wewe sio Mtanzania, ndio hao hao watakaosema "wewe ni Mtanzania swafi..."
 
Yeye ni mzawa wa Zanzibar. Alifukuzwa nchi yake Zanzibar wakati wa yale mapinduzi ambayo ni haramu yaliyomwaga damu za watu wasio na hatia.
Kweli mnatuona machogo mazuzu kabisa. Abdulrazak Gurnah alizaliwa katika Sultanate ya Zanzibar ambayo ilikuwa ni Protectorate ya Uingereza. Hajawahi kuwa raia wa Oman. Aliondoka ( hakufukuzwa) Zanzibar mwaka 1967 kwa visa ya utalii ambayo alipewa na ubalozi wa Uingereza uliokuwa Dar es Salaam. Wakati anaondoka alikuwa amemaliza sekondari na alikuwa ameajiriwa kama mwalimu. Wakati anaondoka aliondoka kama raia wa Tanzania.

Kwa maelezo yake mwenyewe Mapinduzi yalikuwa na watu kutoka jamii zote. Anakumbushia Abdulrahman Babu alikuwa afisa mkubwa serikalini. Anakumbushia pia kuwa mke wa Karume alikuwa Mhindi. Anasema hali ilibadilika sana mwaka 1972 baada ya kuuawa kwa Karume, wakati huo tayari yuko Uingereza.

Kama kuna ubaya alifanyiwa yeye na jamii yake, alifanyiwa na wazanzibari wenzake na sio machogo. Ukweli nyinyi ndio mnatakiwa kumuomba radhi kwa ubaya na maovu mliomfanyia. Hii kumkumbatia sasa baada ya kumsulubu sana ni unafik wa hali ya juu. Lakini ukweli ni kuwa niliacha kushangazwa na kauli zenu miaka mingi iliyopita.

Amandla...
 
Hata Tundu Lisu akipewa tuzo utashangaa Serikali ya Tanzania wana mpongeza japo kwa sasa hawataki kumuona. Na walitaka kumuua.
Huyu alie pewa hii tunzo ni Mtanzania wa kuzaliwa lakini ni raia wa Uingereza. Alitofautiana na wakubwa akahama nchi..
 
Back
Top Bottom