Mshahara wa 2,116,000 kwa Kikokotoo kipya atalipwa shilingi ngapi akistaafu?

Mshahara wa 2,116,000 kwa Kikokotoo kipya atalipwa shilingi ngapi akistaafu?

Naomba kwa wenye utalamu wa kujua kwa mtumishi mwenye mshahara 2,116,000. Na kafanya kazi kwa miaka 32.
Kwa kikokotoo hiki kipya
1 atalipwa keshi tshs ngapi?
2 pesa ya kila mwezi atakuwa anachukua kiasi gani
Naomba kwa anaejua anisaidie
Unataka umvizie Ili umuue? Ndio maana namsifu Mzee wangu hakuna mtu alijua amepata kiasi gani
 
Mi mwenyewe wangu ni 1.87mil na bado nina marupurupu ya laki8 kila mwezi hayapungui hata nisipofanya kazi
Mi pia mwalimu na nina 15yrs kazini
Uongo huu,malupuluou ya 800k kila mwezi uyatoe wapi? Kwa kazi gani?
 
Kimsingi mfuko uwa unaangalia ile mishahara mikubwa zaidi ya miezi 36 (miaka mitatu) ambayo mwanachama alipokea ndani ya miaka kumi ya mwisho wa utumishi wake kabla hajastaafu. Hiyo mishahara mikubwa zaidi ya miezi 36 ndiyo ujumlishwa kwa pamoja na kisha kugawia tatu (yaani miaka mitatu) ili kupata wastani wa kipato hicho kwa mwaka mmoja mzima. Hiyo ndiyo APE kwenye formula Iliyotolewa na mdau kwenye comments za awali. Pia mfuko uangalia idadi ya miezi mwanachama aliyochangia kwenye mfuko (ambayo kwenye formula ndiyo N). Hivi vitu viwili ndivyo ubadilika kwenye formula kutegemea mwanachama na mwanachama wakati vingine havibadiliki.
Hivyo formula ya kupata kiasi cha mkupuo kusomeka kama ifuatavyo:
Commutted Pension Gratuity= (1/580) x N x APE x 12.5 x 33%.

Au kama hautaki kuangaika na mahesabu marefu tumia formula hii kupata pesa ya mkupuo:
0.007112 x N x APE.

Na formula ya kupata pension ya kila mwezi formula ni hii hapa chini:
(1/580) x N x APE x 1/12 x 67% au kwa kifupi chukua 0.0000963 × N x APE.

Kwa kutumia mshahara wa 2,116,000 na idadi ya miaka 32 (miezi 384) aliyotoa mleta mada hesabu inakuwa hivi:
Mkupuo: (1/580) x 384 x [(2,116,000 x 12 x 3)/3] x 12.5 x 0.33= TZS 69,346,427.60.
Kinachowekwa kwenye calculator na formula kuu mbona havifanani? ?
 
Laiti ungejua hali ya maisha ilivyo kwa sasa usingesema hivyo. Ila pia inategemea na mapato yako kwa sasa unapoyalinganisha na kiasi hicho cha pesa. Kwa wengine wataona ni pesa nyingi Sana. Lakini kwa baadhi ya wanaopata kiasi hicho hutwo ni tuela twa mboga tu, zaidi ya hapo waweza kulala njaa na familia yako ya watu watano.
kweli hatufanani mkuu mm naiona nyingi sana aisee
 
ndio mana messi alikuwa GOAT kweli magoli kibao na assit za kutosha CRZ asist likuwa mpaka akaanza kushtumiwa na mwingine ni SALAH anataka altew afunge yeye tu wakipoteza mpira hawakabi. ALIYEPIGA goli mara nyingi ananenda Kumshukuru aliyetoa pande. Kwangu mimi mfungajii ni muhmu sababu anapewa pas yey amalize tu yani kaaminiwa ku finnish the job ni akifunga anakuwa amekamiliha kazi alyopewa ngi hata goli liko wazi wanapiga juu au kumlenga kipa n.k
 
Ukitoa Makato
Bima
Cwt
Kodi
Anabaki kama na 1.2 hivi sijui hapo kwenye bima na CWF wanakataje, ila si haba japokuwa mishahara ya serikali Kwa baadhi ya watu ni pasua kichwa na ukute huo mshahara ni wa staffs aliefanya kazi zaidi ya miaka 20

Anyway, back to the point embu check kwenye website ya PSSSF, I guess kutakuwa Kuna formula. Na mara nyingi huchukua mishahara minono ya muda flani na Kuna formula ya kukupa mafao ya mkupuo then baadae ukomae na pension huku serikali ikiendelea kuomba wastaafu wafe maana Kila baada ya muda mnaenda kuhakikiwa.

Check website ya PSSSF
 
Back
Top Bottom