Msimamo wa Tanzania kuhusu Korona uliotolewa katika kikao cha Umoja wa Afrika AU ni ubabaishaji

Msimamo wa Tanzania kuhusu Korona uliotolewa katika kikao cha Umoja wa Afrika AU ni ubabaishaji

Mindi

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2008
Posts
3,523
Reaction score
4,992
Nimemsikiliza waziri Kabudi ambaye alimwakilisha Rais Magufuli kwenye kikao cha Umoja wa Afrika. Wakati Rais Ramaphosa wa Afrika ya Kusini akiwa ni mwenyekiti anayemaliza muda wake, akieleza jinsi korona ilivyovuruga mipango ya maendeleo katika bara la Afrika, Tanzania ilitoa msimamo wake na pia kushauri Afrika ichukue msimsmo huo.

Msimamo wenyewe ni Tanzania na Afrika kwa ujumla zijiimarishe katika tafiti za chanjo na madawa ili kuondoa utegemezi kwa "mabeberu".

Sina tatizo kimsingi na hoja hiyo. Kwa kweli ni hoja nzuri tu. Tatizo langu ni kwamba hii hoja inatokana na kelele zinazopigwa na viongozi wetu hivi sasa, ili kuenda sawa na misimamo tata ya Magufuli. Kauli aina hii ndio kama anazotoa Profesa Mchembe, katibu mkuu wizara ya Afya. Na ndio zinafanya wengine wanadiriki kupiga marufuku uvaaji barakoa. Ni ujinga na ujuha wa kiwango cha pekee.

Hakuna sera ya utafiti inayotuongoza kufikia hayo anayodai Kabudi, na hata ile "political will" tu haipo. Magufuli arundike mabilioni katika elimu ya juu na utafiti? Apunguze matrilioni yanayokwenda kwenye miundombinu? Aache miradi yaje ya Chato? Wala sioni dalili ya hilo kutokea, hata kama hizo sera zingeandaliwa.

Magufuli huyu anayewafrustrate maprofesa, anayedai vyuo vikuu vitoe hela ya GAWIO serikalini ili ajenge barabara, ndio asimamie miradi ya utafiti wa chanjo za korona, ambayovinahitaji matrilioni, utaalamu wa ngazi ya cutting edge, ambao unahitaji kujengwa na kutunzwa? Sioni hata dalili.

Magufuli sio mtu wa miradi ya muda mrefu, matokeo yaje yeye kaondoka. Anataka afanye na kukamilisha sasa.

Kwa hiyo akina Kabudi na Mchembe wanapiga sound kama za yule waziri wetu mpendwa wa viwanda, aliyetufundisha kwamba hata vyerehani 4 ni kiwanda
 
Comedy phase 3.

Wazungu wamefanya utafiti wa kiyasansi wewe unasema haukubaliani nao na unaagiza waganga wa jadi wafanye utafiti na baada ya wiki 2 wanakuletea vichupa vya dawa unakubali.
 
It is true. Tanzania haina kitu cha kushauri maana hatuna utafiti wowote wa kisayansi. Hii ya kujifukiza na hayo madawa fake ya mikongosho tunayoambiwa ni juhudi za kujiondolea aibu kutokana na msimamo wetu wa mwanzo kuhusu Corona.

Kwa jinsi Hali inavyoendelea ni sisi ndiyo tutaumbuka.
 
You are controdicting yourself. Hivi miradi ya SGR , Julius Nyerere Hydro power, elimu bure kwa watoto wa kitanzania, maboresho ya huduma za afya, ujenzi wa miundo mbinu ya barabara, umeme na miradi mingine mingi unayoijua siyo miradi ya matokeo ya muda mrefu.? Napata shida sana kukuelewa.
 
It is true. Tanzania haina kitu cha kushauri maana hatuna utafiti wowote wa kisayansi. Hii ya kujifukiza na hayo madawa fake ya mikongosho tunayoambiwa ni juhudi za kujiondolea aibu kutokana na msimamo wetu wa mwanzo kuhusu Corona.

Kwa jinsi Hali inavyoendelea ni sisi ndiyo tutaumbuka.
Yaani umeiweka vizuri sana. Badala ya kukiri tumekosea, halafu tukae kwenye mstari, tunazidi kutokomea porini, na visingizio tele
 
You are controdicting yourself. Hivi miradi ya SGR Julius Nyerere Hydro power elimu bure kwa watoto wa kitanzania, maboresho ya huduma za afya, ujenzi wa mondo mbinu ya barabara, umeme na majina mengine mengi unayoyajua siyo miradi ya matokeo ya muda mrefu.? Napata shida sana kukuelewa.
Kwanza Magufuli anapendelea miradi inayomwonesha zaidi kuliko ile ambayomatokeo yake yanachukua muda mrefu kuonekana na pia hayamwoneshi yeye moja kwa moja. Mfano mzuri, hana interest kivile na kilimo, ambapo ndio kiini cha matatizo karibu yote ya kiuchumi. Sijawahi nsikia anaongelea habari ya maafisa ugani, ambao ni moja ya sababu za kukwama eneo hilo. Kujenga barabara inaonekana haraka.

Hayo uliyotaja mengi yanakadiriwa kukamilika angalau kwa kiasi kikubwa ndani ya utawala wa miaka 5 hii, kama hatawazuia wabunge "kumwondolea" ukomo wa urais
 
You are controdicting yourself. Hivi miradi ya SGR Julius Nyerere Hydro power elimu bure kwa watoto wa kitanzania, maboresho ya huduma za afya, ujenzi wa mondo mbinu ya barabara, umeme na majina mengine mengi unayoyajua siyo miradi ya matokeo ya muda mrefu.? Napata shida sana kukuelewa.
Acha kutaja vitu hewa ambavyo havipo!Taja specifically hayo maboresho ya huduma za afya, ujenzi wa miundo mbinu ya barabara, umeme na majina mengine mengi ya miradi ya muda mrefu unayojinasibu nayo ni yapi hayo kwa sababu kuongelea vitu hewa ni rahisi sana!
 
