Msimamo wa Bunge ni upi kuhusu mradi wa Bandari ya Bagamoyo?

Msimamo wa Bunge ni upi kuhusu mradi wa Bandari ya Bagamoyo?

Mkuu, huelewi mkiendeleza fyokofyoko zenu hata hiyo Bagamoyo mtaikosa?

Hoja zitaanza kujengwa kueleza historia nzima ya ukanda huo wa Pwani. Mzanzibari na mtu wa Pwani watadai wao siyo sehemu ya Tanganyika, mnayoitambua nyinyi kama Tanzania kwa sasa.

Mama na ndugu yake watairudisha Bagamoyo mahali pake, na huo ndio utakuwa mwisho wa habari yenu.

'Seriously', kuna mkakati mkubwa kati ya hawa wawili na jamaa zao akina Rostam na Zungu na wenzao. WaTanzania wasiposimama kidete na kupiga kelele, maskini wa nchi hii hataambulia kitu. Tuna majitu manyang'anyi wakubwa wanaosubiri kunyakuwa kila kitu.

Ngoja tusubiri, tutayaona mengi safari hii.
Punguza fix.
 
Mkuu akipatacho mtu hutokana na jasho lake. Mwanasiasa ukimuamini sana utaishia kulaumu unapokuwa umekaa na marafiki zako.

Nimemuelewa vyema Rais anapozungumzia uwekezaji, huwezi kuwa na mitazamo ya uoga halafu ukaweza kufanikiwa kimataifa. Huwezi kuwa na pato kubwa la taifa kwa kutegemea wigo mwembamba wa ukusanyaji wa kodi.

Unauongeza wigo wa kodi kwa kuwa na wingi wa shughuli za kiuchumi kwa maana ya uzalishaji. Kusema kila siku kwamba wazungu wana nia mbaya na sisi ni kuendeleza dhana potofu za kimaskini.

Mzungu aliichora mipaka ya afrika mwaka 1884 wakati huo babu zetu wakiwa wanavaa vibwaya kama kipepe wa gazeti la sani. Mzungu huwezi kumkwepa kama kweli unataka kuwa na Tanzania yenye maisha ya uchumi wa kati na ule wa juu.
Hakuna ninapokataa katika haya uliyoandika hapa ila...
Siyo "mitizamo ya kiuoga', ni lazima uwe na mitizamo ya kujuwa unachokitaka katika uwekezaji huo na kujiamini kwamba unastahili na utakipata unachokitaka. Hata huyo mwekezaji naye haji hapa kiuoga, na atatumia kila fursa ili anufaike zaidi.

Kumbuka, uwekezaji ni mzuri kama unamanufaa kwetu. Hatuwezi kuwa na utitiri wa uwekezaji tukitegemea kwamba tutafaidika nao hata kama hauna manufaa kwetu.

Kwa hiyo sikubaliani na hiyo dhana ya kuwa na uwekezaji mwingi, ni uwekezaji wa manufaa ndio unaohitajika zaidi.

Hapa ndipo panaponikumbusha hii tabia yetu ya utegemezi. Uwekezaji siyo wa nje pekee, uwekezaji mkubwa unapaswa kuwa wa hapa hapa kwetu nyumbani. Tufanye kila juhudi kusaidia uwekezaji huo ufane zaidi.
Ninatambuwa huo wa mabilioni ya dola, kama hatuuwezi kwa sasa, siyo sababu ya kuacha kuhimiza na kulea huu wa vimilioni kadhaa.

Swala la wazungu/wachina, n.k.; wote wana maslahi yanayowaleta hapa, nasi tulinde maslahi yetu kila mara. Hakuna wakati wowote ilipotokea kwamba ukijiweka kupigwa utaacha kupigwa.
 
JK bado ana ushawishi mkubwa nchi hii. Spika alikuwa akiwaandaa kisaikolojia wabunge kabla Rais ajahutubia taifa kuhusiana na suala la bandari ya Bagamoyo.

Ni mchakato unaoendelea chini kwa chini wenye kuongozwa na Mzee wa Chalinze, sio mbaya lakini ukizingatia anaacha heshima nyumbani alipozaliwa na itadumu miaka mingi ijayo.

Isije kuwa ni kwa gharama ya kuiuza Tanzania, tukabakia na uhuru wetu wa bendera tukiwa na eneo ndani ya mipaka, ambalo hatuna nguvu ya kulimiliki.

Naomba Mungu hizo conditions za mradi zisije kutuumiza siku zijazo.
Watu Wana masikio lakini hawasikii, Wana macho lakini hawaoni.
Kwa akili ya kawaida tu unategemea watoke huko waje na pesa zao kwa ajili ya manufaa ya watu wa Tanzania?
 
