Phiri Hana mpira wowote kama walivyo wachezaji wengine wote wa Simba hii mbovu, Phiri akija Yanga anapelekwa Yanga B! Jana kafunga goli kindondokela tu kwa papara za kipa wa Ihefu kuwahi kutoka bila akili maana Kuna mabeki wawili wa Ihefu walikuwa wakimkaba na asingepiga! Diarra humfungi magoli ya short range kama lile, hutulia na kumsoma mfungaji!
Goli la Phiri Jana halikuwa goli la kiufundi kama yalivyo Yale magoli ya Max au Mayele!!
Hata goli la Baleke la kwanza Jana Simba vs Ihefu halikuwa la kiufundi! Na dizaini kama vile magoli ya Simba ni magoli ya kichawi! Magoli ya kichawi Huwa hayafuati formula ya goli linapatikanaje!! We utashtukia tu gooooal!! Mnabaki mnaulizana nani kafunga wakati wote mmetumbua macho mkiangalia mpira!
Simba imeshuka kiwango na kuwa sawa na timu zingine ndogo za ligi kuu, kinachoibeba ni juhudi binafsi za mchezaji mmoja mmoja, marefa na uchawi basi, ushindi wa Simba kwasasa ni wa tabu na kulazimisha. Timu zikikomaa kuifunga Simba mbovu marefa wanazilegeza!!
Ukitaka kujua mpira wa miguu ni kibarua kizito angalia mechi za Simba, ukitaka kujua mpira wa miguu ni rahisi na ni burudani angalia Yanga ikicheza na Skudu Makudubela akiwa uwanjani!!
Simba hii inapuliza kweli kweli japo haitasaidia kipigo Derby Kiko pale pale maana Yanga ni haki yetu kukaa kileleni na kubeba Tena kombe msimu wa tatu!!
Kama wewe ni mbumbumbu kolowizard na hujakereka na hii comment from utopolo og basi piga piga makofi uende peponi ila pia now now nikurushie vocha ya kujaza bando la kuingia JF!