Kwanza Magufuli anapendelea miradi inayomwonesha zaidi kuliko ile ambayomatokeo yake yanachukua muda mrefu kuonekana na pia hayamwoneshi yeye moja kwa moja. Mfano mzuri, hana interest kivile na kilimo, ambapo ndio kiini cha matatizo karibu yote ya kiuchumi. Sijawahi nsikia anaongelea habari ya maafisa ugani, ambao ni moja ya sababu za kukwama eneo hilo. Kujenga barabara inaonekana haraka.

Hayo uliyotaja mengi yanakadiriwa kukamilika angalau kwa kiasi kikubwa ndani ya utawala wa miaka 5 hii, kama hatawazuia wabunge "kumwondolea" ukomo wa urais
Siyo kweli. Katika kipindi chake hata supply za mbolea zinatoka kwa wakati kuliko rais yeyote. Na amekuwa akisisitiza tulime kwa bidii ili tusaidie nchi waliojifungia. Amekuwa akisisitiza kuwa hata toa chakula kwa wasiolima. Mkuu wa mkoa, wilaya, Das na viongozi wote wa eneo ambao watakumbwa na njaa wakati mvua zinanyesha wajiandae kuondoka. So viongozi wanahimizwa Na Mheshimiwa rais MagufuliJP walime na wahimize wananchi walime. Shida ni moja tu kuwa tumekuwa na viongozi wa wizara ya kilimo siyo wabunifu kutafuta masoko nje ya nchi. So kuhusu kuhimiz kilimo amejitajdi sana na hapendi wananchi wake wazulumiwe. Kumbuka issue ya korosho.


Tuseme ukweli.

Kwenye issue ya kusisitiza kujitegemea bara nzima ni nzuri sana sema wanaopokea ndo shida. Nchi kama South Africa ingechukua Hilo kama wazo kuu ingeteka soko la Afrika na tuweze kumuunga mkono. Shida weusi sisi hatuaminiani.
 
Ukitaka uelewe uharamu wa Mabeberu life span ya Waafrika na wao ni tofauti saaaana
 
Tanzania kwa Mara kwanza watafiti waliofanya kitu Chenye impact kwa jamii na dunia ni Magufuli aliyegundua kuwa hadi mapapai yakipimwa na vipimo nayo yanaonekana na corona akachallenge ubora wa vipimo vyao pili akagundua kujifukiza

Wa pili wenye utafiti wenye impact ni NIMRI waliogundua Tiba Lishe ya Corona

Hao wa vyuo stupid wala hela tu za utafiti toka uhuru wana cha maana gani cha tafiti chenye faida kwa watanzania walio wengi? heri pesa ziende kwenye miundombinu kuliko kupelekea hiyo mibwege vyuoni inayojiita utafiti kutwa kujitia kutafiti tu results na impact kwa jamii hakuna
 
Siyo kweli. Katika kipindi chake hata supply za mbolea zinatoka kwa wakati kuliko rais yeyote. Na amekuwa akisisitiza tulime kwa bidii ili tusaidie nchi waliojifungia. Amekuwa akisisitiza kuwa hata toa chakula kwa wasiolima. Mkuu wa mkoa, wilaya, Das na viongozi wote wa eneo ambao watakumbwa na njaa wakati mvua zinanyesha wajiandae kuondoka. So viongozi wanahimizwa Na Mheshimiwa rais MagufuliJP walime na wahimize wananchi walime. Shida ni moja tu kuwa tumekuwa na viongozi wa wizara ya kilimo siyo wabunifu kutafuta masoko nje ya nchi. So kuhusu kuhimiz kilimo amejitajdi sana na hapendi wananchi wake wazulumiwe. Kumbuka issue ya korosho.


Tuseme ukweli.

Kwenye issue ya kusisitiza kujitegemea bara nzima ni nzuri sana sema wanaopokea ndo shida. Nchi kama South Africa ingechukua Hilo kama wazo kuu ingeteka soko la Afrika na tuweze kumuunga mkono. Shida weusi sisi hatuaminiani.
Mkuu kwa Mara ya KWANZA NIMEPATA mbolea ya ruzuku juzi japo muda wakuitumia umeenda lakini nashukuru.
 
Comedy phase 3.

Wazungu wamefanya utafiti wa kiyasansi wewe unasema haukubaliani nao na unaagiza waganga wa jadi wafanye utafiti na baada ya wiki 2 wanakuletea vichupa vya dawa unakubali.
NIMRI ni wanasayansi sio waganga wa kienyeji

Mungu ulisoma hii comment yako atafurahi mno ni heri wazungu tuliondoka physically lakini tunaendelea kubaki vichwani mwao.Wewe ni ushahidi kuwa mkoloni bado yuko Tanzania nchi yetu bado haijapata uhuru mkoloni kahamia vichwani na huyo mkoloni aliye kichwani mwako kumtoa inahitajika watoa mapepo wakalitoe hilo pepo mkoloni kichwani kwako

Mwamposya anzisha ibada ya kutoa mapepo ya kizungu kwenye vichwa vya baadhi ya watanzaniia

Ngoja nianze Pepo mkoloni uliye kwenye kichwa cha hujui mtu toooka kwa Jina la Yesu
 
Back
Top Bottom