Msemo Fyatu: Kwenye wingi wa maji safi, Mpumbavu Hufa kwa Kiu....Una Ukweli?

Msemo Fyatu: Kwenye wingi wa maji safi, Mpumbavu Hufa kwa Kiu....Una Ukweli?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
1637086635509.png


Msemo huu nimeunyambua toka kwa msemo mashuhuri wa Bob Marley kuwa "in the abundance of water a fool is thirsty". Yaani, ukifa kwa kiu wakati unezungukwa na maji safi na salama tatizo ni upumbavu wako...yaani umeshindwa kubuni namna yoyote (hata kulamba kama mbwa) kuyafikisha maji kwenye kanwa lako.

Watu wanaililia serikali umeme na maji..watawala nao wanalia...tumeshindwaje kuvuna umeme wa jua, upepo, au mawimbi? Teknolojia ya renewable energy iko mbali sana na inayowezekana. Mji mpya wa serikali Dodoma ungeweka lengo la kutumia nishati mbadala (RE) kuliko kusubiri mabwawa yajae.

Tunaweza vipi kutengeneza mabwawa ya akiba ya maji ya mvua na mito na kuyafungulia kina cha mabwawa ya umeme kikianza kushuka? Je, tunaweza kuweka Sera katika kodi kwa makampuni na watu binafsi kutumia umeme wa jua au RE nyingine kama sehemu ya energy mixture yao? Kwa kadiri wanaongeza matumizi ya RE wanapata afueni mbalimbali za kodi, mitaji, na?

Swali fyatu kwa kwelini hili...hivi kweli Tanzania Kuna tatizo la ukosefu wa maji na nishati?

Au tumekuwa ni mpumbavu anayelalamikia kiu akiangalia ndoo ya maji safi na salama? Akiiomba serikali imtengenezee kata ya kunywea maji.

MM (Mwanakijiji Podcast Returning Soon)
 
Ni upumbavu tu..juzi hapa mweI wa tatu maji yalikuwa yamefulika pale ruvu hadi yanataka kupita juu ya barabara iweje leo..eti maji hakuna..tunasingzia ngombe..wameshindwa kuchibwa bwawa kubwa la kutunza maji ya kunyshwa wtu Dar kwa mda mrefu.

Kuhusu mgao wa umeme hizo ni mbinu za team msoga kutengenza maIngira baishara za magenerayo na petroli zifanye kazi lakini pia kunazwngww linatengenzwa ilo upigaji na mikataba ya hovyo iingie.

Unaona mama hata hajihangaishi kulitarifu taifa ya nini kimetokea..yeye nikutoa trilion1.7 kununa ndege wakati jiwe aliishanunu nswge 11 kwa triion 1.3 harafu nao wanakuja kuanza kutafuta visabbau vya kununu ndege 4 kwa trillon 1.7
 
Hakuna uhaba wa vyote hivyo. Uhaba uliopo ni artificial ili watu watengeneze madili wapige mpunga.

Bwawa likishajaa haliwezi kauka miezi 4 tu kukosa mvua. Bwawa ni kaziwa kadogo, kinachoendlea ni justification ama ili tuone mradi wa maji wa bwawa la Nyerere si tija tena to switchover kwenda kwingine ama mkakati wa kupiga deal.

literally is nothing but the game so called let " fool the fools". As usually the fools rush in where angels fear to tread.
 
MkamaP, unafikiri kuna uwezekano watu wanasabotage mabwawa haya ya maji? Maana vitu vingine haviingii akilini kama ulivyosema. Rais labda ataenda mwenyewe kuangalia bwawa la JNHP
 
Mawaziri wa Kiswahili kutokea Pwani hawaaminiki kabisa

Jaffo alituambia kajenga madarasa na zahanati za kututosheleza kwa kutumia fosi akaunti kumbe hamna lolote Ummy anaridia kazi ile ile

Huyu Awesu naye kasifiwa kweli, kumbe hamna lolote Dar es salaam imeingia katika mgao wa kihistoria wa maji.

Huko kwenye umeme naomba nisitie neno.
 
Mawaziri wa Kiswahili kutokea Pwani hawaaminiki kabisa

Jaffo alituambia kajenga madarasa na zahanati za kututosheleza kwa kutumia fosi akaunti kumbe hamna lolote Ummy anaridia kazi ile ile....
Mawaziri wa pwani? Waswahili?..ina maana matatizo ya umeme yanamhusu alie ingia mwezi mmoja Tu?? Aliekaa miaka hapo hahusiki??..

Wakiwa waswahili lakini hawatoki pwani je?
Watafaa??

Au wa pwani lakini sio waswahili?
 
Lengo la Ku sabotage?
Hakuna sabotage yoyote, ni lack of vision tu, na kila MTU anawaza kushinda uchaguzi kwa heri au Shari. Au umesahau yule Dada mbunge aliyesema tena mbele ya bunge tukufu kuwa Jinsi Ubunge ulivyo mtamu yuko tayari hata kuua?? MTU kama huyu utaniambia kichwani mwake kumejaa nini?
 
MkamaP, unafikiri kuna uwezekano watu wanasabotage mabwawa haya ya maji? Maana vitu vingine haviingii akilini kama ulivyosema. Rais labda ataenda mwenyewe kuangalia bwawa la JNHP

Bila shaka kabisa, ni mkakati tu wakutu "brainwash" train our brains to believe in what they want us to believe and think.

Bwawa la maji haliwezi pungua maji ndani ya miezi 4 maana hayo yalishajaa kitambo.
 
Back
Top Bottom