Mshikaji wangu ameanza kucheza forex, kila siku anauza vitu kidogo kidogo

Mshikaji wangu ameanza kucheza forex, kila siku anauza vitu kidogo kidogo

Status
Not open for further replies.
Haka kabiashara ukiingia kichwa kichwa utapigwa za uso sana..

Vijana kuweni makini, na sio FOREX na pia BITCOIN pamoja na NETWORK MARKETING kuweni makini nazo

USIJE UKASEMA HATUJAKWAMBIA, 2019 NI MWAKA WA MABADILIKO

Alishawahi kusema mtu ukiona unasisitizwa sana na kushawishiwa sana juu ya FURSA , kaa ujue kuwa wewe ndio FURSA!!!
Mkuu ulopotelea wapi nilizoea kukuta namba moja kila post?
 
Alianza kama utani baada ya kurudi likizo ya semister ya mwisho huyu mshikaji wangu wa chuo sijui alikutana na nani huko kwao akamshauri kuhusu mambo ya forex,

Alivyorudi akanisimulia kuhusu hiyo inshu mi nilichomwambia ni kitu kimoja tu hiyo kitu ya forex mi nilishasoma sana mada zake huko Jamii forum kwa kina Ontario na kujua hasara na faida zake kuna watu wameunguza acount zao wanalia kilio cha mbwa koko hakunisikia,

Sasa bhana wale watu aliokutana nao huku wakawa wanamshauri anatoka dom to dar kwenye semina na darasa lao na kila akirudi story ni forex,forex na yeye,

Basi bhana miezi kadhaa imepita baada ya kutrade sana na ile acount ya dermal kafungua real Account kinachomkuta huko mi sijui naona tu kila siku anauza vitu,

Alianza na Laptop yake min, akafata desk top yake ,juzi kati kauza mtungi mkubwa wa gase pamoja na jiko lake, naona kabakiwa na friji pamoja na kitanda na ata hivyo naona analipigia mahesabu friji anataka kuliuza na hilo sasa sijui kimempata nini huko kwenye forex,

Daily nampa ushauri aachane na hiyo biashara yake ya forex naona hanisikii sasa mi nasubiri kuona mwisho wake.


Sent using Jamii Forums mobile app
Atauza kila kitu mwambie aache kucheza forex maana forex haichezwi kila anayecheza lazima akione cha moto.
FOREX inahitaji watu serious ambao wana dedicate muda na kuielewa wana trade. lakini kwa wanaocheza watalia kilio cha mbwa aliyepigwa jiwe gizan
 
Cheza na ww ili usiandikie mate nakati wino upo.

Prondo ni heri ukishindwa sana kufanya biashara yoyote basi uwe kama wale Mateja day worker wanaopiga debe kuhusu ukonda pale stendi Rafiki.

Hakuna utapeli unaoshamiri kwa kasi sana kama hizi biashara za mitandaoni.

Kuna Rafiki yangu m1 yuko Mwanza alinishawishi niingie QNET kwa mbwembwe nyiiingi za mafanikio ya rafiki zake nilitaka kuingia kwa 6,000,000/= lakini bahati mbaya nilipungukiwa kiasi cha 900,000/= na nilijitahidi kuitafuta zaidi ya wiki 1 niliipata kukamilisha 6,000,000/= lakini roho yangu ilisita sana.

Kifuatacho sasa hivi yule Rafiki yangu aliuza gari, nyumba na hadi sasa hivi anaishi kama shetani kwenye nyumba za kupanga.

Tafadhali kijana fanya biashara halisi(physically contact with customers) lakini hizi biashara za mitandao(online businesses) ni utapeli mtupu kwa 100%.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unawezaje kufananisha forex na q net???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuza $40 mpaka ikakaribia 500, stop loss ikatembea na mzigo wote siku ya news CAD baada ya hapo kila nikijipanga wanaondoka na mzigo mazima, nikasema nitakuja kulaza njaa watoto!
Bila shaka ulijilipua.... halafu shida moja ni kwamba ukishachoma account.... huwa inasumbua kdg kuja kukaa sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cheza na ww ili usiandikie mate nakati wino upo.