Mkuu, huelewi mkiendeleza fyokofyoko zenu hata hiyo Bagamoyo mtaikosa?

Hoja zitaanza kujengwa kueleza historia nzima ya ukanda huo wa Pwani. Mzanzibari na mtu wa Pwani watadai wao siyo sehemu ya Tanganyika, mnayoitambua nyinyi kama Tanzania kwa sasa.

Mama na ndugu yake watairudisha Bagamoyo mahali pake, na huo ndio utakuwa mwisho wa habari yenu.

'Seriously', kuna mkakati mkubwa kati ya hawa wawili na jamaa zao akina Rostam na Zungu na wenzao. WaTanzania wasiposimama kidete na kupiga kelele, maskini wa nchi hii hataambulia kitu. Tuna majitu manyang'anyi wakubwa wanaosubiri kunyakuwa kila kitu.

Ngoja tusubiri, tutayaona mengi safari hii.
Kilichomitisha ni kwa nini haya yanafanyika kwa mufa mfupi sana. Miezi mitatu fastafasta anafufua miradi ya bandari bagamoyo na gesi. Kwamba mama ana haraka sana? Hata kukaa mwaka aone yanaendaje hataki? Kazi ipo
 
Kilichomitisha ni kwa nini haya yanafanyika kwa mufa mfupi sana. Miezi mitatu fastafasta anafufua miradi ya bandari bagamoyo na gesi. Kwamba mama ana haraka sana? Hata kukaa mwaka aone yanaendaje hataki? Kazi ipo
Kuna jambo hapa, siyo bure.

Huyu mama atakuja kutuweka katika hali ngumu ambayo hatukuitegemea kabisa.

Watu hawakumpigia kura aongoze taifa hili, sasa anafanya kila kitu kwa haraka kwa sababu anazojuwa yeye mwenyewe.

Tatizo la nchi hii watu hawana ujasiri wa kuhoji, wanabaki wakilalamikia pembeni basi.

Hata hao mawaziri wake, sijui kama haya yote yamejadiriwa kwenye vikao vyao, na kama yamepitia huko, huenda hata wao ilikuwa ni kupewa taarifa tu, hakuna lolote walilotakiwa kulichangia mawazo na kulifanyia uamzi wa pamoja.Mawaziri kila mmoja wao analinda maslahi yake!
 
Swala la Bagamoyo bora lijadiliwe JF kuliko Bungeni.
Hamna Bunge mle
Umeongea point mkuu gonga tano bunge la Jamhuri ya JF liko kazini kila mtu anajiwakili ccm toeni password kwenye mkataba zishushwe nondo hapa, Dodoma nao wanajiwakilisha wenye na matumbo yao sante mkuu
 
Mkuu akipatacho mtu hutokana na jasho lake. Mwanasiasa ukimuamini sana utaishia kulaumu unapokuwa umekaa na marafiki zako.

Nimemuelewa vyema Rais anapozungumzia uwekezaji, huwezi kuwa na mitazamo ya uoga halafu ukaweza kufanikiwa kimataifa. Huwezi kuwa na pato kubwa la taifa kwa kutegemea wigo mwembamba wa ukusanyaji wa kodi.

Unauongeza wigo wa kodi kwa kuwa na wingi wa shughuli za kiuchumi kwa maana ya uzalishaji. Kusema kila siku kwamba wazungu wana nia mbaya na sisi ni kuendeleza dhana potofu za kimaskini.

Mzungu aliichora mipaka ya afrika mwaka 1884 wakati huo babu zetu wakiwa wanavaa vibwaya kama kipepe wa gazeti la sani. Mzungu huwezi kumkwepa kama kweli unataka kuwa na Tanzania yenye maisha ya uchumi wa kati na ule wa juu.
Mkuu nakupinga tuko uchumi wakati sijui uchumi gani wakati mwingine unauzungumzia

Pili mchina sio mzungu wana mikataba mingi ya kilagai nchi kibao inawatesa

Hoja ni mikataba kuwa wazi kwanini mikataba hapa kwetu ni siri ?
 
Mkuu nakupinga tuko uchumi wakati sijui uchumi gani wakati mwingine unauzungumzia

Pili mchina sio mzungu wana mikataba mingi ya kilagai nchi kibao inawatesa

Hoja ni mikataba kuwa wazi kwanini mikataba hapa kwetu ni siri ?
Huyo mchina usiemuamini Nyerere alimuamini na kumpa reli ya TAZARA ajenge, na ndio ulikuwa mradi mkubwa sana kipindi hicho....kb pt
 
Back
Top Bottom