Jiandae kwa ibada ya Jumapili 15 September, 2024.
Kesho Tarehe 15/09/2024 ni Siku ya Bwana ya 16 baada ya Utatu Mtakatifu:
Masomo ya Siku
Zaburi ya siku : Zab.119:145-152
Somo la Pili: Mt.12:9-14
Somo la Mahubiri: Gal.5:13-15
VVVVVVVVVVVVVVVVVVVVV
Zaburi ya siku
Zab.119:145-152
145 Nimeita kwa moyo wangu wote; Ee Bwana, uitike; Nitazishika amri zako.
146 Nimekuita Wewe, uniokoe, Nami nitazishika shuhuda zako.
147 Kutangulia mapambazuko naliomba msaada, Naliyangojea maneno yako kwa tumaini.
148 Macho yangu yalitangulia makesha ya usiku, Ili kuitafakari ahadi yako.
149 Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako, Ee Bwana, unihuishe sawasawa na hukumu yako.
150 Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki, Wamekwenda mbali na sheria yako.
151 Ee Bwana, Wewe U karibu, Na maagizo yako yote ni kweli.
152 Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako, Ya kuwa umeziweka zikae milele.
Zaburi 119:145-152
``` VNNNNNNMMMMMMNNNNNNVVV
Somo la pili:
Mt.12:9-14
9 Akaondoka huko, akaingia katika sinagogi lao.
10 Na tazama, yumo mtu mwenye mkono umepooza; wakamwuliza, wakisema, Ni halali kuponya watu siku ya sabato? Wapate kumshitaki.
11 Akawaambia, Ni mtu yupi miongoni mwenu mwenye kondoo mmoja, na yule kondoo ametumbukia shimoni siku ya sabato, asiyemshika akamwopoa?
12 Je! Mtu ni bora kuliko kondoo mara ngapi? Basi ni halali kutenda mema siku ya sabato.
13 Kisha akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako; akaunyosha, ukapona, ukawa mzima kama wa pili.
14 Lakini wale Mafarisayo wakatoka wakafanya shauri juu yake jinsi ya kumwangamiza.
Mathayo 12:9-14
VVVVBBBBBBBBBBBBBBBBBB
Somo la Mahubiri
Gal.5:13-15
13 Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru; lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo.
14 Maana torati yote imetimilika katika neno moja, nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako.
15 Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.
Wagalatia 5:13-15