Prondo ni heri ukishindwa sana kufanya biashara yoyote basi uwe kama wale Mateja day worker wanaopiga debe kuhusu ukonda pale stendi Rafiki.

Hakuna utapeli unaoshamiri kwa kasi sana kama hizi biashara za mitandaoni.

Kuna Rafiki yangu m1 yuko Mwanza alinishawishi niingie QNET kwa mbwembwe nyiiingi za mafanikio ya rafiki zake nilitaka kuingia kwa 6,000,000/= lakini bahati mbaya nilipungukiwa kiasi cha 900,000/= na nilijitahidi kuitafuta zaidi ya wiki 1 niliipata kukamilisha 6,000,000/= lakini roho yangu ilisita sana.

Kifuatacho sasa hivi yule Rafiki yangu aliuza gari, nyumba na hadi sasa hivi anaishi kama shetani kwenye nyumba za kupanga.

Tafadhali kijana fanya biashara halisi(physically contact with customers) lakini hizi biashara za mitandao(online businesses) ni utapeli mtupu kwa 100%.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kabla ya kufanya biashara ya Forex huu ujumbe unapatikana kwa kila broker awapatie trader wake.. Sasa sijui kama nyie huwa mnaelewa kinachoandikwa hapo.


Yaani mtu mzima unafananisha Ujinga ujinga na upuuzi wa Qnet na Forex ?? Biashara ambayo ni halali kwenye nchi ya dunia za kwanza miaka na miaka. Hiyo Qnet ni pyramid scheme bussines ambayo katika nchi kama marekani ni kosa la jinai kufanya Ponzi bussines na ukikamatwa ni kifungo.



Ninachojifunza hapa, watanzania ni wavivu wa kutafuta maarifa kabisa. Hufanya maamuzi kwa kusikia watu wanasema nini. Mtu akisikia Deci anaenda. Akisikia D9 anaenda . Akisikia Forex anaenda ila hana sababu zake za kiutafiti kwanini kafanya hayo maamuzi.


Amini nakwambia ukifanya utafiti wako kuhusu biashara ya forex bila kuwa bias utakuja kunitafuta siku moja. Kama una king'amuzi cha Dstv weka channel namba 411 (Bloomberg Tv) naamini utaelewa Forex ni nini.




Sasa Kama MTU anasema forex ni utapeli hivi ukisikia biashara ya stocks, commodities, indices na shares si ndio mtasema ni ujambazi. Hebu nikusaidie tafuta gazeti la either The citizen au Daily News nenda kwenye ukurasa wa bussines utakuta FOREX,INDICES,SHARES & commodities zinachambuliwa vyema kabisa.

Maarifa Maarifa Maarifa .... Tafuteni maarifa. Inauma sana mwaka 2019 bado kuna kiumbe duniani anasema FINANCIAL MARKETS ni utapeli . Bado kuna mtu anashidwa tofautisha Marketing Network na Financial Markets.




IMG_20190101_152425.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli kila mtu na mawazo yake mimi ukiniambia niache forex ni sawa na kuninyonga tena kwa mateso makali pamoja na changamoto zote lakini sa hv inanuchukua hadi nafikisha miezi mitatu sijaenda bank kuchukua mshahara nina balance ya $2000 na taget yangu ni 5% kwa siku hebu niambie napata sh ngap kwa mwezi maisha ni raha sana aiseee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Atauza kila kitu mwambie aache kucheza forex maana forex haichezwi kila anayecheza lazima akione cha moto.
FOREX inahitaji watu serious ambao wana dedicate muda na kuielewa wana trade. lakini kwa wanaocheza watalia kilio cha mbwa aliyepigwa jiwe gizan
Hahahah.... umeongea ukweli kabisa.... Kama kuna mtu anacheza forex basi huyo anagamble...huo ndo ukweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom