Msimamo wa Tanzania kuhusu Korona uliotolewa katika kikao cha Umoja wa Afrika AU ni ubabaishaji

Msimamo wa Tanzania kuhusu Korona uliotolewa katika kikao cha Umoja wa Afrika AU ni ubabaishaji

Siyo kweli. Katika kipindi chake hata supply za mbolea zinatoka kwa wakati kuliko rais yeyote. Na amekuwa akisisitiza tulime kwa bidii ili tusaidie nchi waliojifungia. Amekuwa akisisitiza kuwa hata toa chakula kwa wasiolima. Mkuu wa mkoa, wilaya, Das na viongozi wote wa eneo ambao watakumbwa na njaa wakati mvua zinanyesha wajiandae kuondoka. So viongozi wanahimizwa Na Mheshimiwa rais MagufuliJP walime na wahimize wananchi walime. Shida ni moja tu kuwa tumekuwa na viongozi wa wizara ya kilimo siyo wabunifu kutafuta masoko nje ya nchi. So kuhusu kuhimiz kilimo amejitajdi sana na hapendi wananchi wake wazulumiwe. Kumbuka issue ya korosho.


Tuseme ukweli.

Kwenye issue ya kusisitiza kujitegemea bara nzima ni nzuri sana sema wanaopokea ndo shida. Nchi kama South Africa ingechukua Hilo kama wazo kuu ingeteka soko la Afrika na tuweze kumuunga mkono. Shida weusi sisi hatuaminiani.
Suala la Kilimo lina maeneo muhimu ambayo yanatakiwa kuangaliwa ili kubaini na kupima utendaji wa serikali katika eneo husika.
Umemsifia Magufuli kwamba anahakikisha mbolea inafika muda unaotakiwa. Hiyo ni administrative , logistical issue. Hiyo ni ngazi ya chini sana. Tuanze na ngazi ya kisera. Shida namba mojakatikakilimo ni RUZUKU. serikali ya nyerere iliweka ruzuku kubwa na kuwezesha kilimo bora kiwezekane kwa mtanzania wa kawaida. sasa hivi kilimo ni business venture kubwa inayohitaji mtaji mkubwa.
Ukiangalia bajeti zetu, miundombinu huteka zaidi ya Trilioni 4, wakati kilimo ni bilioni kadhaa, na hata hizo zinazotengwa humegwa na kuongezwa kwenye miundombinu. Magufuli ana obsession na miundombinu, na ana obsession na miradi isiyo ya lazima kama Dodoma na Chato, ambayo imegharimu matrilioni mengi. Hebu fikiri hayo yote yangeingizwa kwenye kilimo?

Katika kilimo, jambo muhimu sana ni muunganiko kati ya mkulima, vituo vya utafiti, na afisa ugani. Mkulima aimarishwe kwa mafunzo na ruzuku katika pembejeo. Afisa ugani apewe mafunzo makini, vitendea kazi, maslahi bora, athaminiwe, asimamiwe. Research centers kama Ukiriguru, Uyole, Naliendele, Tengeru, Mlingano, nk., ziimarishwe na kupatiwa fedha inayotakiwa kama ilivyokuwa hapo zamani.

Enzi za Nyerere vituovvya research vililindwa sana kama mboni. Magonjwa kama ya migomba huko Bukoba yanayotamba sasa, ingekuwa kama zamani wangeshakuja na ufumbuzi. Hata hii nguvu ya GMO isingekuwepo. Tumepiga marufuku GMO, lakini kiutafiti tupo vizuri? Vituo vya utafiti vimetelekezwa.
Nadhani umeelewa kwa nini napiga kelele. Magufuli angeelekeza hasira zote kwenye kilimo, tungevuka
 
Comedy phase 3.

Wazungu wamefanya utafiti wa kiyasansi wewe unasema haukubaliani nao na unaagiza waganga wa jadi wafanye utafiti na baada ya wiki 2 wanakuletea vichupa vya dawa unakubali.
Wazungu wenyewe Wapigaji tu,usizani wanakupenda sana,wanapenda tu hicho ulichonacho!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Comedy phase 3.

Wazungu wamefanya utafiti wa kiyasansi wewe unasema haukubaliani nao na unaagiza waganga wa jadi wafanye utafiti na baada ya wiki 2 wanakuletea vichupa vya dawa unakubali.
Utafiti upi huo ambao wewe kapuku unaukubali wakati wazungu wenyewe wanapingana?


''Spain's country's health chiefs have authorised the use of the drug to inoculate people aged between 18 and 55. However, they followed France, Germany, Italy and Austria in imposing age restrictions.''
 
Siyo kweli. Katika kipindi chake hata supply za mbolea zinatoka kwa wakati kuliko rais yeyote. Na amekuwa akisisitiza tulime kwa bidii ili tusaidie nchi waliojifungia. Amekuwa akisisitiza kuwa hata toa chakula kwa wasiolima. Mkuu wa mkoa, wilaya, Das na viongozi wote wa eneo ambao watakumbwa na njaa wakati mvua zinanyesha wajiandae kuondoka. So viongozi wanahimizwa Na Mheshimiwa rais MagufuliJP walime na wahimize wananchi walime. Shida ni moja tu kuwa tumekuwa na viongozi wa wizara ya kilimo siyo wabunifu kutafuta masoko nje ya nchi. So kuhusu kuhimiz kilimo amejitajdi sana na hapendi wananchi wake wazulumiwe. Kumbuka issue ya korosho.


Tuseme ukweli.

Kwenye issue ya kusisitiza kujitegemea bara nzima ni nzuri sana sema wanaopokea ndo shida. Nchi kama South Africa ingechukua Hilo kama wazo kuu ingeteka soko la Afrika na tuweze kumuunga mkono. Shida weusi sisi hatuaminiani.
Je, hao viongozi wa Wizara ya Kilimo wasio wabunifu huteuliwaje na ni nani huwateua?
 
Mzee wetu mbona hapendi kukutana na wakubwa wenzie? !! Ni nini mbaya wana CCM hebu tuoeni ufafanuzi!!
 
Kabudi ni mchekeshaji wa mfalme
Wakati Sauli Mfalme anatawala Israeli ya kale kulikuwa na watu kazi yao ilikiwa ni kumwimbia mfalme ili afurahi na baadaye apate usingizi na wao kukiowa ujira..... ndiyo hawa sasa kina kabudi katika Tanzania ya leo.
 
Hapa namuunga mkono Pro majalala. Africa inaweza kuanzisha na kuendesha chombo kama hicho. Kila nchi ikichangia Tsh bilioni moja kila mwaka tunapata Tsh 54 bln. Hizo zinatosha kuanzisha taasisi ya kutafiti tiba na chanjo ya magonjwa yanayoisumbua Africa.
 
Tanzania kwa Mara kwanza watafiti waliofanya kitu Chenye impact kwa jamii na dunia ni Magufuli aliyegundua kuwa hadi mapapai yakipimwa na vipimo nayo yanaonekana na corona akachallenge ubora wa vipimo vyao pili akagundua kujifukiza

Wa pili wenye utafiti wenye impact ni NIMRI waliogundua Tiba Lishe ya Corona

Hao wa vyuo stupid wala hela tu za utafiti toka uhuru wana cha maana gani cha tafiti chenye faida kwa watanzania walio wengi? heri pesa ziende kwenye miundombinu kuliko kupelekea hiyo mibwege vyuoni inayojiita utafiti kutwa kujitia kutafiti tu results na impact kwa jamii hakuna
Idiot.
 
Upi kushabiki zaidi

Tanzania muda wote inafanya utafika kupitia taasisi zake kama NIMR na COSTECH kwa kuzitaja chache

Pia Vyuo vinafanya utafiti na Wizara ina kitengo cha Tiba asili kwaajili ya utafiti


Ilan ya sasa imeweka mkazo wa kipekee kwenye Tiba mbadala
COSTECH kimsingi wanafadhili tafiti, hawafanyi utafiti moja kwa moja. Ile ni Tume ya Sayansi na Tekinolojia. Kwa maoni yangu, imepitwa na wakati kimuundo, na pia haipati Bajeti ya kutosha, na ndio maana haishangazi kwamba wasomi wetu kwa asilimia kubwa wanahangaikia scholarship toka nje na sio COSTECH.

NIMRI ingeweza kusaidia, lakini tatizo vipaumbele vyetu ni nini? NIMRI wanaongozwa na sera zipi? Wanatengewa bajeti ya kutosha?

Sasa hivi kuna maendeleo makubwa sana katika sayansi ya tiba. Tunahitaji watanzania wenye vipaji wapate elimu bora katika basic science, kisha tuwapenyeze kwenye maabara kubwa za utafiti za nje, na kisha ndio tuwawezeshe hapa kwetu. Hiyo pekee inahitaji mikakati, political will, na bajeti.

Tunahitaji pia kutumia kikamilifu ujuzi wa jadi na kuuendeleza. Kweli kuna vitengo vya tafiti za dawa asili Muhimbili, nk. Lakini havijapewa umuhimu mkubwa kwa maana ya mafungu, mikakati na vipaumbele.
 
Huyo Magufuli alikinywa kikombe cha babu hakukidharau yuko mzima wa afya na ni Raisi wewe ambaye hukukinywa mbona uko choka mbaya tu maisha umepigika
Inawezekana shida zooote ndio zilianzia hapo kwenye kikombe cha babu. Ndio maana nchi inapelekwapekekwa tu
 
Tanzania kwa Mara kwanza watafiti waliofanya kitu Chenye impact kwa jamii na dunia ni Magufuli aliyegundua kuwa hadi mapapai yakipimwa na vipimo nayo yanaonekana na corona akachallenge ubora wa vipimo vyao pili akagundua kujifukiza

Wa pili wenye utafiti wenye impact ni NIMRI waliogundua Tiba Lishe ya Corona

Hao wa vyuo stupid wala hela tu za utafiti toka uhuru wana cha maana gani cha tafiti chenye faida kwa watanzania walio wengi? heri pesa ziende kwenye miundombinu kuliko kupelekea hiyo mibwege vyuoni inayojiita utafiti kutwa kujitia kutafiti tu results na impact kwa jamii hakuna
Hujui usemalo. Pale chuo kikuu Dar kuna rundo la tafiti, kweli, lakini ni nani anatakiwa kuzifanyia kazi? Hata PhD ya Magufuli kuhusu korosho, ipo pale.

