Msilete Umjini wenu mkija kuzika kijijini

Msilete Umjini wenu mkija kuzika kijijini

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
MISIBA NA UMJINI WA WATU WA MJINI.
Vijana wa mjini ninawaomba sana bamyiitu, mkienda kijijini msilete umjini wenu kwenye mambo ya msingi. Jaribuni kufanya yale ya utaratibu wa kijijini. Salimia, nyenyekea, piga stori, chekesha, yaani fanya yote yafaayo kwa jamii ya wanakijiji uliowakuta pale kijijini. Vaa uhusika wote wa uanakijiji. Hautapungukiwa kitu.

Ukifika kijijini, pita nyumbani kwa watu wa pale kijijini wasalimie. Pita kwenye nyumba zilizopata misiba ili kuwapa salamu ya pole, nenda kawaambie "poleni na msiba". Wasalimie waambie "ndaga mwasyilile". Kufanya haya yote hakukuondolei umjini wako, yaani hakukupunguzii kitu.

Kukitokea msiba wakati upo pale shiriki, hudhuria msibani. Kama wewe ni mkaka ukiona watu wa umri wako ndo wanaofanya shughuli ya kuchimba kaburi nawe shiriki kuchimba kaburi, chimba. Kama ni mdada shiriki hata kupikapika. Kufanya hivyo hakukupunguzii umjini wako, yaani hakukupunguzii kitu.

Muda wa chakula ukifika hakikisha unashiriki. Usikipuuze kile chakula kwasababu ya kuwa kina makabeji yaliyopikwa hovyo, wewe kula tu. Na kwa wale wa kwetu Unyakyusani: hakikisha zile kande (ingaati) zetu zile unazila kisawasawa. Usiseme "hapana sili nimeshiba", kula. Kufanya haya hakuuondoi umjini wako, yaani hakutakupunguzia kitu.

Ninataka kumaanisha nini?

Tukutane siku nyingine, twaganile isiku ilingi...
@ Lusako
 
Waambie na hao wavijijini waache kusema sema hivyo ukipita wanasema,wanakutumbulia macho Kama wameona sijui nani kapita! Ukisema uchimbe kaburi ukishika sururu tu wanaanza kusema vilugha vyao! Waambie na wenyewe wabadilike..
 
Wakumbushe kaka,sio wanakuja kazi kuongea wao kwa wao ,wanapigiana story za mjini,wanasumbua watu ooh kanichajie simu,wapi kuna bia?ukienda kuzika shiriki mwanzo mwisho,hapo ndo chimbuko letu,na ndo tutakapozikiwa,tuheshimu tunaowakuta,tabia ya kuwa bize na smartphone msibani na kupigiana stori za mijini ziishe.
 
wakumbushe kaka,sio wanakuja kazi kuongea wao kwa wao ,wanapigiana story za mjini,wanasumbua watu ooh kanichajie simu,wapi kuna bia?ukienda kuzika shiriki mwanzo mwisho,hapo ndo chimbuko letu,na ndo tutakapozikiwa,tuheshimu tunaowakuta,tabia ya kuwa bize na smartphone msibani na kupigiana stori za mijini ziishe.
Inferiority Complex
 
Sururu unashika Kama umeshika mswaki, utachimbaje kaburi?
Haha! Labda wengine ndo hawajui lkn hapa sururu naielewa vizuri na ishanichubua mikono mara dufu.. lkn hata hivyo si mbaya kumfundisha mtu kama hajui mbona hata wao wakija mijini wanataabika ukimwambia tu awashe tv asalalee ataenda kutafuta kiberiti awashe tv..😂 kwenye matumizi ya smart phone Sasa utapata tabu maana unakuta mtu kanunua simu inayomzidi uwezo kimatumizi!

Ye kazi kuwasiliana,kusikiliza muziki na kuingia Facebook hayo mengine hajui na kumfundisha mtihani kazi kwelikweli.. mkuu nimeishi kijijini nawaelewa watu wa kijijini na for sure maasha ya kijijini nimazuri haswa mahitaji tulani yakiwa yanapatikana.. mixer kuamka mapema kufunga ng'ombe kwenda kulima.. kufanya matusi kwenye mashamba..😂 kijijini raha sana..
 
Wakaapo wenyeji usihangaike weka kitambaa eti nguo zitachafukaaa.... 😂
Nguo zikichafuka usikimbilie fuaa, 😂
Ikipita rubisi/ulanzi/mbege/gongo/buza etc kwenye kata/kikombe we piga pafu mojaaa mpasie na mwenzoo, hapo mwenge hauvuki kijiji!!! eti we wakuja kutoka mujini unataka utengewe special yako 🍷🍺....dadekiii
 
NO.why not mixing with your fellow mourners,why not participating fully on funeral activities?
Hauwezi kumridhisha mwanadamu kwa 100%

Ukibeba jeneza utaambiwa haujabeba kwa mikono miwili ilhali kila mtu alikuwa anataka kulibeba.

Ukimlilia marehemu watasema kilio cha kuigiza.

Kuna watu na viatu.

yna2 njoo huku
 
ni kweli ila na wao wawwe waelewa,siku nimezama kijijini kurekebisha kaburi la mdingi toka mbali sana na muda hauruhusu kukaa sana nilikua na siku 3 tu,nafika Mbeya mjini usiku huKu zikatumwa taarifa za msiba pale kijijini.

opposite kabisa na kwetu na bibi ndio rafiki mkubwa wa huyo mama na ni family friends kwa miaka mingi sana na tunashirikiana karibia kila kitu.
Sasa nikawa sina jinsi nifanyeje nicancel tkt nishiriki msiba au itakuwaje,ikabidi mdingi mdogo aingilie kati akasema twende tukafanye kilichokuleta ntaawaambia kabla watupe baraka zao.

aisee kufika pale kijijini safari ya kutoka dar uchovu niliokua nao na kesho yake kuna shughuli ya kuanza mapema tu nilifika nikasalimia msiba nikashusha pole yangu sukari ya kutosha wanywe chai na mafuta wakaange ndizi na mpunga nikapiga story na watoto wa marehemu ambao ni rafiki toka utotoni then baadae nikawa hoi kwa uchovu.

nikaaga ebana mi ngoja nikalale mana naweza hata kudondoka hapa. wakanambia poa kweli tunakuona unasinzia kapumzike,aisee nimeenda home kwani nililala basi? Nilikabwa na kitu kisichojulikana usiku ule ni kabisa kama vile mtu kaniwekea goti shingoni kuhema sihemi wala kutoa sauti siwezi. Mpaka nakurupuka nikarudi mwenyewee msibani wananiuliza si uliaga wewe vipi nikawaambia acheni tu tukeshe hapa
 
Back
Top Bottom