OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Your browser is not able to display this video.
Tunafahamu Dismas Ten ni moja wa maofisa ndani ya klabu ya Yanga. Kimsingi anaitambua mipaka yake nje na ndani ya ofisi
:
Yanga SC ni mshindani wa Simba SC kimasoko. Kila mmoja ana wajibu wa kuheshimu hatimiliki za mwenzake.
:
Kuna video imepostiwa na Ten ambayo haipo sawa kibiashara
:
➡️ Haki za Matangazo: Ten ametumia picha za Chama, akitangaza jarida la Yanga.
:
Nani amemruhusu kufanya Tangazo na mchezaji wa kampuni shindani?
:
➡️ Haki za Picha: Ten ametumia sura ya Chama, mchezaji halali wa Simba akiwa na jezi za Yanga bila ridhaa ya klabu husika
:
Je, Ten ni mwandishi wa habari? Je, kuna fair use?
:
Kimsingi hakuna fair use kwa sababu kuna commercial promo?
:
Simba wakiamua kumchukulia hatua Ten atakuwa na kesi ya kujibu. Ikumbukwe Ten ni ofisa wa Yanga na ametekeleza kosa hili akiwa kwenye shughuli zake za kila siku ndani ya klabu.
:
Je Yanga wamemchukulia hatua?
:
Kuhariri picha ya mchezaji sio kosa kama una lengo la
:
➡️ Kuhabarisha
➡️ Kutania (Fair Comment)
➡️ Matumizi yasiyo ya kibiashara (Fair use)
:
Simba wana haki ya kumshtaki kwa ajili ya "nominal damages", kwa sababu hili limezua mshtuko kwa washikadau na mashabiki wa klabu ya Simba SC.
:
Simba wana haki ya Compensatory Damages kwa Yanga SC kupitia mauzo ya hilo jarida ambalo Chama ametokea kwenye promo yake labda kama Yanga SC itamkana Ten na kumwadhibu.