Nchi za wenzetu, sekta binafsi imeimarika, inaagiza na kulipia tafiti katika vyuo vikuu, na inazinunua zile wanazohitaji.vkwa nchi yetu ni juu ya serikali kuchochea hali hiyo. Bila hivyo hatutoboi
 
Comedy phase 3.

Wazungu wamefanya utafiti wa kiyasansi wewe unasema haukubaliani nao na unaagiza waganga wa jadi wafanye utafiti na baada ya wiki 2 wanakuletea vichupa vya dawa unakubali.
Tutauona huo utafiti wa kisayansi matokeo yake Mkuu.
 
Comical Ali.

Wafanye utafiti kikombe cha babu alichokunywa Jiwe.
Na kile cha Madagascar, alichokunywa Kabuti Kalamaganda; mwokotwa 'Jalalani'.

Jambo ninaloweza kumsifia Magufuli kulifanya kwa ufanisi, ni namna anavyowaibua na kuwatambua 'comical Ali' wake na kuwaweka sehemu sitahili. Kuna yule msemaji wa serikali Abas, hata Ali waSaddam hamfikii! Na Popole je, kakalia sehemu inayomkaa vyema ndani ya CCM kwa nyakati hizi.
 
Nimemsikiliza waziri Kabudi ambaye alimwakilisha Rais Magufuli kwenye kikao cha Umoja wa Afrika. Wakati Rais Ramaphosa wa Afrika ya Kusini akiwa ni mwenyekiti anayemaliza muda wake, akieleza jinsi korona ilivyovuruga mipango ya maendeleo katika bara la Afrika, Tanzania ilitoa msimamo wake na pia kushauri Afrika ichukue msimsmo huo.

Msimamo wenyewe ni Tanzania na Afrika kwa ujumla zijiimarishe katika tafiti za chanjo na madawa ili kuondoa utegemezi kwa "mabeberu".

Sina tatizo kimsingi na hoja hiyo. Kwa kweli ni hoja nzuri tu. Tatizo langu ni kwamba hii hoja inatokana na kelele zinazopigwa na viongozi wetu hivi sasa, ili kuenda sawa na misimamo tata ya Magufuli. Kauli aina hii ndio kama anazotoa Profesa Mchembe, katibu mkuu wizara ya Afya. Na ndio zinafanya wengine wanadiriki kupiga marufuku uvaaji barakoa. Ni ujinga na ujuha wa kiwango cha pekee.

Hakuna sera ya utafiti inayotuongoza kufikia hayo anayodai Kabudi, na hata ile "political will" tu haipo. Magufuli arundike mabilioni katika elimu ya juu na utafiti? Apunguze matrilioni yanayokwenda kwenye miundombinu? Aache miradi yaje ya Chato? Wala sioni dalili ya hilo kutokea, hata kama hizo sera zingeandaliwa.

Magufuli huyu anayewafrustrate maprofesa, anayedai vyuo vikuu vitoe hela ya GAWIO serikalini ili ajenge barabara, ndio asimamie miradi ya utafiti wa chanjo za korona, ambayovinahitaji matrilioni, utaalamu wa ngazi ya cutting edge, ambao unahitaji kujengwa na kutunzwa? Sioni hata dalili.

Magufuli sio mtu wa miradi ya muda mrefu, matokeo yaje yeye kaondoka. Anataka afanye na kukamilisha sasa.

Kwa hiyo akina Kabudi na Mchembe wanapiga sound kama za yule waziri wetu mpendwa wa viwanda, aliyetufundisha kwamba hata vyerehani 4 ni kiwanda
 
Hili suala la covid-19 lina ukakasi mwingi sana:
1. Tusidanganyane hii kitu imetengenezwa, mbona dunia haizungumzii walio sababisha hili balaa
2. Kwao huko ndo madhara ya corona ni makubwa sana, kwa nn wanahimiza kila mtu achanjwe? Huoni issue ni biashara hapo.
Yako mengi ya kujiuliza mwisho wa siku raisi ana access na intelligence information. Nadhani anapo ongea anavigezo.
Ushauri:
Kama nchi moja moja tumeona udhaifu mkubwa sana kwenye sector ya afya. Ni wakati wa kuwekeza huko.
Pia tufafiti dawa asili na zitumike kitaalamu.
Kwa leo yanatosha
 
Back
Top Bottom